Kiongozi yeyote anayewapa watu vyeo kwa kulipa fadhila anafaa?

Sijui ni kwanini watu wanaangalia kila jambo kwa mboni za kisiasa badala ya masilahi mapana ya nchi.

Jambo zuri rekodi zipo hivyo wengine tunapozungumza tuna uhakika

Hatuhitaji kufanya makosa yale yale kwasababu tu wapo wanaofanya makosa hayo hayo
Hii ni dhana mbovu sana

Huyu bwana alisimama kupinga ukuu wa Wilaya, leo anarudi kuwaambia watu wale wale, taswira yake kama kiongozi inakuwa wapi?

Lakini pia lazima tujifunze kwa viongozi wetu waliotangulia. Wapo walioacha masialhi yao binafsi kutetea nchi. Hata kama ni wachache, hatupaswi kuishi kwa historia yao tu, ni wakati tujenge historia ya kizazi hiki. Je, haya ndiyo tunatarajia kwa vijana kama hawa?

Lakini pia mteule alienda mbali, si kwa ukuu wa Wilaya, alifikia mahali anapotosha umma, anazungumza uongo usiohitaji certificate.
Leo kazawadiwa kwasababu hiyo tu! Tunajenga nchi kweli?

Tukianza kutetea haya, ipo siku watu watateua wajomba zao, nao watasema wanaweza kufanya nao kazi vizuri, kuna shida gani!!

Hebu tuangalie nchi kwa upana wake. Nipo katika rekodi nikipinga nafasi za ukuu wa wilaya. Ninapoona ukuu huo unatolewa kwasababu tu fulani anapepeta sana , inatia shaka

Kiongozi anateuliwa kwasababu alimtwanga mzee fulani katika kongamano!
Ndio tunahitaji hayao?

Halafu tukisema lipo tatizo, wapo wanaosema mbona Mrema naye alitwangwa kule Tanga? ina make sense kweli
Kwani mkuu wewe hili hauliangalii kwa mboni za kisiasa?...Hauoni kama uliyoaandika kwenye bandiko hili ni siasa tupu....Bandiko la kisiasa lazima lijadiliwe kwa mtazamo wa kisiasa Chifu...
 
Bavicha mnapigika kweli siku hizi, mmekosa hoja maskini mnalilia sisiemu eti wawachague chadema ktk nyadhfa, mpaka 2020 sijui mtakuwa mmepigika kiasi gani.
 
Unamsema mr liabilty alipohamia chadema akalazimisha watu wake wawepo kwenye nafasi za ubunge na viti maalum
Amepatikana mwenye chongo katika jamii ya vipofu hivyo nyie vipofu lazima mshangilie ili hali nae ana chongo!
 
Kuna kiongozi wa nchi fulani yeye amempa cheo cha ukuu wa wilaya mtu kama kulipa fadhila huyu hafai kuitwa kiongozi NA ALAANIWE
 
Ukiona kiongozi yeyote chini ya jua anachagua viongozi au watendaji kwa kulipa fadhila bila Kuangalia utendaji wa mtu jua kuna kasoro hapo na usitegemee jipya! Huwezi jaza watu wa propaganda kwenye uongozi utegemee UTENDAJI!

hiki kinachofanyika kwa sasa kitazamwe upya, kiukwel si haina nzuri ya kupata viongozi, wasiojua kujipendekeza kwa wakubwa itakua vigumu sana wao kupata nafasi mbalimbali, au wasiokua jiran kwenye kipndi mbalimbal vya tv kama walivyo hao akina polepole, nadhan na yule anayepiga makelele chanel ten angekua siyo mzee angeweza pata.
 
Je,ikitokea anapatikana kiongozi wa aina hii katika jamii yako,utaaridhika nae na kumwamini?

Mtu wa aina hii ana mapenzi na watu wake au ana mapenzi tu na baadhi ya watu?

Kipimo kizuri cha kiongozi huwa ni muda hivyo ni busara kuweka akiba ya maneno pale unapopata kiongozi mpya katika jamii yako.

Ni ushauri tu.
Kuna aliyekuwa mgombea aliahidi hadi vyeo katika idara nyeti za serikali kwa watakaomfanikisha kuingia magogoni.
 
Mbowe kampa mkewe mdogo ubunge viti maalum,Ndesamburo mtoto wake mbunge Viti maalum, Lowasa aliwaahidi kuwapa watu vyeo ndani ya idara mbalimbali.
 
Mbona hapa vyama vingine ni hivyo hivyo tu....hebu angalia mgawanyo wa viti maalumu......lazima wahusika kwa namna moja au nyingine wawe na kauhusiano fulani na wakubwa wa chama......
Sasa na wao kama wakipewa urais watashindwa kufanya waliyoyafanya wenzao.......ikiwa nafasi kama za viti maalumu wanagawana kama mkate wa familia....?!!

Nchi hii hakuna mpambanaji mwenye kuwatetea wanyonge kwa dhati kabisa bali kuna wachumia tumbo tu wanaojifanya kuukosoa mfumo kwa kuwa wao hawapo kwenye huo mfumo wa wizi......wakisha ingia humo wanakuwa kimya kabisa....na wengine bila ya aibu wanawasifia hao hao......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom