Kituo cha Afya Fore Plan Clinic chafungwa

Kituo cha Afya Fore Plan Clinic chafungwa

Wakuligo

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
259
Reaction score
106
Wizara ya Afya imekifunga kwa mda usiojulikana kituo cha Fore plan Clinic kilichopo ilala Bungoni. Kituo hiki kinamilikiwa na Dr J.J Mwaka mtaalam wa magonjwa ya kinamama akitibu kwa kutumia tiba mbadala.

Wizara imesema kituo hakijatimiza vigezo na masharti yanayotakiwa na serikali ikiwemo kutokuwa na wataalam wenye sifa na elimu stahiki.

Dr J.J Mwaka amekuwa akionyesha kazi nzuri za kituo chake kwenye vyombo vya habari ikiwemo kutibu ugumba na upungufu wa nguvu za aina mbalimbali.
Watu wengi wamekua wakifurahia sana tiba hii mbadala itolewayo na Dr Mwaka na mpaka kituo kinafungwa wagonjwa wengi walikua wakisubilia huduma.
 
Mwenye kituo ameachwa au ameenda kunyea debe?:Serikali inatakiwa imchukue na mmiliki imtie ndani maana wanachezea sana afya za watu. Madawa yao ni ghali, na hayatibu chochote! Heko wizara ya afya

mkuu hata mimi walinipa dawa ya kuharisha siiwezi kuisahau.
 
Wizara ya Afya imekifunga kwa mda usiojulikana kituo cha Fore plan Clinic kilichopo ilala Bungoni. Kituo hiki kinamilikiwa na Dr J.J Mwaka mtaalam wa magonjwa ya kinamama akitibu kwa kutumia tiba mbadala.

Wizara imesema kituo hakijatimiza vigezo na masharti yanayotakiwa na serikali ikiwemo kutokuwa na wataalam wenye sifa na elimu stahiki.

Dr J.J Mwaka amekuwa akionyesha kazi nzuri za kituo chake kwenye vyombo vya habari ikiwemo kutibu ugumba na upungufu wa nguvu za aina mbalimbali.
Watu wengi wamekua wakifurahia sana tiba hii mbadala itolewayo na Dr Mwaka na mpaka kituo kinafungwa wagonjwa wengi walikua wakisubilia huduma.
waache wayafungie hayo madokta . Kazi kuwalandua wagonjwa kwa bei za kufa mtu ! Madawa yenywe hayatibu chochote !
 
Sikutarajia kituo kama hiki kufungiwa sababu dk Mwaka amekuwa akijatangaza sana kwenye radio na tv na niliamini kituo kina vigezo vyote vya kitaalamu vinavyotakiwa
 
Mimi pia nimeshangaa jana tu nimetoka kusikia tangazo lake anadai ametiza masharti na kituo kimesajiliwa na wizara ya afyaa...
 
dozi nilimnunulia mkewangu 250000 kunakauafazari kidogo baada ya kutumia dawa hizi
 
Sasa twende wapi? Muhimbili iliyokidhi vigezo hakuna dawa, hawa wana dawa mnasema hawajakidhi vigezo na sio vituo vipya vipo miaka mingi tu mnasema hawajakidhi vigezo au jamaa kasitisha 10% kwa mkuu fulani wa afya? Bora mtuchimbie kabisa makaburi yaliyokidhi vigezo ili msije kutufukua baadae mkasema hayajakidhi vigezomakaburi watakayotuchimbia ndugu zetu.
 
Wenye ushahidi wa msaada wa hii clinic na dawa zake wautoe.
 
Kuhusiana na hili la kufungiwa kwa muda, mwenye ufahamu kwa UNDANI SANA juu ya kitengo hiki TFDA atujuze, hata pamoja na kwamba kazi yake ni kuthibiti but what's extra authority about natural remedies?
Ambayo weeengi naona tunaikataa kwamba si dawa salama na ina garama kubwa?
 
Wenye ushahidi wa msaada wa hii clinic na dawa zake wautoe.

Binafsi mkewangu anaendelea vizuri baada ya kutumia dawa za huyu bwana.ila pesa yake ndefu.dozi mimi nimenunua 250000

Baada ya kuhangaika nae sana wife tukaenda akapimwa kipimo elfu 30 kadi 10 namshukuru mola wife anaendea vizuri kiukweli
 
chaajabu ...hikibkituobkina zaidi ya miaka 3 sasa walikuwa wapi kukifungia kabla....serikali yetu bhana aaaaagh
 
kila kitu bongo lazima kilete madhara ndio kinashtukiwa.
 
Binafsi mkewangu anaendelea vizuri baada ya kutumia dawa za huyu bwana.ila pesa yake ndefu.dozi mimi nimenunua 250000

Baada ya kuhangaika nae sana wife tukaenda akapimwa kipimo elfu 30 kadi 10 namshukuru mola wife anaendea vizuri kiukweli

Sipigi debe kwa hili…
Ila binafsi nafaham kiduchu tu kuhusu tiba asili hasa kama ukifuata utaratibu unaotakiwa kiafya unapona kabisa. Kinachosababisha hawa jamaa kuwa na bei ya juu ni utafutaji, utengenezaji na uandaaji wa hizo dawa, mf. unachukua kitu kinaitwa beetroot, garlic, white carrot, ginger na limon vyooote hivo ukifanikiwa kupata juice yake basi unaweza kuponya magonjwa flani ndani ya mwili.
Na vinapatikana sokoni But kwa mtu binafsi uende sokoni kununua uje uandae kisha utengeneze juice huo muda uko wapi?
Hapo ndipo wanapotupiga shekeli hao kona mwaka.
 
Back
Top Bottom