sakwano
JF-Expert Member
- Sep 15, 2021
- 304
- 828
Moja kwa moja naomba nijikite kwenye mada, miezi kadhaa iliyopita nilipata kufahamiana na jamaa mmoja ambae aligeuka kuwa rafiki yangu mpenzi(best friend). Rafiki huyo alikua akiishi kwa raha na furaha pamoja na demu wake..(hajamuoa).Alikuwa akimsifia sana na pia kujihakikishia mbele yangu na hata baadhi ya marafiki wengine kuwa haitatokea akamuacha.
Kwa upande wangu niiliipenda hii familia ya best yangu na mara kadhaa nilienda kuwatembelea kama ndugu zangu..
Binafsi:
Mimi siku ya kwanza kumuona huyu demu wa jamaa nilimpenda sabb ni wife material, lakini nilijisemea tu moyoni na moyo ulikataa kufanya wizi wala ushawishi wowowte wa kumla kimasihara nilimuheshimu na maisha yakaendelea.
Miezi kadhaa kupita jamaa akapata demu mwingine,hii kitu ilipelekea mahusiano kuvunjika sabb jamaa Alikuwa akimcheat demu wake pasipo na umakini wowote hatimae kusababisha kuporomoka kwa mahusiano yao.
Demu:
Upande wa demu mahusiano kwake yakawa ni jeraha pamoja na majuto..ukizingatia alimpenda sana jamaa yake. Baada ya hayo yote mimi nikageuka kuwa mfariji na mrudisha mahusiano.Hali hii ya kuwa karibu na demu wa jamaa ilitupelekea kuanzisha mahusiano ya kimapenzi.
Ilikuwa ni rahisi sana kwa sabb toka watengane yule binti alihamia kwangu mm nikawa namficha nyumbni kwangu hata ikitokea jamaa kaja kunitembelea mimi nilikuwa nikimfungia chumbani kabla hajaonekana. Nilifahamu fika jamaa angejua angeniletea noma kubwa sana kwa sabb jamaa ni mkorofi..namfahamu vizuri.
Ndoa:
Baada ya kuhofia changamoto za huyu jamaa mimi nilimrudisha binti kwao,nikawa naishi mwenyewe kama ilivyokuwa nikiishi mwanzo,..
Kwa ufupi tu mimi nataka nimuoe huyu binti kwa sababu nimejirizisha ananifaa ...je?jamaa akijua itakuwaje?na kwenye harusi nimpe mualiko ama vipi?...angalizo ni kuwa jamaa hajui kama mimi na mahusiano na Aliekuwa mpenzi wake,
Niko njiapanda wakuu naombeni ushauri wenu...mtanisamehe kwa uwandishi mbaya ila imani yangu nimeeleweka.
Ahsanteni sana poleni na majukumu.
Kwa upande wangu niiliipenda hii familia ya best yangu na mara kadhaa nilienda kuwatembelea kama ndugu zangu..
Binafsi:
Mimi siku ya kwanza kumuona huyu demu wa jamaa nilimpenda sabb ni wife material, lakini nilijisemea tu moyoni na moyo ulikataa kufanya wizi wala ushawishi wowowte wa kumla kimasihara nilimuheshimu na maisha yakaendelea.
Miezi kadhaa kupita jamaa akapata demu mwingine,hii kitu ilipelekea mahusiano kuvunjika sabb jamaa Alikuwa akimcheat demu wake pasipo na umakini wowote hatimae kusababisha kuporomoka kwa mahusiano yao.
Demu:
Upande wa demu mahusiano kwake yakawa ni jeraha pamoja na majuto..ukizingatia alimpenda sana jamaa yake. Baada ya hayo yote mimi nikageuka kuwa mfariji na mrudisha mahusiano.Hali hii ya kuwa karibu na demu wa jamaa ilitupelekea kuanzisha mahusiano ya kimapenzi.
Ilikuwa ni rahisi sana kwa sabb toka watengane yule binti alihamia kwangu mm nikawa namficha nyumbni kwangu hata ikitokea jamaa kaja kunitembelea mimi nilikuwa nikimfungia chumbani kabla hajaonekana. Nilifahamu fika jamaa angejua angeniletea noma kubwa sana kwa sabb jamaa ni mkorofi..namfahamu vizuri.
Ndoa:
Baada ya kuhofia changamoto za huyu jamaa mimi nilimrudisha binti kwao,nikawa naishi mwenyewe kama ilivyokuwa nikiishi mwanzo,..
Kwa ufupi tu mimi nataka nimuoe huyu binti kwa sababu nimejirizisha ananifaa ...je?jamaa akijua itakuwaje?na kwenye harusi nimpe mualiko ama vipi?...angalizo ni kuwa jamaa hajui kama mimi na mahusiano na Aliekuwa mpenzi wake,
Niko njiapanda wakuu naombeni ushauri wenu...mtanisamehe kwa uwandishi mbaya ila imani yangu nimeeleweka.
Ahsanteni sana poleni na majukumu.