DASA
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 1,031
- 301
Kwa asilimia kubwa wizi wa magari maeneo ya UDSM na maeneo jirani ya hapo unafanywa na polisi wa kituo hiki kama sio wenyewe binafsi ni kwa kushirikiana na watu wanaowajua wao.
Dada mmoja kwa jina la Jackline komba aliibiwa gari aina ya suzuki swift maeneo ya Engineering january 16 ikiwa imepita takriban kama wiki moja tangu dada mwingine aibiwe gari aina ya Escudo maeneo hayo hayo. Huyu dada alipotoa taarifa kituo cha polisi baada ya muda polisi hao hao walikuwa wanampigia simu kwamba gari lake wanalo na ili alipate awapelekee kiasi cha shilingi milioni 3, lakini alipowaomba kwamba ana 2.5 walimkubalia azipeleke. Huyu Dada alishtuka akaenda kutoa taarifa Kituo cha urafiki na ndipo walipotengeneza mtego na kuwakamata askari hao kwenye baa maeneo ya makaburini. Afande aliyekamatwa anaitwa afande Lufefe na mwingine kwa jina la Davis kutoka makao makuu.
Hichi kituo cha polisi watu wamekosa imani nacho sababu wanashirikiana na hao majambazi kama sio kuiba wenyewe.
Source: Nipashe la jana.
Dada mmoja kwa jina la Jackline komba aliibiwa gari aina ya suzuki swift maeneo ya Engineering january 16 ikiwa imepita takriban kama wiki moja tangu dada mwingine aibiwe gari aina ya Escudo maeneo hayo hayo. Huyu dada alipotoa taarifa kituo cha polisi baada ya muda polisi hao hao walikuwa wanampigia simu kwamba gari lake wanalo na ili alipate awapelekee kiasi cha shilingi milioni 3, lakini alipowaomba kwamba ana 2.5 walimkubalia azipeleke. Huyu Dada alishtuka akaenda kutoa taarifa Kituo cha urafiki na ndipo walipotengeneza mtego na kuwakamata askari hao kwenye baa maeneo ya makaburini. Afande aliyekamatwa anaitwa afande Lufefe na mwingine kwa jina la Davis kutoka makao makuu.
Hichi kituo cha polisi watu wamekosa imani nacho sababu wanashirikiana na hao majambazi kama sio kuiba wenyewe.
Source: Nipashe la jana.