Kitu ambacho matajiri hawatakuambia kamwe!!!

Kitu ambacho matajiri hawatakuambia kamwe!!!

Sisi wakinga ,chanzo cha utajiri wetu mbona siyo Siri? uwa mmoja alee wenzake.
 
Asanteni kwa michango mizuri
Hope kila mmoja amejifunza
 
Hivi inakuaje mtu anaenda kumsikiliza mtu anaefundisha kutajirika ili hali ni masikini? Mtu ambae siyo tajiri hana haki ya kumfumdisha mwingine kuwa tajiri, maana hata yeye kashindwa..
 
Yeah, hili nalo ni tatizo kubwa sana, watu wengi wanajaribu kuhalalisha umasikini wao kwa kujiaminisha kuwa kutajirika kihalali haiwezekani.. Mimi naamini kutajirika kihalali inawezekana.
Na jamii kubwa imejaa watu wenye mawazo haya mAtokeo watu wanachangamkia fursa si tunaanza tu badae tunaanza kuwa tuhumu wakifanikiwa
 
True mkuu..kila tajiri na SIRI YA UTAJIRI WAKE.....
 
1 KAMWE huwezi kutajirika bila kufanya kazi kwa bidii. Wewe unayesema kwamba hakuna tajiri asiyeiba unajiliwaza tu kwa kuwa umejikatia tamaa. Hata kama mtu anatajirika kwa kuiba, LAZIMA afanye kazi ngumu ya kupanga mbinu za wizi na kuzitekeleza kwa akili nyingi sana ili asikamatwe.
2. Kweli wapo watu wanatumia uchawi katika biashara zao. Lakini huwezi kwenda kwa mganga kutafuta uchawi wa kuongeza utajiri kama huna shughuli yoyote ya kukupatia kipato.
3 Siri pekee ya kutajirika ni kufanya shughuli ya kuwapa watu wa jamii inayokuzunguka huduma ambayo haipo kwa wakati huo lakini inahitajika.
4. Bila kuwa na mpango-kazi 'uliosimama' vizuri hutaweza kupanua biashara yako. Lazima uwe na shughuli ambayo itakuletea faida ya kutosha, uwe na mpango maalum wa kuwekeza faida unaopata, na ujue kwamba ukianza shughuli fulani ikifanikiwa utajitanua kibiashara kwenye shughuli ingine ipi.
5. Mwisho ni lazima uwe UNAJIAMINI, NA UNAJUA KUTAFUTA FURSA na kuzifanyia kazi pale ambapo wenzako hawazioni.
 
Hakuna shaka na.hata moja ulilosema.bila.hilo kamwe hautafanikiwa
 
Back
Top Bottom