Kisa cha mfalme Belshaza na yanayofanyika CHADEMA

dawa yenu

JF-Expert Member
Jan 7, 2014
2,822
3,650
MENE MENE TEKEL NA PERES, kiganja cha mkono kilionekana kikiandika maneno hayo ukutani. Hiyo ilikuwa ni siku ya karamu kubwa iliyoandaliwa na mfalme wa Babeli aliyeitwa Belshaza ambaye ni mjukuu wa Nebukadreza. Siku hiyo walialikwa wageni wa heshima nao wakala na kunywa wakitumia vikombe vya dhahabu na fedha na mabakuli yaliyochukuliwa katika hekalu la Yehova huko Yerusalemu, hili lilikuwa ni chukizo mbele ya Mungu ndipo katika hali ya kustaajabisha maneno yakaandikwa ukutani MENE MENE TEKEL NA PERES.

Ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Mungu kwenda kwa mfalme Belshaza ila nani atatafsiri maneno hayo? Waliletwa “wachawi” wenye akili lakini hakuna aliyekuwa na ujuzi wa kusoma maandishi yale ukutani. Baada ya tafakuri kubwa ndipo mama wa mfalme akapendekeza aitwe Daniel kwa maana yeye anaijua miungu mitakatifu hivyo ataliweza zoezi hili. Baada ya Daniel kuitwa alitafsiri maneno hayo ya Mungu.

Daniel alisema Yehova alimuondoa Nebukadreza babu ya Belshaza asiwe mfalme kwa kuwa alikuwa na kiburi sana, naye Yehova alimuadhibu Nebukadreza. Belshaza aliyajua yote yaliyompata babu yake ila naye anafuata njia ile ile ya babu yake, amechukua vikombe na mabakuli katika hekalu la Yehova na kuvinywea. Ndiyo sababu Mungu amepeleka mkono uandike maneno hayo MENE MENE TEKEL NA PERES yaani “Mungu amezihesabu siku za ufalme wako na kuzimaliza, umepimwa katika kipimo na kuonekana hufai kitu, ufalme wako wamepewa Wamedi na Waajemi.” Maneno hayo yalitimia siku hiyo hiyo na ufalme wa Belshaza ukafikia hatima yake kutokana na kiburi chake.(Daniel 5:1-31)

Naliona anguko la Chadema kama chama kikuu cha upinzani Tanzania. Ni anguko lililodhahiri kama yale maneno ukutani ila kama ilivyo kwa mfalme Belshaza ndivyo ilivyo kwa Mbowe, ameshindwa kuliona anguko hilo, MENE MENE TEKEL NA PERES. Zaidi ya mikutano na matamko yasiyo na tija sijaona jitihada za wazi za kimkakati za kuifanya Chadema iendelee kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania. Ni kama vile viongozi wa Chadema wanadhani chama chao kina “devine right” hivyo kitaendelea kupendwa na Watanzania katika mazingira yoyote yale, hii si sawa.

Chadema ina wafuasi wengi ulikilinganisha na vyama vingine vya upinzani na kama mazingira ya kisiasa yangekuwa fair huenda kina wafuasi wengi kuliko CCM ila sioni hali hii ikiendelea kutokana na viongozi wa chama kutotaka kubadili mbinu kwa kuzingatia mabadiliko ya kisiasa yaliyotokea Tanzania kwa kipindi hiki cha miaka mitatu. Kwa sasa uwepo wa Chadema unategemea zaidi huruma ya Watanzania ila wakati umekaribia ambapo huruma haitokuwa kigezo bali kitaangaliwa chama chenye nia thabiti, mipango na mikakati yakinifu ya kukiondoa chama cha Mapinduzi. Je Chadema wamejiandaa kwa hili?

Chadema sio chama cha upinzani cha kwanza kuwa na nguvu Tanzania, ilikuwepo NCCR MAGEUZI pia ilikuwepo CUF ila kwa sasa vyama hivi havina mvuto machoni mwa Watanzania walio wengi kwa sababu havikuonyesha nia dhabiti ya kusiamamia kile walichokuwa wakikinena. CHADEMA inalijua hili ila inapuuza kama mfalme Belshaza alivyopuuza yaliyoupata ufalme wa babu yake hadi ufalme wake pia ukaanguka na ali hii itaipata pia CHADEMA ikiwa haitajitathmini na kuchuka hatua stahiki kwa ajili ya kujihakikishia uhai wake.

Ni ajabu sana kuona makamanda wa CHADEMA wanavyobeza nguvu ACT-WAZALENDO kwa Tanzania bara. Wanadhani haina nafasi, nadhani wamesahau hata wao hawakuwa na nafasi mwaka 2005 ila jitihada zao za wazi zimewafikisha hapo walipo leo na ndivyo itakavyokuwa kwa ACT-WAZALENDO. Ni wazi vijana taratibu wameanza kumuamini tena Zitto Kabwe na zile kauli kuwa ni msaliti zimeanza kupungua na wengi wameanza kumuona kama shujaa atakayewafikisha nchi ya ahadi, Mbowe umeliona hili?

Wazungu wanasema, “pride comes before a fall” huu ubezaji wanaoufanya akina Yeriko Nyerere hakika ni mwanzo wa anguko la CHADEMA kama lilivyotokea kwa ufalme wa Belshaza. Makamanda ni lazima waache ego na pride zisizo na tija na waitambue nguvu ya Zitto na ACT na kutazama namna gani watasonga mbele pamoja kwa manufaa ya upinzani wote vinginevyo watagawana kura 2020 na CCM itabaki kuwa kinara. Na endapo hili halitafanyika sioni CHADEMA ikiendelea kuwa chama kikuu cha upinzani baada ya 2020.

Ni wakati wa CHADEMA kuyasoma maandishi ukutani, MENE MENE TEKEL NA PERES.
 
Belshazar mwenyewe hakuwahi kuwa mfalme,yeye alikuwa mwwana wa mfalme,crown prince lakini hakupata kuwa mfalme hadi kifo chake,
Chanzo changu kinaonyesha alikuwa mfalme, ila hebu tuache kubishania rangi ya paka, tujadili uwezo wa paka kukamata panya.... Je unaona jitihada zozote za Chadema katika kuipambania nafasi yao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chadema kwisha habari yake nasimama na CHAUMA chini ya mwanasiasa safi kabisa HASHIM Rungwe

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
MENE MENE TEKEL NA PERES, kiganja cha mkono kilionekana kikiandika maneno hayo ukutani. Hiyo ilikuwa ni siku ya karamu kubwa iliyoandaliwa na mfalme wa Babeli aliyeitwa Belshaza ambaye ni mjukuu wa Nebukadreza. Siku hiyo walialikwa wageni wa heshima nao wakala na kunywa wakitumia vikombe vya dhahabu na fedha na mabakuli yaliyochukuliwa katika hekalu la Yehova huko Yerusalemu, hili lilikuwa ni chukizo mbele ya Mungu ndipo katika hali ya kustaajabisha maneno yakaandikwa ukutani MENE MENE TEKEL NA PERES.

Ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Mungu kwenda kwa mfalme Belshaza ila nani atatafsiri maneno hayo? Waliletwa “wachawi” wenye akili lakini hakuna aliyekuwa na ujuzi wa kusoma maandishi yale ukutani. Baada ya tafakuri kubwa ndipo mama wa mfalme akapendekeza aitwe Daniel kwa maana yeye anaijua miungu mitakatifu hivyo ataliweza zoezi hili. Baada ya Daniel kuitwa alitafsiri maneno hayo ya Mungu.

Daniel alisema Yehova alimuondoa Nebukadreza babu ya Belshaza asiwe mfalme kwa kuwa alikuwa na kiburi sana, naye Yehova alimuadhibu Nebukadreza. Belshaza aliyajua yote yaliyompata babu yake ila naye anafuata njia ile ile ya babu yake, amechukua vikombe na mabakuli katika hekalu la Yehova na kuvinywea. Ndiyo sababu Mungu amepeleka mkono uandike maneno hayo MENE MENE TEKEL NA PERES yaani “Mungu amezihesabu siku za ufalme wako na kuzimaliza, umepimwa katika kipimo na kuonekana hufai kitu, ufalme wako wamepewa Wamedi na Waajemi.” Maneno hayo yalitimia siku hiyo hiyo na ufalme wa Belshaza ukafikia hatima yake kutokana na kiburi chake.(Daniel 5:1-31)

Naliona anguko la Chadema kama chama kikuu cha upinzani Tanzania. Ni anguko lililodhahiri kama yale maneno ukutani ila kama ilivyo kwa mfalme Belshaza ndivyo ilivyo kwa Mbowe, ameshindwa kuliona anguko hilo, MENE MENE TEKEL NA PERES. Zaidi ya mikutano na matamko yasiyo na tija sijaona jitihada za wazi za kimkakati za kuifanya Chadema iendelee kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania. Ni kama vile viongozi wa Chadema wanadhani chama chao kina “devine right” hivyo kitaendelea kupendwa na Watanzania katika mazingira yoyote yale, hii si sawa.

Chadema ina wafuasi wengi ulikilinganisha na vyama vingine vya upinzani na kama mazingira ya kisiasa yangekuwa fair huenda kina wafuasi wengi kuliko CCM ila sioni hali hii ikiendelea kutokana na viongozi wa chama kutotaka kubadili mbinu kwa kuzingatia mabadiliko ya kisiasa yaliyotokea Tanzania kwa kipindi hiki cha miaka mitatu. Kwa sasa uwepo wa Chadema unategemea zaidi huruma ya Watanzania ila wakati umekaribia ambapo huruma haitokuwa kigezo bali kitaangaliwa chama chenye nia thabiti, mipango na mikakati yakinifu ya kukiondoa chama cha Mapinduzi. Je Chadema wamejiandaa kwa hili?

Chadema sio chama cha upinzani cha kwanza kuwa na nguvu Tanzania, ilikuwepo NCCR MAGEUZI pia ilikuwepo CUF ila kwa sasa vyama hivi havina mvuto machoni mwa Watanzania walio wengi kwa sababu havikuonyesha nia dhabiti ya kusiamamia kile walichokuwa wakikinena. CHADEMA inalijua hili ila inapuuza kama mfalme Belshaza alivyopuuza yaliyoupata ufalme wa babu yake hadi ufalme wake pia ukaanguka na ali hii itaipata pia CHADEMA ikiwa haitajitathmini na kuchuka hatua stahiki kwa ajili ya kujihakikishia uhai wake.

Ni ajabu sana kuona makamanda wa CHADEMA wanavyobeza nguvu ACT-WAZALENDO kwa Tanzania bara. Wanadhani haina nafasi, nadhani wamesahau hata wao hawakuwa na nafasi mwaka 2005 ila jitihada zao za wazi zimewafikisha hapo walipo leo na ndivyo itakavyokuwa kwa ACT-WAZALENDO. Ni wazi vijana taratibu wameanza kumuamini tena Zitto Kabwe na zile kauli kuwa ni msaliti zimeanza kupungua na wengi wameanza kumuona kama shujaa atakayewafikisha nchi ya ahadi, Mbowe umeliona hili?

Wazungu wanasema, “pride comes before a fall” huu ubezaji wanaoufanya akina Yeriko Nyerere hakika ni mwanzo wa anguko la CHADEMA kama lilivyotokea kwa ufalme wa Belshaza. Makamanda ni lazima waache ego na pride zisizo na tija na waitambue nguvu ya Zitto na ACT na kutazama namna gani watasonga mbele pamoja kwa manufaa ya upinzani wote vinginevyo watagawana kura 2020 na CCM itabaki kuwa kinara. Na endapo hili halitafanyika sioni CHADEMA ikiendelea kuwa chama kikuu cha upinzani baada ya 2020.

Ni wakati wa CHADEMA kuyasoma maandishi ukutani, MENE MENE TEKEL NA PERES.
Umetumia takwimu gani kuhalalisha huu upupu wako?

Hiyo Act unayoiona inakuja kuwa na nguvu ni kwa sababu ya Maalim Seif kujiunga Act au hiyo nguvu ya Act inatoka wapi?

Kama jibu lako ni kwa sababu Maalim Seif na timu yake wamejiunga Act utakuwa unakosea sana, Maalim Seif hana ushawishi wowote kwa siasa za Tanganyika.

Cuf hiyo ilikuwa inapumlia mashine na yeye akiwa sehemu ya uongozi (Katibu Mkuu).

Uzi wako huu hauna fact zaidi ya hisia hisia tu kama uko na mpnz wako kitandani.
 
dawa yenu,

..kwanini act, chadema, na cuf-maalim wasiungane na kuwa chama kimoja?

..Zitto ni mbunge pekee wa chama chake.

..Maalim Seif na wenzake wameporwa chama chao, kwa maana hiyo hawakuwa na chama.

..Chadema ndiyo wenye wabunge wengi na wamesambaa maeneo mengi kuzidi chama chochote cha upinzani.

..Sasa kwanini Zitto, na Maalim hawakujiunga na Chadema na kuunda chama chenye nguvu kubwa zaidi, badala yake ni kama wameamua kuanza upya na wanataka kuifufua Act?

..Act tayari kina usajili. Lakini practically ni chama kipya kutokana na ukweli kwamba kina mbunge mmoja tu.

..naweza kuwa nimekosea, lakini kwa maoni yangu this was a GOLDEN OPPORTUNITY ya kuwa na chama kikubwa cha upinzani kitakachoi-challenge CCM na hawa ndugu zetu wameiacha nafasi hiyo ipite.

..Maalim Seif, Zitto Kabwe, na Freeman Mbowe, walitengenezewa mazingira, na sababu, za kuunda chama chenye nguvu, lakini hawakuona sababu ya kufanya hivyo.



Cc tindo, Nguruvi3, Mag3, MTAZAMO
 
Wasaliti wa harakati hawana muda mrefu watabakia majina tuu.Ili wimbi la maalim kuhamia chama ambacho hakifungani na ukawa mwisho wake Oct 2020 watakapo angukia pia vibaya sana.
 
MENE MENE TEKEL NA PERES, kiganja cha mkono kilionekana kikiandika maneno hayo ukutani. Hiyo ilikuwa ni siku ya karamu kubwa iliyoandaliwa na mfalme wa Babeli aliyeitwa Belshaza ambaye ni mjukuu wa Nebukadreza. Siku hiyo walialikwa wageni wa heshima nao wakala na kunywa wakitumia vikombe vya dhahabu na fedha na mabakuli yaliyochukuliwa katika hekalu la Yehova huko Yerusalemu, hili lilikuwa ni chukizo mbele ya Mungu ndipo katika hali ya kustaajabisha maneno yakaandikwa ukutani MENE MENE TEKEL NA PERES.

Ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Mungu kwenda kwa mfalme Belshaza ila nani atatafsiri maneno hayo? Waliletwa “wachawi” wenye akili lakini hakuna aliyekuwa na ujuzi wa kusoma maandishi yale ukutani. Baada ya tafakuri kubwa ndipo mama wa mfalme akapendekeza aitwe Daniel kwa maana yeye anaijua miungu mitakatifu hivyo ataliweza zoezi hili. Baada ya Daniel kuitwa alitafsiri maneno hayo ya Mungu.

Daniel alisema Yehova alimuondoa Nebukadreza babu ya Belshaza asiwe mfalme kwa kuwa alikuwa na kiburi sana, naye Yehova alimuadhibu Nebukadreza. Belshaza aliyajua yote yaliyompata babu yake ila naye anafuata njia ile ile ya babu yake, amechukua vikombe na mabakuli katika hekalu la Yehova na kuvinywea. Ndiyo sababu Mungu amepeleka mkono uandike maneno hayo MENE MENE TEKEL NA PERES yaani “Mungu amezihesabu siku za ufalme wako na kuzimaliza, umepimwa katika kipimo na kuonekana hufai kitu, ufalme wako wamepewa Wamedi na Waajemi.” Maneno hayo yalitimia siku hiyo hiyo na ufalme wa Belshaza ukafikia hatima yake kutokana na kiburi chake.(Daniel 5:1-31)

Naliona anguko la Chadema kama chama kikuu cha upinzani Tanzania. Ni anguko lililodhahiri kama yale maneno ukutani ila kama ilivyo kwa mfalme Belshaza ndivyo ilivyo kwa Mbowe, ameshindwa kuliona anguko hilo, MENE MENE TEKEL NA PERES. Zaidi ya mikutano na matamko yasiyo na tija sijaona jitihada za wazi za kimkakati za kuifanya Chadema iendelee kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania. Ni kama vile viongozi wa Chadema wanadhani chama chao kina “devine right” hivyo kitaendelea kupendwa na Watanzania katika mazingira yoyote yale, hii si sawa.

Chadema ina wafuasi wengi ulikilinganisha na vyama vingine vya upinzani na kama mazingira ya kisiasa yangekuwa fair huenda kina wafuasi wengi kuliko CCM ila sioni hali hii ikiendelea kutokana na viongozi wa chama kutotaka kubadili mbinu kwa kuzingatia mabadiliko ya kisiasa yaliyotokea Tanzania kwa kipindi hiki cha miaka mitatu. Kwa sasa uwepo wa Chadema unategemea zaidi huruma ya Watanzania ila wakati umekaribia ambapo huruma haitokuwa kigezo bali kitaangaliwa chama chenye nia thabiti, mipango na mikakati yakinifu ya kukiondoa chama cha Mapinduzi. Je Chadema wamejiandaa kwa hili?

Chadema sio chama cha upinzani cha kwanza kuwa na nguvu Tanzania, ilikuwepo NCCR MAGEUZI pia ilikuwepo CUF ila kwa sasa vyama hivi havina mvuto machoni mwa Watanzania walio wengi kwa sababu havikuonyesha nia dhabiti ya kusiamamia kile walichokuwa wakikinena. CHADEMA inalijua hili ila inapuuza kama mfalme Belshaza alivyopuuza yaliyoupata ufalme wa babu yake hadi ufalme wake pia ukaanguka na ali hii itaipata pia CHADEMA ikiwa haitajitathmini na kuchuka hatua stahiki kwa ajili ya kujihakikishia uhai wake.

Ni ajabu sana kuona makamanda wa CHADEMA wanavyobeza nguvu ACT-WAZALENDO kwa Tanzania bara. Wanadhani haina nafasi, nadhani wamesahau hata wao hawakuwa na nafasi mwaka 2005 ila jitihada zao za wazi zimewafikisha hapo walipo leo na ndivyo itakavyokuwa kwa ACT-WAZALENDO. Ni wazi vijana taratibu wameanza kumuamini tena Zitto Kabwe na zile kauli kuwa ni msaliti zimeanza kupungua na wengi wameanza kumuona kama shujaa atakayewafikisha nchi ya ahadi, Mbowe umeliona hili?

Wazungu wanasema, “pride comes before a fall” huu ubezaji wanaoufanya akina Yeriko Nyerere hakika ni mwanzo wa anguko la CHADEMA kama lilivyotokea kwa ufalme wa Belshaza. Makamanda ni lazima waache ego na pride zisizo na tija na waitambue nguvu ya Zitto na ACT na kutazama namna gani watasonga mbele pamoja kwa manufaa ya upinzani wote vinginevyo watagawana kura 2020 na CCM itabaki kuwa kinara. Na endapo hili halitafanyika sioni CHADEMA ikiendelea kuwa chama kikuu cha upinzani baada ya 2020.

Ni wakati wa CHADEMA kuyasoma maandishi ukutani, MENE MENE TEKEL NA PERES.
Hivyo ndivyo mlivyompumbaza Lipumba. Akajiuzulu akatoka CUF kwa kejeli. Mkamuanisha nae akaamini kuwa bila yeye walobaki watakwama.
Mlipoona CUF imepata mafanikio ambayo haijawahi, mkatumia 'dola' kumrudisha CUF.
Sasa Propesa kabaki na majivu ya nyumba mliyomsaidia kuichoma, kama afanyavyo shetani.
Hizo juhudi zako ingefaa ukazitumie kumsaidia namna ya kujenga upya imani kwa watz, avutie watu wanachama hai wenye nia ya kupigania democracy na haki za wananchi. Sijui mtafanyaje maana nyie ndio mwategemea zaidi nguvu ya dola baada ya kukosa ushawishi/mvuto.
Porojo nyingine peleka kwenu mlikozoea makelele ya mipasho ya kijiwejiwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
dawa yenu,

..kwanini act, chadema, na cuf-maalim wasiungane na kuwa chama kimoja?

..Zitto ni mbunge pekee wa chama chake.

..Maalim Seif na wenzake wameporwa chama chao, kwa maana hiyo hawakuwa na chama.

..Chadema ndiyo wenye wabunge wengi na wamesambaa maeneo mengi kuzidi chama chochote cha upinzani.

..Sasa kwanini Zitto, na Maalim hawakujiunga na Chadema na kuunda chama chenye nguvu kubwa zaidi, badala yake ni kama wameamua kuanza upya na wanataka kuifufua Act?

..Act tayari kina usajili. Lakini practically ni chama kipya kutokana na ukweli kwamba kina mbunge mmoja tu.

..naweza kuwa nimekosea, lakini kwa maoni yangu this was a GOLDEN OPPORTUNITY ya kuwa na chama kikubwa cha upinzani kitakachoi-challenge CCM na hawa ndugu zetu wameiacha nafasi hiyo ipite.

..Maalim Seif, Zitto Kabwe, na Freeman Mbowe, walitengenezewa mazingira, na sababu, za kuunda chama chenye nguvu, lakini hawakuona sababu ya kufanya hivyo.



Cc tindo, Nguruvi3, Mag3, MTAZAMO
Tumeona siasa za Tanzania zilivyo, nadhani ubinafsi wa viongozi wa upinzani ndio uliotufikisha hapa. Kuna maslahi ya pamoja na pia Kuna maslahi binafsi ila shida Ni pale maslahi binafsi yanapokuwa na nguvu kuliko maslahi ya pamoja. Maslahi ya pamoja ndani ya upinzani ni kuiondoa CCM lakini zito ana jingine zaidi ya Hilo nalo ni kwamba CCM inapotoka basi anayeingia isiwe CHADEMA bali ACT lakini bado ACT hawana nguvu hiyo. Kwa hiyo nyuma ya pazia Zitto anaihujumu CHADEMA lakini ukimtazama usoni utaona anaupigania upinzani. Sasa hii hujuma ilipaswa CHADEMA waione na kisha wajue namna gani watakaa na ACT kuhakikisha maslahi ya pamoja yanawezekana? Hii ndio hoja yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umetumia takwimu gani kuhalalisha huu upupu wako?

Hiyo Act unayoiona inakuja kuwa na nguvu ni kwa sababu ya Maalim Seif kujiunga Act au hiyo nguvu ya Act inatoka wapi?

Kama jibu lako ni kwa sababu Maalim Seif na timu yake wamejiunga Act utakuwa unakosea sana, Maalim Seif hana ushawishi wowote kwa siasa za Tanganyika.

Cuf hiyo ilikuwa inapumlia mashine na yeye akiwa sehemu ya uongozi (Katibu Mkuu).

Uzi wako huu hauna fact zaidi ya hisia hisia tu kama uko na mpnz wako kitandani.
Labda unajisahaulisha kuwa siasa za upinzani zinaangalia mtu kuliko chama kama taasisi.... Leo hii Tundulisu akihama ndio mwisho wa Chadema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Barack Obama jr Myra haha kwa mtazamo wangu yupo sahihi kwa chama kupendwa lakini viongozi kukosa mbinu mbadala kukabiliana na maccm.
Umetumia takwimu gani kuhalalisha huu upupu wako?

Hiyo Act unayoiona inakuja kuwa na nguvu ni kwa sababu ya Maalim Seif kujiunga Act au hiyo nguvu ya Act inatoka wapi?

Kama jibu lako ni kwa sababu Maalim Seif na timu yake wamejiunga Act utakuwa unakosea sana, Maalim Seif hana ushawishi wowote kwa siasa za Tanganyika.

Cuf hiyo ilikuwa inapumlia mashine na yeye akiwa sehemu ya uongozi (Katibu Mkuu).

Uzi wako huu hauna fact zaidi ya hisia hisia tu kama uko na mpnz wako kitandani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chanzo changu kinaonyesha alikuwa mfalme, ila hebu tuache kubishania rangi ya paka, tujadili uwezo wa paka kukamata panya.... Je unaona jitihada zozote za Chadema katika kuipambania nafasi yao?

Sent using Jamii Forums mobile app
Cdm inajimaliza au inahujumiwa ?!. Na kama inahujumiwa na nani na kwa faida ya nchi ?!. Wanaoihujumu chadema hawana nia njema na taifa bali kulinda maslahi yao na madaraka yao. Madaraka ambayo hayana faida kwa nchi bali maslahi yao.

Vyombo vya dola na vya maamuzi vinatumika vibaya nawe unashangilia kama zuzu. Pengine ukidhani ni ufahari kuipoteza Cdm na kurudia mfumo wa chama kimoja !!!!. Aina ya akili zilizoko CCM ndiyo zimefanya Tz kuwa miongoni mwa nchi 10 bora masikini .


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom