Kiwanda cha nguo Urafiki kimekufa?

Kiwanda cha nguo Urafiki kimekufa?

Mpaka sasa awamu hii imeshajenga zaidi ya viwanda elf tano....kwaiyo hicho kikifa amna shida tushajenga vingi....na vimetoa ajira kwa watanzania wa kutosha...

kwa sasa Tatizo la ajira limepungua vya kutosha....Uchumi umeongezeka mfumko wa bei umeshuka...wananchi wanafurahia maisha....Tuendelee kumuunga mkono mheshimiwa ndugu zangu.
 
Viwanda kibao vimekufa ndani ya miaka hii mitatu...mpaka 2025 tutakua na viwanda vya beer, sigara na kampuni za kubeti tu maana Sera na sheria za nchi yetu zinalenga kukomoa wafanyabiashara na sio kuwawezesha....

Wale kula kulala nyumbani wasiojua hata bei ya nyanya sokoni inauzwaje ndio wanaoshangilia utendaji wa sasa
 
Nimestuka Jana nimefika kutembelea jamaa nyumba za urafiki pale Ubungo, nikashangaa kusikia toka mwezi wa 12 wafanyakazi walipumzishwa likizo, hii Leo tunaenda June bado hakuna dalili za kuitwa kazini, mini kinaendelea?

Kiwanda hiki kilipewa mwekezaji wa kichina miaka kadhaa iliyopita. Nakumbuka enzi za baba wa taiga palikua na shift tatu, jumla ya wafanyakazi 7000, uzalishaji ilikua 24hrs, walizalisha mpaka wafanyakazi wakagawana bonasi.

Walikua na Maduka makubwa kiwandani na mjini, usafiri wao binafsi wa mabasi, Fire, hospital, shule, ukumbi, vikundi vya burudani, ngoma, Band ya dansi, timu za mpira wa miguu netball na hata timu ya ndondi, vyote vilikwenda na walipata posho zao walilipwa likizo na bado kiwanda kikasafirisha nje-export-na kujipatia faida kubwa na bonasi juu.

Tunaomba Serikali ifuatilie kwa karibu kiwanda hiki mama cha nguo nchini.
Kinachoshangaza Je watu wanaovaa hizo kanga hawapo? (Soko) je malighafi haipo ? (Pamba). Je watu wa kufanya kazi hawapo? Kama vyote hivi vipo ni wapi sisi kama Watanzania Tunashindwa?
Je kuna watu wanatuhujumu kwa maslahi yao wenyewe?

Kwanini iwe sisi tu ?
 
Back
Top Bottom