Kituo cha Polisi Mlangali-Ludewa,njombe ni kitovu cha rushwa

Fall Army Worm

JF-Expert Member
Jan 8, 2015
19,322
14,244
Wakuu natumai mnaendelea vizuri na kusukuma gurudumu la maendeleo ya Taifa.

Kama kichwa kinavyoeleza,Kituo cha Polisi cha Mlangali,Kata ya Mlangali,Katika Wilaya ya Ludewa iliyoko mkoa wa Njombe,pana nuka rushwa.Iko hivi hawa jamaa wakimkamata raia na kosa lolote lile hata km ni dogo namna gani watamuweka ndani halafu kutoka ni hadi utoe pesa ambayo haina risiti.Najua mtaniuliza kwanini hujapeleka kunako husika ??,Je,JF itaweza kukusaidia kutatua changamoto hiyo?

Kama kuna hoja ya namna hiyo ni kwamba hadi wilayani wanafahamu tatizo hilo,OCD anajua lkn hamna utatuzi,Naleta hapa JF ili kuuhabarisha umma wa Watanzania ujue kuwa kuna Askari wanaotumia vibaya nafasi zao kunyanyasa raia na kujipatia pesa kwa njia ya rushwa.Hebu niende kwenye visa na mikasa ya hao Polisi.

Kuna matukio kadhaa yanawapata ndugu zangu na watu wengine ambapo kwa kweli yanatia simanzi.

TUKIO LA KWANZA.
Kuna jamaa mmoja,ambaye si ndugu yangu,ila nilimfahamu kwa vile alikuwa ni Fundi simu,hivyo tulifahamiana kupitia kunitengezea simu,huyu alipelekewa simu na mteja ili aifrash,kumbe simu ile ilikuwa imeokotwa,yule aliyeipoteza alipoanza kufuatilia trend ya wahusika wakamkata na yule fundi simu,kutoka wakamdai 50,000/=,yule akawauliza Polisi kosa lake ni lipi?,maana ile ni ofisi na inajulikana na Serikali kuwa yeye ni Fundi simu na hata Polisi wenyewe huwa wanaenda kufrash hapo.Ile ishu aliingilia kati Afisa tarafa akaamuru yule jamaa arudishiwe pesa yake.

TUKIO LA PILI
Juzi kuna jamaa wamweka ndani kwa kesi isiyo na kichwa wala miguu,kiasi kwamba Polisi wenyewe wanatofautiana,wapo waliosema hapa hamna kesi na wengine kuna kesi, kikubwa walikuwa wakidai pesa ,sasa jamaa yule alikuwa na pesa kidogo yaani Polisi wale hawana hata mshipa wa aibu,walisikika wakisema pesa ni kidogo mno tutagawanaje?,tupo wengi.Jamaa akampigia simu OCD,wakapelekwa Wilayani huko wakakutanishwa na OC-CID na yeye hali ikawa hivyo hivyo,anasema jamaa wameniletea dili kwa hiyo lazima utoe pesa ya kutosha kuwagawia na wenzangu,na kwamba asipofanya hivyo basi atamfunga miaka saba jela au kumtengenezea kosa kubwa zaidi,Ili bidi jamaa zimtoke.Kwa hiyo Askari wale wote ni kitu kimoja,kuanzia wale wakubwa hadi wadogo.Lakini kitu kinachostaabisha zaidi ni jinsi hawa Polisi wanavyoweza kuomba rushwa waziwazi na kisha kugawana fedha hizo waziwazi bila woga,hadi mtoto mdogo anajua kabisa jamaa wanakula rushwa na wanagawana.
Hayo ni matukio mawili niliyoyasimulia kimuhtasari tu.Yapo mengi,ambayo nikisema niyaeleze hapa yote nitajaza Seva.

NINI NAFIKIRIA KUKIFANYA??
Kwa kuwa wananchi wengi wa Mlangali ni waoga,wanawaogopa wale Polisi,Mimi nataka kujitoa mhanga,Siogopi chochote wala yeyote Ila Mungu tu mwenye uwezo na mamlaka juu ya pumzi yangu,yeye awezaye kuua mwili na Roho;Nataka kuwa mkombozi kwao,Maana hakuna kitu ninakichukia sana ktk maisha km dhuluma,nasema hivi najitoa mhanga sina cha kupoteza,Ninasubiri waingie kwenye 18 zangu halafu wanidai rushwa, mimi nitakubali halafu nitawapigia TAKUKURU makao makuu,maana sina Imani na TAKUKURU ya Ludewa.Halafu nione je na Makao Makuu nao watapuuzia?,wakipuuza nitatafuta kila namna niende kwa Rais.Kwasababu Ikulu sio mbinguni,ni duniani na ipo kwaajili yetu.Huo ndio mpango wangu,nina hasira za kufa mtu,siwezi kuvumilia uonevu huu.Najua ktk kufanya hivyo kuna watu watapata madhara matharani wategemezi wa wahusika lkn sina namna.

WITO WANGU KWA JESHI LA POLISI
Askari Polisi msitumie vibaya madaraka yenu,hiyo kazi ni dhamana tu.Vitendo vyenu vya unyanyasaji ndivyo vinavyofanya raia tuwachukie ninyi.Mfano mmoja kule Ngara Mwanajeshi alipata ajari ya gari ambapo raia waliokuwa karibu wangemnusuru mapema angeweza kuokoa maisha, lkn jamaa walipochungulia kwenye gari na kuona ni mjeda,walisema acha afe,hatumsaidii Kwasababu ya uoenezi waliokuwa wanawafanyia.Ninyi sio miungu watu.Kutokana na dhuluma mnazozifanya na manung'uniko ya hao wanaodhulumiwa wengi wenu mkistaafu huwa mnakuwa na hali mbaya,nina Ushuhuda huo,wa Askari mmoja aliyekuwa OCD baada ya kustaafu maisha yalimwendea kombo sana hadi sasa ukimwona huwezi amini maana hadi funza wameota miguuni.Binafsi siwaombei mabaya lkn acheni kunyanyasa watu wanyonge,hizo fedha za dhuluma hazitawafikisha popote.Ombi langu kwa IGP Sirro,ni kwamba juhudi ulizozionyesha ktk kudhibiti wahalifu nchini,zionyeshe pia ktk kudhibiti nidhamu ya Askari wako nchini,Namsifu sana Mwema aliyeanzisha Polisi jamii ili kuondoa uhasama kati ya Polisi na mwananchi.
Maisha sasa hivi magumu sana,fikiri ikiwa wewe mwenye mshahara unaona hali ni ngumu,vipi kwa yule mkulima hokhe!hakhe!,hali ikoje?,halafu bado unambambikizia kesi ili akupe rushwa.Kweli wananchi wapo sahihi kutomsaidia Askari hata km anakata roho.Mjue pia mnafanya Wananchi waichukie Serikali Kwasababu ya huo mchezo wenu mchafu.
Ni matumaini yangu,kuwa nimeeleweka.Nasisitiza siogopi chochote,nimetoka mavumbini,nitarudi Mavumbini,na Kila nafsi itaonja mauti.


ALAMSIKI
 
Asante kwa kuibua haya aisee wewe ndio mzalendo. Shida ya haya majamaa yanayovaa mashati ya kijani wanafikiri kumtetea magufuli ndio uzalendo. Hapo IGP Sirro apate ujumbe huu wanalichafua jeshi la polisi
 
Asante kwa kuibua haya aisee wewe ndio mzalendo. Shida ya haya majamaa yanayovaa mashati ya kijani wanafikiri kumtetea magufuli ndio uzalendo. Hapo IGP Sirro apate ujumbe huu wanalichafua jeshi la polisi

Lakini mkuu umesahau kuwa kuna kuwapa senti ya kung'arisha viatu kwa kiwi na haiitwi rushwa? hata hivyo tatizo hili la kubabikia watu inaelekea huko ni sugu sana kwani hoja za mlalamikaji zimenikumbusha bwana mmoja alisamehewa na Rais JPM naye alikuwa kutoka Njombe na alipewa kesi ya kichwa na kufungwa maisha lakini JPM akamnusuru

Inaelekea Jeshi letu kuna mahali pana shida kwani haiwezekani kila mahali pameoza hakuna palipo na nafuu ktk hili jambo anzia Dar mpaka kule Isangang'walugesha Simiyu mambo ni yaleyale na ni rahisi kujua kwani mtu akifanya research ktk kituo chochote cha Polisi haitochukua hata lisaa limoja ataona jinsi palivyo hovyo

Nyerere aliwahi kuvunja Jeshi la KAR na kuunda JWTZ na mambo yakawa sawa kwanini tunaogopa kuunda Jeshi upya lenye nidhamu kama jeshi la Rwanda?
 
Asante kwa kuibua haya aisee wewe ndio mzalendo. Shida ya haya majamaa yanayovaa mashati ya kijani wanafikiri kumtetea magufuli ndio uzalendo. Hapo IGP Sirro apate ujumbe huu wanalichafua jeshi la polisi
Hakika nimedhamiria kufanya hivyo ili kuwakomboa wananchi wenzangu walio wanyonge.Siwezi kukubali dhuluma
 
Itakuwa nao wanatafuta ya kununua kiwi..! Maana wale wa barabarani waliambiwa kuomba ya ku-brash viatu sio dhambi.
Mkuu,bora wa barabarani kwa kuwa wanawaomba wenye magari ambao wapo well off kiuchumi,sasa fikiri mkulima maskini kabisa unamtaka atoe Laki mbili,yeye atapata wapi?.Japo hata huko barabarani sio uungwana kufanya hivyo kwani ni chanzo cha uvunjifu wa Sheria za barabarani na kupeleka ajari zinazogharimu maisha ya watu wengi.
 
Lakini mkuu umesahau kuwa kuna kuwapa senti ya kung'arisha viatu kwa kiwi na haiitwi rushwa? hata hivyo tatizo hili la kubabikia watu inaelekea huko ni sugu sana kwani hoja za mlalamikaji zimenikumbusha bwana mmoja alisamehewa na Rais JPM naye alikuwa kutoka Njombe na alipewa kesi ya kichwa na kufungwa maisha lakini JPM akamnusuru

Inaelekea Jeshi letu kuna mahali pana shida kwani haiwezekani kila mahali pameoza hakuna palipo na nafuu ktk hili jambo anzia Dar mpaka kule Isangang'walugesha Simiyu mambo ni yaleyale na ni rahisi kujua kwani mtu akifanya research ktk kituo chochote cha Polisi haitochukua hata lisaa limoja ataona jinsi palivyo hovyo

Nyerere aliwahi kuvunja Jeshi la KAR na kuunda JWTZ na mambo yakawa sawa kwanini tunaogopa kuunda Jeshi upya lenye nidhamu kama jeshi la Rwanda?
Mkuu,hakuna lisilowezekana,shida hapo ni uthubutu tu kwa Viongozi wetu.Lkn wananchi tukipiga kelele kwa sauti moja naamini tabia hii itakomeshwa.
 
Hiyo siyo huko tu ni kanuni ya sehemu karibu zote kwamba... Kuingia bure, kutoka kwa hela.

Nakumbuka waliwahi kusema (katika storistori) "lazima tuwachukue hela ili kesho mjifunze kuyamaliza hukohuko, siyo kila jambo ni la kuletana polisi".
 
Hiyo siyo huko tu ni kanuni ya sehemu karibu zote kwamba... Kuingia bure, kutoka kwa hela.

Nakumbuka waliwahi kusema (katika storistori) "lazima tuwachukue hela ili kesho mjifunze kuyamaliza hukohuko, siyo kila jambo ni la kuletana polisi".
Mkuu Polisi,wamewekwa kwa mujibu wa sheria ili kuwalinda raia na Mali zao,sasa waliraka raia wakimbilie wapi?.Hivi kila taasisi ingesema iende kwa mtindo huo tungefika kweli?!!!.Matokeo ya mtizamo huo ni uhasama kati yao na raia kitu ambacho sio kizuri.
 
Wakuu natumai mnaendelea vizuri na kusukuma gurudumu la maendeleo ya Taifa.
Kama kichwa kinavyoeleza,Kituo cha Polisi cha Mlangali,Kata ya Mlangali,Katika Wilaya ya Ludewa iliyoko mkoa wa Njombe,pana nuka rushwa.Iko hivi hawa jamaa wakimkamata raia na kosa lolote lile hata km ni dogo namna gani watamuweka ndani halafu kutoka ni hadi utoe pesa ambayo haina risiti.Najua mtaniuliza kwanini hujapeleka kunako husika ??,Je,JF itaweza kukusaidia kutatua changamoto hiyo?.Km kuna hoja ya namna hiyo ni kwamba hadi wilayani wanafahamu tatizo hilo,OCD anajua lkn hamna utatuzi,Naleta hapa JF ili kuuhabarisha umma wa Watanzania ujue kuwa kuna Askari wanaotumia vibaya nafasi zao kunyanyasa raia na kujipatia pesa kwa njia ya rushwa.Hebu niende kwenye visa na mikasa ya hao Polisi.
Kuna matukio kadhaa yanawapata ndugu zangu na watu wengine ambapo kwa kweli yanatia simanzi.

TUKIO LA KWANZA.
Kuna jamaa mmoja,ambaye si ndugu yangu,ila nilimfahamu kwa vile alikuwa ni Fundi simu,hivyo tulifahamiana kupitia kunitengezea simu,huyu alipelekewa simu na mteja
ili aifrash,kumbe simu ile ilikuwa imeokotwa,yule aliyeipoteza alipoanza kufuatilia trend ya wahusika wakamkata na yule fundi simu,kutoka wakamdai 50,000/=,yule akawauliza Polisi kosa lake ni lipi?,maana ile ni ofisi na inajulikana na Serikali kuwa yeye ni Fundi simu na hata Polisi wenyewe huwa wanaenda kufrash hapo.Ile ishu aliingilia kati Afisa tarafa akaamuru yule jamaa arudishiwe pesa yake.

TUKIO LA PILI
Juzi kuna jamaa wamweka ndani kwa kesi isiyo na kichwa wala miguu,kiasi kwamba Polisi wenyewe wanatofautiana,wapo waliosema hapa hamna kesi na wengine kuna kesi, kikubwa walikuwa wakidai pesa ,sasa jamaa yule alikuwa na pesa kidogo yaani Polisi wale hawana hata mshipa wa aibu,walisikika wakisema pesa ni kidogo mno tutagawanaje?,tupo wengi.Jamaa akampigia simu OCD,wakapelekwa Wilayani huko wakakutanishwa na OC-CID na yeye hali ikawa hivyo hivyo,anasema jamaa wameniletea dili kwa hiyo lazima utoe pesa ya kutosha kuwagawia na wenzangu,na kwamba asipofanya hivyo basi atamfunga miaka saba jela au kumtengenezea kosa kubwa zaidi,Ili bidi jamaa zimtoke.Kwa hiyo Askari wale wote ni kitu kimoja,kuanzia wale wakubwa hadi wadogo.Lakini kitu kinachostaabisha zaidi ni jinsi hawa Polisi wanavyoweza kuomba rushwa waziwazi na kisha kugawana fedha hizo waziwazi bila woga,hadi mtoto mdogo anajua kabisa jamaa wanakula rushwa na wanagawana.
Hayo ni matukio mawili niliyoyasimulia kimuhtasari tu.Yapo mengi,ambayo nikisema niyaeleze hapa yote nitajaza Seva.

NINI NAFIKIRIA KUKIFANYA??
Kwa kuwa wananchi wengi wa Mlangali ni waoga,wanawaogopa wale Polisi,Mimi nataka kujitoa mhanga,Siogopi chochote wala yeyote Ila Mungu tu mwenye uwezo na mamlaka juu ya pumzi yangu,yeye awezaye kuua mwili na Roho;Nataka kuwa mkombozi kwao,Maana hakuna kitu ninakichukia sana ktk maisha km dhuluma,nasema hivi najitoa mhanga sina cha kupoteza,Ninasubiri waingie kwenye 18 zangu halafu wanidai rushwa, mimi nitakubali halafu nitawapigia TAKUKURU makao makuu,maana sina Imani na TAKUKURU ya Ludewa.Halafu nione je na Makao Makuu nao watapuuzia?,wakipuuza nitatafuta kila namna niende kwa Rais.Kwasababu Ikulu sio mbinguni,ni duniani na ipo kwaajili yetu.Huo ndio mpango wangu,nina hasira za kufa mtu,siwezi kuvumilia uonevu huu.Najua ktk kufanya hivyo kuna watu watapata madhara matharani wategemezi wa wahusika lkn sina namna.

WITO WANGU KWA JESHI LA POLISI
Askari Polisi msitumie vibaya madaraka yenu,hiyo kazi ni dhamana tu.Vitendo vyenu vya unyanyasaji ndivyo vinavyofanya raia tuwachukie ninyi.Mfano mmoja kule Ngara Mwanajeshi alipata ajari ya gari ambapo raia waliokuwa karibu wangemnusuru mapema angeweza kuokoa maisha, lkn jamaa walipochungulia kwenye gari na kuona ni mjeda,walisema acha afe,hatumsaidii Kwasababu ya uoenezi waliokuwa wanawafanyia.Ninyi sio miungu watu.Kutokana na dhuluma mnazozifanya na manung'uniko ya hao wanaodhulumiwa wengi wenu mkistaafu huwa mnakuwa na hali mbaya,nina Ushuhuda huo,wa Askari mmoja aliyekuwa OCD baada ya kustaafu maisha yalimwendea kombo sana hadi sasa ukimwona huwezi amini maana hadi funza wameota miguuni.Binafsi siwaombei mabaya lkn acheni kunyanyasa watu wanyonge,hizo fedha za dhuluma hazitawafikisha popote.Ombi langu kwa IGP Sirro,ni kwamba juhudi ulizozionyesha ktk kudhibiti wahalifu nchini,zionyeshe pia ktk kudhibiti nidhamu ya Askari wako nchini,Namsifu sana Mwema aliyeanzisha Polisi jamii ili kuondoa uhasama kati ya Polisi na mwananchi.
Maisha sasa hivi magumu sana,fikiri ikiwa wewe mwenye mshahara unaona hali ni ngumu,vipi kwa yule mkulima hokhe!hakhe!,hali ikoje?,halafu bado unambambikizia kesi ili akupe rushwa.Kweli wananchi wapo sahihi kutomsaidia Askari hata km anakata roho.Mjue pia mnafanya Wananchi waichukie Serikali Kwasababu ya huo mchezo wenu mchafu.
Ni matumaini yangu,kuwa nimeeleweka.Nasisitiza siogopi chochote,nimetoka mavumbini,nitarudi Mavumbini,na Kila nafsi itaonja mauti.


ALAMSIKI
Mkuu pole sana kwa madhila yaliyokupata. Wewe binafsi uliwahi kumtafuta huyo OCD ukasikia kauli yake au huyo ndugu yako alipofika huko Ludewa alibahatika kuonana naye?
Inawezekana askari akasema anaongea na kiongozi fulani kwenye simu kumbe siyo. Cha msingi kama ulivyoamua kuliweka hili bayana ungetafuta mawasiliano ya huyo OCD umpe malalamiko ili uone kama yatafanyiwa kazi au naye ataungana na hao askari wa Mlangali waliodai rushwa kutoka kwa ndugu zako.
 
Asilimia kubwa wakuu wa POLISI Wala rushwa wakuu, kwa hiyo hata ukipeleka malalamiko kwa OCD hakuna hatua inayochukuliwa, vilevile takukuru nao wanawabeba Sana POLISI kwa hiyo hakuna pa kukimbilia mjomba,kikubwa Ni kupambana nao tu, usikubali kutoa pesa kirahisi,uwe unajua utaratibu
 
Mkuu pole sana kwa madhila yaliyokupata. Wewe binafsi uliwahi kumtafuta huyo OCD ukasikia kauli yake au huyo ndugu yako alipofika huko Ludewa alibahatika kuonana naye?
Inawezekana askari akasema anaongea na kiongozi fulani kwenye simu kumbe siyo. Cha msingi kama ulivyoamua kuliweka hili bayana ungetafuta mawasiliano ya huyo OCD umpe malalamiko ili uone kama yatafanyiwa kazi au naye ataungana na hao askari wa Mlangali waliodai rushwa kutoka kwa ndugu zako.
Yaa, niliifanya hivyo lkn ni wale wale kwasababu kile mtakachoongea naye yeye anawaambia wale Askari unaowalalamikia kwa hiyo hamna Cha maana.Lkn MUNGU ni mwema tuliyamaliza japo kigumu.
 
Asilimia kubwa wakuu wa POLISI Wala rushwa wakuu, kwa hiyo hata ukipeleka malalamiko kwa OCD hakuna hatua inayochukuliwa, vilevile takukuru nao wanawabeba Sana POLISI kwa hiyo hakuna pa kukimbilia mjomba,kikubwa Ni kupambana nao tu, usikubali kutoa pesa kirahisi,uwe unajua utaratibu
Sahihi kabisa Mkuu.
 
Watanzania tuungane kudai katiba mpya, bila katiba mpya haya yataendelea milele daima.
Ni sawa kwasababu Katiba ndio mama wa sheria zote, hivyo tuanzie huko kwanza kisha twende kwenye kurekebisha sheria pia za kuwabana Askari wanaotumia vibaya madaraka yao kugandamiza raia wanyonge.
 
Ni sawa kwasababu Katiba ndio mama wa sheria zote, hivyo tuanzie huko kwanza kisha twende kwenye kurekebisha sheria pia za kuwabana Askari wanaotumia vibaya madaraka yao kugandamiza raia wanyonge.
Kukiwa na utawala wa haki na sheria, uchumi utapanda kwani ubadhirifu wa mali za umma utapungua. Matokeo yake polisi na waajiriwa wengine wataongezewa mishahara na matatizo ya rushwa yatapungua kama si kuisha.
 
Kukiwa na utawala wa haki na sheria, uchumi utapanda kwani ubadhirifu wa mali za umma utapungua. Matokeo yake polisi na waajiriwa wengine wataongezewa mishahara na matatizo ya rushwa yatapungua kama si kuisha.
Kweli kabisa,tukifika hapo tutaishi km tupo peponi vile.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom