Kitimtim comedy imulikwe

Sasa Dr. Mariposa, saa tatu usiku ya jana, hadi saa moja na dakika ishirini na nane asubuhi ya leo, kweli Mama Mdogo anaweza walau wizara, Baraza la Sanaa na TCRA kwamba hawajafanya lolote..!!?? Wangefanyia kazi muda gani..!!??
Hawana utaratibu wa kuhakiki kabla ya kuonyeshwa?
Hadi madhara yafanyike kwanza?!
 
Sijui hata kama umeelewa mada inahusu nini,
Isome tena kwa utulivu
Pointi ni kwamba hata serikali huwa hawafungii kila kitu,

Mpaka unaona kipindi kwenye TV ni kwamba kimepitishwa na bodi ya filamu.

Hapo kazi ni kwako mtazamaji kuhakikisha nyumbani kwako vipindi hivyo inatazamwa na kundi sahihi
 
Vipindi vyote vya tivi tunavyoona na filamu zinazotoka za kitanzania huwa lazima zipate vibali vya bodi ya filamu
Aagh wapi..!! Filamu inayofuata process ndefu YES, Lakini kipindi kupata kibali cha bodi ya filamu kweli..!! I doubt
 
Siku hizi sanaa na kila kitu ni kuganga njaa tu! Ukitaka kufanya kitu hakikisha una idea ukiachilia mbali na kipaji...,Vilevile usiisahau nidhamu.

Ukifuatilia maigizo kadhaa ya miaka kenda yaliyokuwa yakiandaliwa na wizara na mabaraza mengine ya lugha na tamaduni basi ungegundua utofauti mkubwa sana na hawa walamba midomo na wapenda maisha mazuri wa sasa. (Watazame kina mzee Jangala, wale wa siri ya mtungi na wengineo)

Inaonesha wazi vijana hawataki kujishughulisha miili na akili kwenye mambo mengine yatakayowasaidia wao, vizazi vyao na taifa kwa ujumla... wanakimbilia kuonekana kwenye luninga wapate umaarufu halafu basi! Waulize "what's next sasa?!" Hana la kujibu anahunyahunya... baadae anasema "blaza au faza yule hater" Masenge sana haya matoto ya sasa hivi. Yapoyapo tu maskini!

NOTED! Ahsante kwa taarifa na uzalendo.
 
Kumbe upo bongo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Hapana, nimeuliza kwa sababu nilitaka kujua kama TV za bongo zinafuata maadili ya kutoonesha mambo yenye maudhui ya kikubwa muda ambao watoto wengi bado wapo macho.
 
Binafsi naona kimepoteza mvuto, siangalii kabisa siku hizi
 
Ukishaona kipindi mwanaume anaigiza kama Mwanamke ujue hicho kipindi na waigizaji wote hawajielewi, watazamaji, na hata hicho chombo kinaruhusu hayo madudu
 
Alafu ile eti inaitwa comedy,dah na kuna watu wanaangalia kabisa...upuuzi.
 
Hiko kipindi huwa sikupendi!!
Upuuzi mwingi sana
 
Chai
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…