"Kikao cha mwisho cha chama ambacho nilishiriki na Regia nilihudhuria kwa muda mfupi sana. Wenzangu watakumbuka mengine katika kila kikao kile. Mimi ninakumbuka moja tu ambalo ni moja ya sifa pekee aliyokuwa nayo na wanayo wanasiasa wachache sana na hasa wanasiasa vijana (ambao hupenda zaidi siasa za kuridhisha kwa kusema watu wapendacho). Regia alikuwa na uwezo mkubwa wa kusema usichopenda kusikia. Alisema tu. Katika kikao kile wajumbe na Wabunge walikuwa katika emotion sana kuhusiana na muswada wa mchakato wa kuandika Katiba. Mjadala ulikuwa mkali sana. Mwenyekiti wetu akampa nafasi Regia aseme. mimi nashauri tuombe kuonana na Rais Kikwete yalikuwa ni maneno yake makali kupenya kwenye ngome za masikio ya wengi na yalipokelewa kwa mguno mkubwa. Mwenyekiti akaamrisha wajumbe na Wabunge watulie kwani Regia ana haki ya kutoa maoni yake. Mimi niliondoka baada ya muda mfupi maana nilikuwa ndio nimetoka nchini India kwa matibabu na nilikuwa na masharti ya kupumzika muda mrefu. Ushauri wa Regia (pamoja na wajumbe na viongozi wengine wa chama walioshauri ama waziwazi au kwa chinichini) ndio uliofuatwa na sasa kumekuwa na mazungumzo ya mara kwa mara ya viongozi kuhusu sheria ile ya mchakato wa kuandika Katiba. Huyu ndio dada Regia. Maisha mafupi lakini mafunzo makubwa katuachia vijana wenzake kwenye medani ya siasa".By Zitto
Kufuatia taifa kugubikwa na wasiwasi mkubwa sana baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kupitisha muswada wa marekebisho ya Katiba huku ukiwa unalamikiwa karibu katika kila pembe ya nchi yetu; leo baada ya kupokea ushuhuda wa Mhe Zitto ya nini kilichojiri hata kuiacha Tanzania ikiwa salama salmini hadi leo. Ni dhahiri kuwa kifo cha ndugu yetu Regia Mtema kitakuwa kimeacha pengo kubwa katika taifa hili kwani alikuwa miongoni mwa watu wanaoweza kutoa suluhisho la amani na utulivu hata katika hali tete kama ilivyokuwa wakati huo.
Ni kwa kuzingatia hilo natoa raia kuwa kitengo na sera za usalamaza CDM viimarishwe ili viweze kutoa ushauri wa mambo ya kiulinzi na usalama ili kupunguza ama kuepusha kutokea tena kwa kadhia kama hii. Ikumbukwe kuwa hii ni mara ya pili kwa mbunge wa CDM kufariki kutokana na ajali za barabarani, wa kwanza alikuwa Marehemu Chacha Wangwe.
Na mara zote makosa ya kibinadamu ndio yametajwa kusababisha ajali hizi. Mathalani katika ajali ya Marehemu Chacha Wangwe yafuatayo yalibainika:-
a) Dereva hakuwa na leseni ya kuendesha gari na kupatikana na hatia ya kosa hilo na mahakama na kuhukumiwa.
b) Licha ya kutokuwa na leseni ya kuendesha gari, dereva alikuwa kiendesha gari husika kwa mwendo wa kasi sana.
c) Kutokana na gari husika kusemekana lilihitaji matengenezo kabla ya kuanza safari, inadhaniwa kuwa gari halikuwa katika hali nzuri kumudu sfari hiyo achlia mbali kutumiwa na Mhe Mbunge.
Katika ajali iliyopoteza uhai wa Regia Mtema yafutayo yanatajwa kusababisha ajali hiyo:-
a) Mwendo wa kasi wa dereva (Vyombo vya habari vinataja kuwa Marehemu Regia ndio alikuwa dereva wa gari hilo wakati wa ajali).
b) Kwa mujibu wa mmoja wa askari aliyeshuhudia ajali hiyo, dereva (Vyombo vya habari vinataja kuwa Marehemu Regia ndio alikuwa dereva wa gari hilo wakati wa ajali) alifanya kosa kwa kuamua kulifuata gari lingine lilokuwa mbele yake upande wa kulia ili kulipita gari lililokuwa mbele yao; hivyo gari lililokuwa mbele ya gari la marehemu lilipomaliza kulipta gari hilo, ghafla lilirudi haraka upande wa kushoto na kuliacha gari la marehemu likitazamana uso kwa uso na gari liliokuwa likija toka upande wa wa pili (Ruvu), ndipo gari la marehemu likalazimika kuingia porini na kupindika mara tatu.
c) Kwa uzoefu wangu binafsi wa kuhusika na ajali na majadiliano niliyoyafanya na baadhi ya madereva ambao wamewahi kuhusika katika ajali mbali mbali na kunusurika; ajali hii haikuwa kubwa kiasi cha kusababisha vifo kama hatua mbali mbali za kiusalama zingekuwa zimezingatiwa, inadhaniwa kuwa marehemu na pengine hata abiria katika gari hilo hakuwa amefunga mkanda wakati ajali inatokea.
d) Kwa kuzingatia hali ya marehemu kimaumbile, haikuwa kitu cha hekima na busara kuendesha gari lenye nguvu kama Toyota Land Cruiser. Sijui kama gari hili lilikuwa ni maalum kwa walemavu. Kama gari hili lilikuwa ni gari la kawaida haiingii akilini marehemu kwa hali yake ya kimaumbile aliwezaje kuruhusiwa kuendesha gari hili; Chama chake na Kikosi cha Usalama barabarani wailikuwa wapi kutochukua hatua mapema hadi Mbunge anapoteza maisha?
Kwa kuzingatia hayo machache wakati sote tukiwa na uchungu mkubwa, ni vyema viongozi wa CDM wakaondoa dhana ambayo bado wanaoonekana kuwa nayo kuwa CDM bado ni chama kidogo. Hivyo wachukue hatua mara moja ya kuwa kuimarisha kitengo cha uslama pamaoja na sera ya usalama wa viongozi wao ili kuepusha majanga kama haya kutumaliiza viongozi wetu.