Kiti moto cha Hagel

Kiti moto cha Hagel

Kwameh

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2011
Posts
1,793
Reaction score
2,161
OB-WE457_Hagel1_G_20130131094941.jpg

Swali, Kamati ya Bunge, Huduma za Kijeshi:
Umewahi kutamka kwamba kundi la ushawishi la Wayahudi linatisha watu wengi sana hapa, na kwamba wewe sio Mbunge wa Israel wewe ni Mbunge wa Nebraska, na kwamba hili shinikizo linafanya watu wafanye mambo ya kipumbavu saa nyingine. Taja mtu mmoja kwa mawazo yako ambae anatishwa na kundi la ushawishi la Israel kwenye Bunge la Marekani.

Chuck Hagel, Waziri wa Ulinzi Mteule wa Obama: Aah, kwanza kabisa

Swali: Taja mmoja!

Hagel:
Sijui

Swali: Kwa nini ulisema?

Hagel: Sikuwa na mtu kichwani niliemmaanisha

Swali: Unakubali kwamba ni maneno ya kichokozi na hakuna maneno ya kichokozi kuzidi hayo kuhusu uhusiano wetu na Israel na Bunge hili? Taja kitu kimoja cha kipumbavu ambacho tumesukumwa kufanya na kundi la ushawishi la Israel

Hagel: Nimesema nasikitika

Swali:
Lakini ulitamka kwamba wanatufanya tufanye mambo ya kipumbavu, huwezi kutaja Mbunge mmoja anaetishwa, basi nipe mfano mmoja wa kitu cha kipumbavu ambacho tunashinikizwa kufanya hapa.

Hagel: Kwenye ule usaili nilikua naongelea...

Swali: Sawa, nipe mfano ambapo tumetishwa na kundi la ushawishi la kiyahudi la Israel kufanya kitu cha kipumbavu kuhusu Mashariki ya Kati, Israel au popote

Hagel:
Siwezi

Swali: Ahsante, unakubaliana na mimi kwamba usingesema kitu kama hicho?

Hagel: Ndio nilichemka, nimeshasema hivyo.

========================================================

Kwa maoni yangu, inatia moyo kusikia wabunge wa Wamarekani wanapinga na kukasirishwa na nadharia ya kwamba Marekani inapelekeshwa puta na Israel, japo inawezekana ni kweli. Na nitafurahi Hagel akipita kwa sababu haamini katika upuuzi wa "Taifa Teule" wala kuifagilia fagilia Israel, japo ni Mkristo kama mimi.
 
Kama chuck atapita,atapita kwa mbinde sana na israel hawamtaki kabisa huyo jamaa.
 
It was bad kwa kweli .Hapo
Obama anakuambia the best choice ever
 
Kama chuck atapita,atapita kwa mbinde sana na israel hawamtaki kabisa huyo jamaa.

Chuck hagel alikuwa pro Israel senator .Ila ana kiburi babu huyo " alimwambia democratic wakauze nyanya" .Anadharau na kiburi na alikuwa best friend wa MCcain .
 
Kama chuck atapita,atapita kwa mbinde sana na israel hawamtaki kabisa huyo jamaa.
Obama atapigana kwa udi na uvumba kuona Hagel anapita kwa sababu walishampiga chini chaguo lake la Waziri wa Nchi, Susan Rice. Kwenye hili akikubali kwenda chini mbili bila ataonekana dhaifu mbele ya republicans na watapata nguvu ya kumburuza na kumpinga kwa kila kitu anachojaribu.
 
Chuck hagel alikuwa pro Israel senator .Ila ana kiburi babu huyo " alimwambia democratic wakauze nyanya" .Anadharau na kiburi na alikuwa best friend wa MCcain .

Natalia nadhani umechanganya data kidogo hapo. Hagel sio pro Israel senator. Hagel amewahi kusema yeye sio senator wa Israel, ni senator wa Nebraska, na amewakandia ma lobbyist wa Israel kwa kusema wanafanya masenators wenzie wafanye vitu vya kipumbavu. Kitu ambacho ni kikubwa na hatari sana kukitamka mwanasiasa wa Marekani.

Mi namkubali sana Hagel. Hahusudishi vita wala unilateral actions za Marekani. Pia hawafagilii Waisrael.

Ila republicans walimpiga ngumi za mbavu nyingi kuhusu hili la unilateral actions, walimuuliza, wewe unajifanya unapenda sana multilateral actions za Marekani na washiriki wake, sasa kwa nini ulikataa kusaini barua ya bunge hili kwenda EU kuwaomba na wao waiorodheshe Hezbollah kama kikundi cha kigaidi? Hagel masikini ya Mungu akatokea hana jibu lenye ushawishi.
 
Back
Top Bottom