Kiwanda cha nguo Urafiki kimekufa?

Kiwanda cha nguo Urafiki kimekufa?

Mitsubish

Member
Joined
Apr 26, 2018
Posts
85
Reaction score
58
Nimestuka Jana nimefika kutembelea jamaa nyumba za urafiki pale Ubungo, nikashangaa kusikia toka mwezi wa 12 wafanyakazi walipumzishwa likizo, hii Leo tunaenda June bado hakuna dalili za kuitwa kazini, mini kinaendelea?

Kiwanda hiki kilipewa mwekezaji wa kichina miaka kadhaa iliyopita. Nakumbuka enzi za baba wa taiga palikua na shift tatu, jumla ya wafanyakazi 7000, uzalishaji ilikua 24hrs, walizalisha mpaka wafanyakazi wakagawana bonasi.

Walikua na Maduka makubwa kiwandani na mjini, usafiri wao binafsi wa mabasi, Fire, hospital, shule, ukumbi, vikundi vya burudani, ngoma, Band ya dansi, timu za mpira wa miguu netball na hata timu ya ndondi, vyote vilikwenda na walipata posho zao walilipwa likizo na bado kiwanda kikasafirisha nje-export-na kujipatia faida kubwa na bonasi juu.

Tunaomba Serikali ifuatilie kwa karibu kiwanda hiki mama cha nguo nchini.
 
Nimestuka Jana nimefika kutembelea jamaa nyumba za urafiki pale Ubungo,nikashangaa kusikia toka mwezi wa 12 wafanyakazi walipumzishwa likizo,hii Leo tunaenda June bado hakuna dalili za kuitwa kazini,mini kinaendelea?
Kiwanda hiki kilipewa mwekezaji wa kichina miaka kadhaa iliyopita
Nakumbuka enzi za baba wa taiga palikua Na shift tatu,jumlavya wafanyakazi 7000,uzalishaji ilikua 24hrs,walizalisha mpaka wafanyakazi wakagawana bonasi!walikua Na Maduka makubwa kiwandani Na mjini, usafiri wao binafsi wa mabasi,fire,hospital,shule,ukumbi,vikundi vya burudani,Ngoma,Band ya dansi,timu za mpira wa miguu netball Na hata timu ya ndondi,Vyote vilikwenda Na walipata posho zao walilipwa likizo Na bado kiwanda kikasafirisha nje-export-na kujipatia faida kubwa Na bonasi juu
Tunaomba serikali ifuatilie kwa karibu kiwanda hiki mama cha Nguo nchini.
Acheni kumdhalilisha rais wa viwanda
 
Huu uzi umeuanzisha kichochezi. Habari yoyote inayoonyesha mambo hasi dhidi ya agenda kuu ni uchochezi
 
Huku kiwanda kiiwasaidia sana wazee wetu walikuwa uhakika Wa kazi Ila dah! Imebaki aibu tu
Nalog off
 
Sasa viwanda ambavyo tuko bize navyo ni vipi? Wiki kadhaa zilizopita nilipita maduka ya kanga kariakoo, kanga za urafiki hamna, zipo za Nida tu
 
Kitakufaje wakati Tuko kwenye awamu ya viwanda

OvA
 
Mitumba mwisho Disemba. Viwanda vyetu vizalishe nguo mpya za kutosha na sio kuagiza nje. Kuvaa nguo zilizokwishavaliwa na wazungu ni kujidhalilisha utu wetu.
 
Mchakato wa ufufuaji wa viwanda unaendelae kwa kasi nchi nzima, viwanda vya nguo vikiwa vimepewa kipaumbele kwa nia ya kuwezesha wakulima wa hapa nchini kupata soko la huakika la uuzaji wa pamba yao.Lakini kubwa kuliko nimemsikia Waziri mwenye zamana na Viwanda akiweka msisitizo kuzuia uingizaji wa mitumba nchini na kupiga kodi kubwa kwa importations zote za nguo toka nje, hili kuvipa nguvu viwanda vya ndani, hii ni hatua kubwa sana ktk kukuza viwanda vya ndani ingawa inachangamoto zake.
 
Mitumba mwisho Disemba. Viwanda vyetu vizalishe nguo mpya za kutosha na sio kuagiza nje. Kuvaa nguo zilizokwishavaliwa na wazungu ni kujidhalilisha utu wetu.
Sure mkuu,"hata kuomba misaada na kukopa fedha nje ni kujidhalilisha tunataka kuwa donor country" alisema hivyo..kilichotokea daah anajua mwenyewe
 
Back
Top Bottom