Kitabu cha Roho ya Paka by Ben Mtobwa

Kitabu cha Roho ya Paka by Ben Mtobwa

nameless girl

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2012
Posts
4,195
Reaction score
2,685
Inspekta Kombora anaitwa katika hoteli moja jijini Dar
es Salaam ambapo anaonyeshwa mwill wa msichana aliyeuawa kikatili kupita kiasi. Ngozi na nyama ya uso wake mzima na sehemu ya shingo lake imeliwa kwa aina
fulani ya sumu na hivyo kufanya sura yake ibakie fuvu la kutisha. Katika kinywa cha fuvu hile
maandishi uliosomeka: Tunamtaka Joram Kiango.


Salamu ambazo zinamfikia Joram kwa namna nyingine.
Zilifuatiwa na patashika nzito, roho mkononi, huku watu wengi walio na wasio na hatia wakipoteza roho zao. Lakini ni roho ya Joram Kiango ndiyo aliyokuwa anahitajika kwa udi na uvumba. Naye, akijua kuwa anapambana na mbogo waliojeruhiwa, alichukua hadhari zote mithili ya
paka. Hata roho yake pia inabadillka na kuwa "Roho ya paka....

Na. BEN R. MTOBWA


Jipatie kitabu hiki cha kusisimua kwa shilingi 10,000 pamoja na vitabu vingine vingi vya Hayati Ben Mtobwa sasa, unaweza kuvitazama hapa orodha ya vitabu tulivyonavyo. Heko Publisher Ltd
Kwa anayehitaji naomba nipigie kwa 0712504985. Maeneo ambayo vitabu hivi vinapatikana ni Kinondoni, Posta na Arusha.

Karibuni sana....
 
Bongo lini watu wataanza kufanya adaptation of novels to films?!
Tumeanza. Ingawa hatufanyi vizuri sana lakini tunajitahidi mdogomdogo.
Mfano Mtobwa alishatoa filamu ya Joram Kiango mwaka 2007 ya Lazima Ufe Joram. Pia Ngoswe iliwahi kutoka chini ya kampuni ya Heko na nyingine nyingi.
 
Tumeanza. Ingawa hatufanyi vizuri sana lakini tunajitahidi mdogomdogo.
Mfano Mtobwa alishatoa filamu ya Joram Kiango mwaka 2007 ya Lazima Ufe Joram. Pia Ngoswe iliwahi kutoka chini ya kampuni ya Heko na nyingine nyingi.
Tupo kwenye kipindi cha mpito cha film industry kuaminisha tena Watanzania kwamba they can deliver. Ni bahati mbaya sana stori mbovu kwenye filamu zetu zikafanya majority ya Watanzania waachane na filamu zetu!

Mbaya zaidi, hili lilitokea kipindi ambacho watu ulimwenguni wakiwa na option ya kupata filamu kutoka popote pale duniani kwa pesa ndogo tu!!
 
Tupo kwenye kipindi cha mpito cha film industry kuaminisha tena Watanzania kwamba they can deliver. Ni bahati mbaya sana stori mbovu kwenye filamu zetu zikafanya majority ya Watanzania waachane na filamu zetu!

Mbaya zaidi, hili lilitokea kipindi ambacho watu ulimwenguni wakiwa na option ya kupata filamu kutoka popote pale duniani kwa pesa ndogo tu!!
Yeah ni kweli. Kuna sababu nyingi zinazotufanya tushindwe kufanya vizuri.
Lakini kwa upande wangu bado sijakata tamaa. Mungu akipenda tutamuweka Joram katika filamu.
 
Tupo kwenye kipindi cha mpito cha film industry kuaminisha tena Watanzania kwamba they can deliver. Ni bahati mbaya sana stori mbovu kwenye filamu zetu zikafanya majority ya Watanzania waachane na filamu zetu!

Mbaya zaidi, hili lilitokea kipindi ambacho watu ulimwenguni wakiwa na option ya kupata filamu kutoka popote pale duniani kwa pesa ndogo tu!!
Shida/ changamoto kubwa wakifanya filamu wanafanya zenye mahadhi ya kizungu, wakifanya kama walivyofanya kwenye tamthilia ya “Hukumu ya Tunu” na ile ya “siri ya mtungi” akina “Cheche” mbona tunavutika saaanaaa kuzitizama.
 
Back
Top Bottom