Zamani vijana wa CCM walikuwa imara sana kukijenga chama,nasema zamani enzi chama cha wakulima na Wafanyakazi,walijali na kuzifuata kanuni za chama chao wakaweka taratibu zote,leo wenyechama hawapo tena si wakulima na wafanyakazi hataa ni matajiri na viongozi wa serikali,vijana hawapo wanalumbana kwa ushabiki wa watoa nia na si mustakabali wa Taifa wazee wa CCM nao kushney haya yanatokea wameweka mikono nyuma tuu,aibu kubwa ccm kwa haya yanayotokea...ndani ya miaka 10 uongozi wa ccm ulianguka mara kadhaa akibaki mwenyekiti pekee,na hata yeye aliponea kiduchu kutunguliwa nafasi hiyo,ni aibu kwa chama hiki kilicholeta ukombozi wa baadhi ya nchi za Afrika,leo ushabiki,Rushwa ufisadi kuvunja sheria na kutofuata kanuni ni jambo la kawaida kabisa kwa ccm,miradi yote ya chama hiki haikinufaishi chama hata mgombea wa nafasi ya njumba kumi kumi lazima avunje kanuni,amini nawaambia CCM kwa mwendo huu mtatuletea machafuko makubwa na hayata koma.Vijana wa CCM mko wapi angalieni Tanzania kwa Jicho la mbali zaidi.