Kiwango cha uzazi dar chapungua

101 East

JF-Expert Member
Feb 25, 2015
1,040
2,121
Moja kati ya taarifa kubwa kuanzia Wiki iliyopita hadi Wiki hii ni taarifa ya uzazi na visababishi vyake kutoka kwenye Ripoti ya Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria ya 2022 iliyozinduliwa hivi karibuni na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ripoti hiyo inaonesha kuwa utafiri kwa kulinganisha Mikoa umeonesha Wanawake wa Dar es salaam kiwango chao cha uzazi kipo chini kwa wastani wa Watoto 2.8 kwa kila Mwanamke huku Wanawake wa Mkoa wa Simiyu kiwango chao cha kuzaa kikiwa juu kwa wastani wa Watoto 6.6 kwa kila Mwanamke.

Wanawake wa Arusha kiwango chao ni wastani wa Watoto 4.7 kwa Mwanamke, Mwanza ni wastani wa Watoto 4.9, Tanga Watoto 5.2 kwa kila Mwanamke, Mbeya Watoto 4.3, Iringa Watoto 3.9 na Njombe wastani wa Watoto 4.0.

Ripoti hiyo inaonesha Wanawake wanaoishi katika maeneo ya Vijijini wana uwezo wa kuwa na Watoto wengi kuliko Wanawake wa maeneo ya mijini (wastani wa Watoto 5.5 dhidi ya 3.6 mtawalia).
 
Tatizo single mothers kwa sasa kukuta mwanamke ana miaka 40 na ana mtoto mmoja ni kawaida halafu ni single mother haswa Dar..

Lakini kweny ndoa wakikaa miaka 10 basi tambua ni watoto kuanzia watatu...
 
Kwa nyakati hizi bora kuwa na watoto wachache sana dunia ishabadilika mambo mengi yamekuwa tafrani unamleta mtoto duniani kula raha au kuteseka tu? Dunia ya sasa hivi ipo overpopulated with low resources, ina magonjwa ya kutosha, maisha magumu n.k yaani nikiwaza hivyo nafikiri ntakuwa na mtoto mmoja au wawili stoooooop!
 
Kwa nyakati hizi bora kuwa na watoto wachache sana dunia ishabadilika mambo mengi yamekuwa tafrani unamleta mtoto duniani kula raha au kuteseka tu? Dunia ya sasa hivi ipo overpopulated with low resources, ina magonjwa ya kutosha, maisha magumu n.k yaani nikiwaza hivyo nafikiri ntakuwa na mtoto mmoja au wawili stoooooop!
Hii pia ni point ✍️
 
Kampeni ya kataa ndoa naona inaenda vizuri.

Kwa takwimu hiyo ipo sahihi kabisa. Pia wangetoa takwimu ya single mothers ilivyopaa kwa mkoa wa Dar-es-salaam ingesaidia kutoa alert.

Nashauri wanawake na wao waje na kampeni ya kataa ujauzito.
 
Moja kati ya taarifa kubwa kuanzia Wiki iliyopita hadi Wiki hii ni taarifa ya uzazi na visababishi vyake kutoka kwenye Ripoti ya Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria ya 2022 iliyozinduliwa hivi karibuni na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ripoti hiyo inaonesha kuwa utafiri kwa kulinganisha Mikoa umeonesha Wanawake wa Dar es salaam kiwango chao cha uzazi kipo chini kwa wastani wa Watoto 2.8 kwa kila Mwanamke huku Wanawake wa Mkoa wa Simiyu kiwango chao cha kuzaa kikiwa juu kwa wastani wa Watoto 6.6 kwa kila Mwanamke.

Wanawake wa Arusha kiwango chao ni wastani wa Watoto 4.7 kwa Mwanamke, Mwanza ni wastani wa Watoto 4.9, Tanga Watoto 5.2 kwa kila Mwanamke, Mbeya Watoto 4.3, Iringa Watoto 3.9 na Njombe wastani wa Watoto 4.0.

Ripoti hiyo inaonesha Wanawake wanaoishi katika maeneo ya Vijijini wana uwezo wa kuwa na Watoto wengi kuliko Wanawake wa maeneo ya mijini (wastani wa Watoto 5.5 dhidi ya 3.6 mtawalia).
Sio Dar tuu Bali Tanzania nzima.

Aidha hata population growth rate ya Dar imepungua kiasi kwamba Iko chini kabisa ya wastani wa kitaifa.

Sababu ziko nyingi ila mojawapo ni hiyo ya kupungua Kwa uzazi na pia kubwa zaidi ni kwamba watu wameacha kushoboka na Dar.

You can earn life popote pale

Mwisho impacts ya Elimu kiujumla Huwa inapelekea wanawake kupunguza uzazi.
 
Back
Top Bottom