Kiswahili ndiyo kibaya hivi kweli?

Kiswahili ndiyo kibaya hivi kweli?

Ligogoma

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2010
Posts
3,502
Reaction score
6,458
Habari WanaJF?

Nimekuwa nikiona jamii ya watu wenye ulemavu wakikataa kutumika maneno ya Kiswahili katika ulemavu wao kwa madai kuwa yanaonyesha dharau kwao. Nimejiuliza sana kwa nini iwe ni walemavu wote?

Mfano: Zeruzeru - watu wenye Albinism
Kiwete - Wanataka waitwe walemavu wa miguu
Kipofu - Wanataka waitwe walemavu wa macho au wenye uoni hafifu
Taahira - Wanataka waitwe walemavu wa akili
Chongo - Wanaka waitwe walemavu wa macho pia
Mbilikimo - sijajua wanataka waitweje lakini ukimwita mtu mfupi Mbilikimo ugomvi wake haushikiki. Anahisi umemdharau.
Andunje - pia ni tabu tupu

Hebu wadau wa Kiswahili tupeni elimu, ni kweli Kiswahili kipo kwa ajili ya kubeza walemavu au ni wao walemavu wanajishtukia?

Nawasilisha
 
Tatizo lilianza pale watu walipo anza kutumia neno kipofu kama tusi


Kw. Mf unaweza kuwa unaoneshwa kitu na rafiki yako afu wewe kwa haraka haraka usikione

Rafikiako akwambie WE KIPOFU NINI? UNASHINDWAJE KUONA WAKATI MI NAKIONA KABISA?....

SASA KWA MUKTADHA KAMA HUO YULE ALIYE KIPOFU/MLEMAVU WA MACHO ANAONA KAMA HALI ALIYO NAYO INABEZWA SANA NA WALE WASIO VIPOFU NA HIVYO KUANZA KUCHUKIA NENO KIPOFU....


THE SAME KWA WALEMAVU WENGINE. ni mtazamo tu


Nyambizi ni aina ya samaki au meli lakini neno hilo likitumika kwa msichana linaweza kumaanisha tusi

Neno kama MAYASA lilivuma enzi hizo ila kwa asili sidhani kama lilikuwa ni tusinila matimizi yake ndio yaliyosababisha liwe kama tusi



Ni mtazamooooo tuuuuu
 
Kweli ni ajabu kabisa haya maneno hayatakiwi kutumiwa, kwani ni nani aliyeyatunga?
 
Yaani kuyasema siku hizi ni kama nilipokuwa mdogo niliambiwa sipaswi kulinyooshea kaburi kidole. Naogopa kutamka kumwita mtu zeruzeru maana anaweza kukushtaki kuwa unataka umkate mkono....kiswahili kimechafuliwa sana.
 
We unaona ubaya gani kwenye hayo maneno!!! ... Au ulitaka yawekewe udambwi udambwi kama ya kiingereza
 
We unaona ubaya gani kwenye hayo maneno!!! ... Au ulitaka yawekewe udambwi udambwi kama ya kiingereza

Mi sioni ubaya wowote ndo mana nashangaa wenye ulemavu ukibainisha ulemavu wao kwa jina halisi wanakataa. Mfano mwite mtu zeruzeru uone kasheshe lake ila ukiliwekea mbwembwe za kiingereza wanakubali.

Kuna dada mmoja Iringa ni mfupii, aliitwa mbilikimo! Nilisikitika matusi yote yalimtoka, akidai katukanwa kwa kuitwa mbilikimo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom