Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Klabu ya Simba 'Wekundu wa Msimbazi' ya jijini Dar es salaam, leo imemtambulisha rasmi kocha mpya Mbelgiji Patrick Aussems, ambaye anatarajia kuifundisha klabu hiyo kuelekea kwenye maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara sambamba na michuano ya Kimataifa.
Kocha Aussems amesaini mkataba wa mwaka mmoja mbele ya Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah (Try Again) pamoja na Kaimu Makamu Rais Idd Kajuna, kukinoa klabu hiyo akichukua nafasi ya Pierre Lechantre raia wa Ufaransa aliyemaliza muda wake mwezi uliopita.
Kocha Aussems amesaini mkataba wa mwaka mmoja mbele ya Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah (Try Again) pamoja na Kaimu Makamu Rais Idd Kajuna, kukinoa klabu hiyo akichukua nafasi ya Pierre Lechantre raia wa Ufaransa aliyemaliza muda wake mwezi uliopita.