Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,473
- 13,629
My elder sister you are right. Lowassa alitoswa akabaki ameduwaa, Mkapa akabakia na Sumaye mpaka mwisho wa dahari.Shida adabu yako.
Kikwete ndiye Rais pekee aliyefunga mawaziri kwa ufisadi ndiye Rais pekee aliyemtosa waziri mkuu kwa ufisadi. Na ndiye Mwenyekiti aliyeacha roadmap (ilani) inayofatwa sasa hivi.
Koma.
Mkuu nimeisoma substance katika andiko lako. Mkwere alikuwa anafanya jambo jema lakini muda huo huo kunakuwepo mazingira ya upigaji yanayotengenezwa.Nilijua utatoka shimoni kwako tu uje umtetee mfadhili wako!! Mbona husemi ufisadi wa HOME SHOPPING CENTRE na jinsi alivyofadhili hawa jamaa kupitisha makontena bandarini bila kulipa kodi; jinsi alivyowalinda wauza madawa ya kulevya mpaka ameingia Magufuli ndio wakapelekwa Marekani; Unajua yeye ndiye aliyemlazimisha Mattaka kuingia mkataba wa kukodisha ile ndege ya AIRBUS kutoka kwa mlebanoni iliyolimbikiza deni la mabilioni kwa serikali!! Halafu unasema alikuwa anapiga vita ufisadi? Unajua gharama ya Barabara ya Bagamoyo mpaka Msata umegharimu kiasi gani na mjenzi akiwa swahiba wake Subash Patel?
Unajua kısa cha yeye kusabotage kukamilika kwa rasimu ya katiba ya Warioba? Aliogopa kama ile rasimu ingepitswa na katiba kukubaliwa yeye hivi leo yangempata yaliyompata Jacob Zuma kule South Afrika!!!
Sasa wewe ndio ukome ukomae.
Naam ndio huyo huyo.Kwan Huyo Sioi Ndio Yule Mkwe Wa Lowasa Au Ni Mwingine! Ndio Yule Aliyegombea Ubunge Akashindwa Na Joshua Nasari? Sorry Lkn.
Mambo yao magumu sanaRuge na Singh nao vipi?
Mataka huyu alitokea bima taifa akaenda PPF. Mwisho akakwamia ATCL. Alisha fungwa na Sasa Yuko huru.M
Mataka tena rc bora wa simiyu
Porojo hizo
Lazima useme porojo kwavile Mkwere sio Kafir sio?
Ulikuwa hujui?
Ndio maana wanaume wa Dar tunasakamwa, ati Mataka RC bora wa simiyu, are we not updated to such extent?? Ivi hukuwai kumsikia mataka wa ATCL na hata akapelekwa mahakamani kwa kuhujumu na maamuzi ya ivyo dhidi ya shirika la ATCL??M
Mataka tena rc bora wa simiyu
Wacha wasote maana imeandikwa utaishi kwa jasho lako sio wizi.IKIWA ni zaidi ya miaka miwili tangu aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake kufi kishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wameendelea kusota rumande kwa sababu upelelezi bado haujakamilika.
Aprili Mosi 2016, Kitilya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kampuni inayoshughulikia Uwekezaji wa Mitaji na Dhamana (Egma) pamoja na maofisa wawili wa Benki ya Stanbic akiwemo aliyekuwa Miss Tanzania (1996), Shose Sinare na Sioi Solomon ndio ilikuwa mara ya kwanza kufikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka nane ikiwemo ya utakatishaji fedha.
Hata hivyo, washitakiwa hao wanaendelea kusota rumande kwa sababu mashitaka ya utakatishaji fedha yanayowakabili hayana dhamana kisheria. Jana upande wa mashitaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Patrick Mwita alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba wanawasiliana na wachunguzi ili wajue upelelezi umefikia wapi.
Mwita aliieleza mahakama kuwa upelelezi bado haujakamilika kwani wanaendelea kuwasiliana na wachunguzi. Baada ya kueleza hayo, Hakimu Shaidi aliahirisha kesi huyo hadi Novemba 16, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama upelelezi umekamilika ama la.
Washitakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha. Wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Machi 2013 na Septemba 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani milioni 550 kwa Serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard Chartered Uingereza.
Wanadaiwa kuwa Machi 2013 jijini Dar es Salaam walijipatia dola za Marekani milioni sita, wakionesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo na zililipwa kupitia Kampuni ya Egma T Ltd.
Washitakiwa hao wanadaiwa kutakatisha fedha kwa kuhamisha, kuchukua na kuweka dola za Marekani milioni sita katika akaunti tofauti za benki. Kati ya Machi 2013 na Septemba 2015, wanadaiwa kuwa waliweka fedha hizo katika akaunti mbalimbali zilizomilikiwa na kampuni ya Egma na kwamba walipaswa kufahamu kuwa fedha hizo ni mazao ya uhalifu wa kughushi.
Huko kote inaonekana sio chuki au kisasi ila kwa jpm tukila rais alitafuta WA kumtingisha kipindi chake hivyo magufuli sio wa kwanza kumbuka
Mkapa alimtingisha nalaila kiula
JK mramba na yona
Jiwe ndio hao na kina seth