Kodi ya kichwa irudishwe

Kodi ya kichwa irudishwe

man dunga

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2013
Posts
3,519
Reaction score
6,065
Maendeleo yanaletwa na kodi. Wanaopanga kodi gani ikusanywe kwa wananchi ni viongozi wanaochaguliwa na wananchi.

Wote tunajua hawa viongozi wanachaguliwa na raia wa mjini na vijijini ili mradi tu ana umri wa miaka kuanzia 18.

Napendekeza kodi ya kichwa irudishwe kwa kila raia kuanzia wa miaka 18 wa mjini na vijijini. Kwa sasa kodi ya kichwa ipo kwa mgongo wa VAT ambapo kwa watu wa mjini ndio wanailipa kwa kiasi kikubwa.

Watu wa mjini wanakodi lukuki wakati watu wa vijijini tunaochagua nao viongozi wengine hawajui hata neno kodi ni nini.

Kwa hiyo kodi ya kichwa irudishwe ili ikitokea kiongozi akisema ataleta maendeleo kwa unafuu wa kodi kwa raia aeleweke na raia wote na sio sasa wengine (wa vijijini) wanalipiwa kodi na wengine(wa mjini) wakati viongozi wanaoleta mamizigo ya kodi kwa raia wanachaguliwa na wote.
 
mkuu umeongea kweli ila tatizo linakuja mfumo wa kukusanya hio kodi utakuwa sio rafiki Kwa watanzania na hio kodi itakuwa ni kubwa sana ww si umeona TANESCO wameamua kufidia ela ya panga boi Kwa 1.1%.
 
Head Tax inabid wewekewe watu wavijijin na sio mjini maana sisi wa mjini japo ndo tunalipa kodi kwa wingi lakin maendeleo tunapata japo kwa uchache ...hospat tunazo shule tunazo balabala za lami tunazo...Mimi naona watu wavijijin wawekewe head tax ili angalau nawenyewe waonje laa ya hospatali nzuri na shule nzuri na lami pia.
 
Vijijini ndiyo wazalishaji wakubwa nashangaa maendeleo yanabaki mjini inakiwa kila sehemu ijiendeshe kutokana na mapato yake haiwezekani sisi tuhangaike kuzalisha maendeleo yanapelekwa dar na dodoma
 
Hiyo haiwezi tokea, kodi ya kichwa ilikuwa kodi ya kikoloni
Sio kuwa na maana!
Utakichaji kichwa kimezalisha nini, kimetoa huduma gani?
Kodi ni kwenye goods and services
Kichwa sio bidhaa wala service
 
Naunga mkono hoja.kodi irudishwe ile kasi ya maendeleo iende kwa spidi.nibora kulipa kodi yakichwa ili tupate madawa pembejeo kuboresha elimu na nk kuliko hali ilivyo sasa
 
Mtoa mada nafikiri una tatizo hasa la Kisaikolojia tafakari vizuri alafu urudi tena na andiko lako.
 
Nakuunga mguu kwa %100 maana kunamijitu iko kijijini haitambui hata kodi ninini
Mi nadhani kodi ya bichwa ikiludishwa pengine kipindi cha uchaguzi yatajitafakali Nani yampe kura
 
Kila mwezi nalipa zaidi ya 19% kama PAYE. achilia mbali indirect taxes ninazolipa kwenye kila bidhaa ninayotumia kila siku. Na ndio maana rais anapata jeuri ya kufuja kodi zangu na kwenda kununua ndege kama unavyonunua gazeti.
Wakileta na kodi ya kichwa basi kutakua na haja ya kuanzisha ka 'M23' ketu hapa nchini ili tuheshimiane
 
Back
Top Bottom