Kitendo cha kutotoka nje D9 kwa tamko kwa Umma sio ushindi wa dola ni kashfa kwa serikali

Kitendo cha kutotoka nje D9 kwa tamko kwa Umma sio ushindi wa dola ni kashfa kwa serikali

mager6

Senior Member
Joined
Jul 5, 2025
Posts
145
Reaction score
220
Wale waliotaka kuandamana Gz waliomba waandamane Kwa amani.

Wangeruhusiwa ingesaidia kujua wanataka Nini. Kwa namna walivyo nificha siku Ile ni sahihi kusema watatafuta Plan C.

Ikumbukwe walikuwa na kundi nyuma yao tuliite anonymous mbinu zote za kuchoma miundombinu na Mali za waliowahisi wezi wa fedha za walipa kodi sio burebure ni mbinu za kivita.

Ni kawaida vitani kulipua madaraja.

Mamlaka kuwa kimya kana kwamba hakuna kilichotokea na kutosikiliza Hawa watoto wa 2000 ni bomu kubwa zaidi ya kilichotokea.

Ieleweke kwamba vyuo vikuu, kidato cha nne na sita hizi taasisi zinamwaga makundi Kwa makundi wasichana Kwa wavulana Kila mwaka inamaana kwamba bado mto wa kizazi hiki unaendelea kutiririsha watoto wa Gen Z wanaendelea kuonhezeka Malaki Kwa Malaki.

Makundi yaliyomo kwenye hii sintofahamu.

1. Ndani ya serikali iliyopita wamo
2. Ndani ya vyombo ulinzi wamo
3. Upinzani wamo
4. Uraiani wamo

Hili jambo ilikuwa Mh Samia angeamrisha vyombo vya usalama viruhusu maandamano ya amani wawalinde wananchi asikie kero na wanachotaka.

Baada ya hapo ni kukaa mezani na mwisho wa siku katiba ya warioba ichukuliwe irekebishwe na makubaliano mojawapo iwe.

Katiba iwaache Marais waliopita nje na isiwahukumu. Lkn kipengele hicho kirekebishwe. Kwamba rais ashitakiwe
 
Back
Top Bottom