Kipimo cha DNA...Ungekuwa Ungefanyaje?

Kipimo cha DNA...Ungekuwa Ungefanyaje?

Wanawake sio watu wa kuwaamini sana sema unachoweza kufanya ni kwenda kupima nae kisiri siri,hakuna kitu inauma kama kujua unalea mtoto wa mbaya wako,bora hata awe alikuja nae. Kuhusu kutishia kuondoka ni bora afanye hivyo manake naweza kumchinja kabisa.
 
^^
The guilt are always afraid....
^^

Wrong!
Aliyechepuka kweli alijua tangu mimba kuwa si ya mume,alimchunguza tangu mtoto akiwa kachanga na akajua kuna siku iso jina mambo yatakuwa hadharani hivyo anajipanga mapema.
Anayeumia na kujiona katusiwa ni yule aliye faithful kwa mumewe,akiambiwa mtoto akapimwe only because hajafanana na baba yake inaumiza sana,inaleta maswali mengi kwa kweli na hata kipimo kiki prove ni mtoto wa Mr damage inabaki kubwa kwenye mahusiano ya wawili hao!
Labda kama mwanamke hana nyongo!!
 
Hahaaa! Umesababisha nicheke Himidini!
Hivi kuna wanaoongoza kuzaa nje ya ndoa kama wanaume? Au kwa sababu pua zenu hazikui sambamba na mimba mlizosababisha ndio mnajiona mko salama sana na kujivika utakatifu msiokuwa nao?
Kupeleka mtoto kupima DNA ni kumtusi mwenza wako,period!!

Sawa nakubalina na wewe as u said. Sasa inatokea mumeo amekufanyia surprise, na akamchukua mtoto kwenda kumpima na at the end ikabainika kuwa huyo mtoto...vinasaba havifanani na hitimisho ni kuwa mtoto sio wake. Sasa je kati ya mke au mume nani hapo atakuwa ame-mtusi mwenzake? come this way please!
 
Wrong!
Aliyechepuka kweli alijua tangu mimba kuwa si ya mume,alimchunguza tangu mtoto akiwa kachanga na akajua kuna siku iso jina mambo yatakuwa hadharani hivyo anajipanga mapema.
Anayeumia na kujiona katusiwa ni yule aliye faithful kwa mumewe,akiambiwa mtoto akapimwe only because hajafanana na baba yake inaumiza sana,inaleta maswali mengi kwa kweli na hata kipimo kiki prove ni mtoto wa Mr damage inabaki kubwa kwenye mahusiano ya wawili hao!
Labda kama mwanamke hana nyongo!!

^^
Nimekupata vizuri, Kusema umpime mtoto kisa tu hajafanana na mzazi hiyo hata genetics inakataa! Nakubali..
Hoja yangu ni hii, kama kweli u mwaminifu kwa nini uogope DNA?
^^
 
Sawa nakubalina na wewe as u said. Sasa inatokea mumeo amekufanyia surprise, na akamchukua mtoto kwenda kumpima na at the end ikabainika kuwa huyo mtoto...vinasaba havifanani na hitimisho ni kuwa mtoto sio wake. Sasa je kati ya mke au mume nani hapo atakuwa ame-mtusi mwenzake? come this way please![/QUOTE]

Here I am.
Nisome vizuri mkuu hapo juu,aliyebambika mtoto(aliyechepuka aka conceive) huwa haumii wala kuona ametusiwa!
Alishajipanga mapema na possible baba halali aliambiwa mapema kabla baba mlezi hujastuka,ukianza tu kumpekua sana mtoto mama naye anaanza ku pack mabegi anajua safari imewadia!!
Vipi ukiwa na mke "Hewalla bwana",akakubali mkaenda kupima mkakuta mtoto ni wako kweli,unamuomba radhi mkeo au unaanza kujichekesha chekesha?
 
^^
Nimekupata vizuri, Kusema umpime mtoto kisa tu hajafanana na mzazi hiyo hata genetics inakataa! Nakubali..
Hoja yangu ni hii, kama kweli u mwaminifu kwa nini uogope DNA?
^^
Siiogopi DNA hata kidogo,ila naumizwa na imani ndogo aliyonayo mume wangu kwangu.
Kama haniamini kiasi hicho sioni sababu ya kuendelea kuwa naye,kumuonesha siogopi naweza kwenda naye kupima then akishaambiwa mtoto ni wake namuuliza umeridhika au kuna kipimo kingine?
Kama hamna,nabeba kila kilicho changu,namshukuru kwa kutoniamini naenda kuanza maisha upya!!!
 
Put yourself in the woman's shoes,think and then judge!

^^
Kuna usemi unasema, Kuku mweupe haogopi mwewe! Yaani mtu asiye na kosa hana hofu!
Hata nikivaa viatu vya mwanamke, hulka ya mwanamke katika hatua hii itakuwa ile ya kutaka kuhurumiwa, kujificha nyuma ya machozi, kuonekana hajakosea!
Kama kweli ni Kuku mweupe excuse za nini mpaka aseme haaminiki au anaenda kuanzisha maisha?
Something alarming
^^
 
Hahaaa! Umesababisha nicheke Himidini!
Hivi kuna wanaoongoza kuzaa nje ya ndoa kama wanaume? Au kwa sababu pua zenu hazikui sambamba na mimba mlizosababisha ndio mnajiona mko salama sana na kujivika utakatifu msiokuwa nao?
Kupeleka mtoto kupima DNA ni kumtusi mwenza wako,period!!

^^
Sijafanya utafiti kiasi cha kuwa na takwimu hapa kubaini kundi lipi linaongoza kuzaa nje ya ndoa!
Ikiwa kweli, uaminifu ndiyo zawadi bora uwezayo kumpa mwenza wako basi pasiwepo na kujitetea kusiko maana kati ya mume au mke!
^^
 
Last edited by a moderator:
^^
Sijafanya utafiti kiasi cha kuwa na takwimu hapa kubaini kundi lipi linaongoza kuzaa nje ya ndoa!
Ikiwa kweli, uaminifu ndiyo zawadi bora uwezayo kumpa mwenza wako basi pasiwepo na kujitetea kusiko maana kati ya mume au mke!
^^

You can say that again and again mkuu!!!
 
Beba mtt wako kama unaenda nae shoping pita kwenye vipimo chukua rudi jm kwenye majibu utarudi mwenyewe haina shida
 
Siiogopi DNA hata kidogo,ila naumizwa na imani ndogo aliyonayo mume wangu kwangu.
Kama haniamini kiasi hicho sioni sababu ya kuendelea kuwa naye,kumuonesha siogopi naweza kwenda naye kupima then akishaambiwa mtoto ni wake namuuliza umeridhika au kuna kipimo kingine?
Kama hamna,nabeba kila kilicho changu,namshukuru kwa kutoniamini naenda kuanza maisha upya!!!

^^
Na hapa ndipo palipo na kosa la wanawake wengi.. KUTAKA KUAMINIWA WAKATI WOTE NA WAUME ZAO
hata kama kuna mambo mwanaume anayaona hayako sawa! Kuna wanaume ni mabingwa wa kutilia shaka chochote! Kuna wakati maisha ya ndoa ni mchezo wa 'kaa chonjo'
Kosa la pili, kwa sababu anahisi haaminiki, basi jawabu ni kuondoka, kuzira au kuamua kuthibitisha kuwa anaweza kuvunja uaminifu asigundulike.
Hakuna nyakati zinazohitaji HEKIMA na BUSARA za mke kama hizi
^^
 
Dhana ni kitu kibaya sana...kama kuna kila sababu zinazokupelekea usimuamini mtu hapo sawa lakini kama mtu mnaishi kwa amani kabisa halafu unazuka mkapima DNA from nowhere atakuelewaje lazima ujipange haswa kujieleza sababu zinazoeleweka zikapelekea wewe kuchukua hatua hizo!

Endapo nina shaka yoyote juu ya jambo fulani baina yetu basi ni jukumu la mke wangu kuniondolea hofu hiyo. Nafahamu matatizo yatakayo ibuka endapo ikigundulika kuwa ni kweli mtoto wangu ila ni vipi endapo itabainika si mtoto wangu?
 
[/B][/COLOR]
You can say that again and again mkuu!!!

^^
Yeah, I can repeat it countless times, If am right, and your faithful why then do you manufacture excuses before the test? Ennie
^^
 
Last edited by a moderator:
Naona mpambano wa moto moto hapa,siku zote anayejijua ana makosa huwa anatafuta sababu za kuuficha uovu wake,mambo ya kusema unanitukana,mara umenichoka,au naoenda kwetu ni uoga tu baada ya kuja mambo yamekuwa si mambo,kama unajiamini kwamba haujawah kutoka na mwingine kwanini uogope kupima?
 
^^
Na hapa ndipo palipo na kosa la wanawake wengi.. KUTAKA KUAMINIWA WAKATI WOTE NA WAUME ZAO
hata kama kuna mambo mwanaume anayaona hayako sawa! Kuna wanaume ni mabingwa wa kutilia shaka chochote! Kuna wakati maisha ya ndoa ni mchezo wa 'kaa chonjo'
Kosa la pili, kwa sababu anahisi haaminiki, basi jawabu ni kuondoka, kuzira au kuamua kuthibitisha kuwa anaweza kuvunja uaminifu asigundulike.
Hakuna nyakati zinazohitaji HEKIMA na BUSARA za mke kama hizi
^^


Mie naona hekima na busara vingeanzia kwa mume,ajiulize mkewe atakavyojisikia kama si kweli kuwa alichepuka.
Kama una sababu ya kutomuamini,tafuta ushahidi hata mdogo tu kuwa mke si muaminifu then komalia kipimo.
USINIAMINI WAKATI WOTE,ILA USINITUHUMU KAMA HUNA USHAHIDI.
Ni bora niende ndio ili nipate amani ya nafsi,mtu asiyeweza kufanya hata uchunguzi mdogo tu anaendeshwa na hisia na kukurupuka kama chafya hata katika vitu vinavyohitaji umakini mie wa nini?
 
Back
Top Bottom