Kiwanja cha kanisa apewa mwekezaji - walaaniwe!

Kiwanja cha kanisa apewa mwekezaji - walaaniwe!

idumu

Member
Joined
Jun 5, 2009
Posts
44
Reaction score
1
Kama jana uliona taarifa ya habari ya ITV, Kweli dunia inaelekea ukingoni. Kama kanisa lina 40 years kwenye kiwanja leo mwekezaji anakuja kuchukua kiwanja. Is True?? Nani ana data za uhakika kuhusu hicho kiwanja, Nani anamiliki??

Bless
 
Hivi yule Jerry Muro wa ITV na Pastor Anta Muro ni ndugu maana Jerry Muro huwa ana-cover habari za kanisa hilo mara ya pili sasa kisha zinachukua muda mrefu. Ningependa haswa kusia stori ya upande wapi pili. Ila kama ni kweli stori ilivyoelezwa na Muro jana, basi si haki mfanyibiashara huyo anavyofanya.
 
Rushwa inaitafuna nchi hii taratibu kama vile kansa inavyomtafuna mgonjwa. Nakumbuka kipindi kile mafisadi walipovamia kiwanja cha Mwalimu JK Nyerere (RIP) hadi rais akaingilia kati, sasa itakuwa hiki cha kanisa? sasa hivi kila mtu anajiona yuko juu ya sheria can do anything. Nchi inapotea na kukosa mwelekeo
 
Ila inasikitisha sana! Kama wamekuwa wanamiliki kwa more than 30 years na aliekuwa Askofu aliishi kwenye ile nyumba iweje tena wao waseme wamepewa na mahakama? Au walikiweka rehani? Anyway tuombe Mungu haki itendeke.
 
Jamani si wote tunaoangalia ITV, hivyo unapoleta habari jitihidi kuielezea ili msomaji yeyote apate kuelewa.
 
Hivi yule Jerry Muro wa ITV na Pastor Anta Muro ni ndugu maana Jerry Muro huwa ana-cover habari za kanisa hilo mara ya pili sasa kisha zinachukua muda mrefu. Ningependa haswa kusia stori ya upande wapi pili. Ila kama ni kweli stori ilivyoelezwa na Muro jana, basi si haki mfanyibiashara huyo anavyofanya.

Usijadili mtu, jadili habari yenyewe, pls.
 
Usijadili mtu, jadili habari yenyewe, pls.

Swali nililouliza ni la msingi, kwa upeo wako nadhani hujanielewa. Kuuliza kuwa Jerry Muro wa ITV na Pastor Anta Muro kama ni ndugu, maana yake ni kuwa; Narrator (Jerry Muro) anaweza kuwa na upendeleo kwa kuwa labda kesi inahussha dhehebu lake. Au mchungaji husika ni kaka yake. It is imparative to establish whether the narrator was bias or not, by so doing we will be able to determine the credibility of the story. Upo?
 
Swali nililouliza ni la msingi, kwa upeo wako nadhani hujanielewa. Kuuliza kuwa Jerry Muro wa ITV na Pastor Anta Muro kama ni ndugu, maana yake ni kuwa; Narrator (Jerry Muro) anaweza kuwa na upendeleo kwa kuwa labda kesi inahussha dhehebu lake. Au mchungaji husika ni kaka yake. It is imparative to establish whether the narrator was bias or not, by so doing we will be able to determine the credibility of the story. Upo?
Kwa hiyo asiripoti kwa kuwa dhuluma inafanywa kwa kaka yake na yeye ni ripota?

Hii si hoja. Hoja hapa ni kwamba where is the law in this country? Kweli yaani mwekezaji aje tu achukue ardhi hata kama nimeimiliki mwezi tu, bila ridhaa yangu?
Something behind is boiling now. Tuwe macho na serikali hii.

Mimi nilitegemea serikali imuombe mwekezaji akazungumze na mwenye kiwanja ili wa compromise either alipe pesa au waingie ubia kwa mtaji wa kiwanja chake. Hapa ndipo tunaweza kuijua serikali makini yenye nia njema kwa wananchi wake.

Si hivyo hakuna lolote. Umasikini juu ya umaskini. hawa mafisadi akikitamani kiwanja chako anamtafuta mtu anaitwa mwekezaji(Kama walivyofanya kwa trl,ttcl,nasaco etc etc), na wanakufanyia dhuruma.
 
Kwa hiyo asiripoti kwa kuwa dhuluma inafanywa kwa kaka yake na yeye ni ripota?

Hii si hoja. Hoja hapa ni kwamba where is the law in this country? Kweli yaani mwekezaji aje tu achukue ardhi hata kama nimeimiliki mwezi tu, bila ridhaa yangu?
Something behind is boiling now. Tuwe macho na serikali hii.

Mimi nilitegemea serikali imuombe mwekezaji akazungumze na mwenye kiwanja ili wa compromise either alipe pesa au waingie ubia kwa mtaji wa kiwanja chake. Hapa ndipo tunaweza kuijua serikali makini yenye nia njema kwa wananchi wake.

Si hivyo hakuna lolote. Umasikini juu ya umaskini. hawa mafisadi akikitamani kiwanja chako anamtafuta mtu anaitwa mwekezaji(Kama walivyofanya kwa trl,ttcl,nasaco etc etc), na wanakufanyia dhuruma.


Mimi ni Mkristo kabisa ila naamini sana haki. Kumbuka mtangazaji alisema kuwa fisadi husika alivunja nyumba ya Askofu wakati ndugu wa fisadi alikanusha na pia polisi aliyekuwepo alikanusha kuvunjwa kwa nyumba. Ukiangalia kwenye TV utaona mawe mengi yakiashiria uvunjaji wa nyumba wakati yale mawe nadhani sio ya uvunjaji wa karibuni. Usishabikie tu hivi hivi bila kujua stori kwa kina. Ilikuwaje mpaka fisadi huyo akachukua hiyo sehemu. Mimi nikitangaza stori ya kaka yangu au dada yangu lazima niwe na hisia sometimes upendeleo kwa mbali. Kutokana na majibu yenu inaonyesha wazi kuwa Jerry Muro na Mchungaji Anta Muro ni ndugu. Tafadhali msitafute mashabiki kwa lazima huku hamtaki kueleza stori kamili, sisi ni watu na akili zetu tunachambua vitu kwa makini kabla ya kushabikia ndio maana hatukujiunga na DECI japokuwa ililetwa kwa kutumia mgongo wa Dini.
 
Back
Top Bottom