Koboko (black mamba) ana kiburi, jeuri na dharau sana ila nitamfundisha adabu

Mkuu huyu tumeshawahi kuwakurupusha mara nyingi, utakuta ukienda chooni usiku unamkuta kajinyoosha kwenye paa huku kichwa kakiweka kama anataka kukining'iniza hivi

Ilifikia kipindi ikawa kuingia chooni mwisho saa kumi na moja jioni na asubuhi inabidi uingie saa moja jua likiwa limechomoza

Tulivyoona hivyo ndo tukachukua ile chumvi ya mawe ( yenye mabonge mabonge isipitia kiwandani )
Tukakoleza moto wa kutosha kisha tukamwaga kama kiganja kimoja hivi sasa bwana ilipoanza ile Ta ta ta ta ta tukaona jamaa anajiseti kwanza hapo wote tulikua tumejihami na maji ya moto kusema kua ukiona anakufata tu mmwagie aungue kidogo kisha tumuue alivyotoka hapo hizo mbio nilikubali, nikajikuta naanza mazoezi ya kukimbia ili kujiandaa kama siku akinitoa nduki
koboko hana tatizo kama hakuwahi bughudhiwa au jeruhiwa,na hatembei usiku..ila kwa chumvi hata cobra hakimbii
[/QUOTE
 
Hivi hakuna dawa ya kufanya famigesheni kuwahamisha hao wadudu?
 
Je alihama?
 
We una wazimu wewe__koboko huyu huyu mzee wa kutafuna bangi...au unamzungumzia yupi???, kama ni huyo atakumaliza wewe''ni mwehu yule;oohooooo!!!

Smart guy
 
Shida yote ya nini mzee... Tafuta hawa wadau .. Wakikuta umeua nyoka wanaumia sana.
 
Hii thread imekaa kama vile TWITI ZA NAPE NNAUYE KULE twitter.
Isije ikawa kuna fumbo fulani hapa!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…