kiwanda cha TANZANIA MACHINE TOOLS nani anakitafuna?

kiwanda cha TANZANIA MACHINE TOOLS nani anakitafuna?

Joined
Jan 1, 2012
Posts
21
Reaction score
3
kiwanda hiki kipo kilimanjaro(w)Hai,chini ya PSRC ni miaka mingi hakizalishi na hakuna anayewajibika walau kutaka kujua nini? Kinaendelea, wakati kilikuwa mkombozi wa wanahai ambao wanaeneo dogo sana la kilimo hekta 46,506 sawa na asilimia 46 lingine ni misitu na miamba.hiki kiwanda ni kitagauchumi muhumu sana,wadau kama mpo mnausika tazameni hili linaathiri sana uchumu na pata la halmashauri ambalo lipo chini ukilinganisha na idadi ya watu 167097(sensa 2002) na pato la 68624368.74(2008/2009,huu ni mfano mdogo tu bado hujagusa ajiri.ni hatari
 
Usishangae kuskia kuna wakurugenzi na wanahudhuria semina huku wakijilipa posho huku kiwanda hakizalishi kitu!
Hii ndo Tanganyika bana!
 
Mkuu, umefikiria jambo la maana sana mkuu.
lakini unajua viwanda vya caste iron na fabrication ya iron vilikuwa vingapi Tanzania?

mimi najua viwili tu, kimoja ni Moshi machine tools, na kingine kilikuwa Ulanga.

ilikuwa kazi ya Nyerere..............mzee wangu alikuwa anachongesha spare za lorry lake hapo, spare za mandolini alikuwa anachongesha hapo pia.

wahuni wamekiua kiwanda ili wafanye biashara za spare za machines including magari kuwa ghali, na kuanzisha biashara ya used spare parts..............UHUNI mtupu!!!

ukiachilia mbali economic value ya kiwanda tajwa kwa wilaya ya Hai, uwepo wake ungelikuwa na economic vlue kubwa sana kwa nchi hii.......spare zote za mitambo na magari zingeweza kutengenezwa hapo.......at least karibia zote.

sasa hivi watu wananunua tyre rod end ya used..........si kifo hiki.

Watu wangelijua ni kwa nini CCM haitakiwi kuwepo.......hata as a political party, nchi hii ingeendelea sana.
 
Usishangae kuskia kuna wakurugenzi na wanahudhuria semina huku wakijilipa posho huku kiwanda hakizalishi kitu!
Hii ndo Tanganyika bana!

The hunter nimecheka sana na hii comment yako japo ni suala la kusikitisha na kuhuzunisha.Kweli Tanganyika ni zaidi ya uijuavyo.
 
Hiyo Machine Tools iko mbali, kuna hicho cha Urafiki, kuna wafanyakazi kibao, wachina ndo wengi ajabu angalia production kama ipo, namjua jamaa mmoja pale alisomeshwa China kwa kodi ya wazalendo wa nchi hii, yeye dili zake ni kupangisha zile kota kwa wafanyabiashara wakubwa, utafkiri ndo alichoenda kusomea China.
Wamemaliza dili kupangisha nyumba wakarudi za kuuza machine za kiwanda wakijifanya vyuma chakavu.
Hii ndo bongo na Tanganyika ya Jey Keyi
 
kufa kwa manufacturing industry ni janga ktk africa nzima ili kudumisha ukoloni mpya wa kutegemea bidhaa kutoka nje, maendleo halisi ni yale ya mtu kuweza kujizalishia kitu chake mwenyewe na hapo ndio wazungu walipotukalia kooni hatutaweza kujikwamua! hata ukichukua loan au iwe msaada kwa mabwana wa wakubwa pesa hizo hazitakiwi zikatumike kwenye manufacturing industry, pesa hizo ni za kujenga barabara au zahani tu ushaona pesa ya msaada imejenga kiwanda au pesa ya msaada au loan inaenda kuwekeza hapana tunalazimishwa kwa hiyo hii jitamba ya serikali kua inajenga mabarabara nchi nzima ni kwa sababu wamelazimishwa kufanya hivyo!
 
Hiki kiwanda sidhani kama baada ya kuazishwa kilifanya kazi kwa zaidi ya mwaka mmoja. Viwanda kama hivi vilipaswa kuwa engine ya maendeleo ya nchi kiuchumi. Ingawa ujenzi wa kiwanda katika eneo hili la Hai mahali ambapo hamna reli ni swala la ku-question.
 
kufa kwa manufacturing industry ni janga ktk africa nzima ili kudumisha ukoloni mpya wa kutegemea bidhaa kutoka nje, maendleo halisi ni yale ya mtu kuweza kujizalishia kitu chake mwenyewe na hapo ndio wazungu walipotukalia kooni hatutaweza kujikwamua! hata ukichukua loan au iwe msaada kwa mabwana wa wakubwa pesa hizo hazitakiwi zikatumike kwenye manufacturing industry, pesa hizo ni za kujenga barabara au zahani tu ushaona pesa ya msaada imejenga kiwanda au pesa ya msaada au loan inaenda kuwekeza hapana tunalazimishwa kwa hiyo hii jitamba ya serikali kua inajenga mabarabara nchi nzima ni kwa sababu wamelazimishwa kufanya hivyo!
Hii maana yake hatuko huru..kuna sababu gani ya kujiita Taifa huru na kisha kutumia gharama kubwa katika sherehe za uhuru...!!!???
 
kile kiwanda kilikuwa kinauwezo wa kutengeneza a single wood machinery yenye seven operations

very sad to see the defunct tools & machines manufacturing industry at moshi
 
Back
Top Bottom