Hapa ndipo tunapotofautiana. Kazi nyingine tunaambiwa tutangulize utaifa mbele, wakati wengine wanatakiwa watangulize maslahi mbele. Juzi wabunge wamapewa 1Milioni kila mmoja kwa ajili ya kuhamasisha sensa, wakati ambapo wabunge haohao hadi sasa tangu wamalize kikao cha bunge, wamebana huko mijini, na huku majimboni hawajafika. Hiyo milioni waliyopewa haijafanyiwa kazi, na wala haitarejeshwa. wakati huohuo, karani analazimishwa aende kituoni bila kulipwa, eti atangulize utaifa, akale nini huko????, akalale wapi????, akafanye nini????. Hivi utaifa ni kutesana????
Tunaambiwa eti Ualimu ni kazi ya wito, Udaktari ni kazi ya wito, je! ubunge si kazi ya wito??????? Tuache siasa, tufanye kazi.
Nimepata habari za kuaminika kutoka kwa rafiki yangu ambaye naye ni karani wa sensa hapa DSM kuwa yule kiongozi wao aliyeonekana kupitia tv mbalimbali(kijana mnene mweupe hv) akisisitiza serikali kuwalipa pesa yao yote ya semina ya siku saba jina lake limekatwa,na sasa hajapangiwa kituo na hajaripwa posho ya ukarani wa sensa.
mytake:Hawa makarani wanapaswa kutanguliza utaifa mbele na sio maslahi yao,wakumbuke walimu na madaktari n.k wote wako kazini kwa kutanguliza uzalendo
Nae kesha sema haesabiwi
Umenena vyema. Mimi karani ila hali ya maandalizi ni mbaya sana. Hakuna tshirt wala kofia. Vitambulisho ndio vijibandiko vya uchochoroni. Mwitikio wa watu ni kidogo sana. Mwaka wa dhaifu na sensa dhaifu.
Ukipanda utendaji DHAIFU utavuna mazao DHAIFU.
Hapa ndipo tunapotofautiana. Kazi nyingine tunaambiwa tutangulize utaifa mbele, wakati wengine wanatakiwa watangulize maslahi mbele. Juzi wabunge wamapewa 1Milioni kila mmoja kwa ajili ya kuhamasisha sensa, wakati ambapo wabunge haohao hadi sasa tangu wamalize kikao cha bunge, wamebana huko mijini, na huku majimboni hawajafika. Hiyo milioni waliyopewa haijafanyiwa kazi, na wala haitarejeshwa. wakati huohuo, karani analazimishwa aende kituoni bila kulipwa, eti atangulize utaifa, akale nini huko????, akalale wapi????, akafanye nini????. Hivi utaifa ni kutesana????
Tunaambiwa eti Ualimu ni kazi ya wito, Udaktari ni kazi ya wito, je! ubunge si kazi ya wito??????? Tuache siasa, tufanye kazi.
Nakubaliana nawe katika hili. tatizo mara nyingi ni kutofanya mambo kwa umakini. Taarifa sahihi ni jambo la msingi sana. Unapomwambia mtu kuwa utaratibu wa malipo upo namna fulani na lazima uheshimu, kama kuna tatizo ni bora utumie utaratibu muafaka kumwarifu ili ajue kuhusu mabadiliko badala ya kutumia ubabe.
na si ajabu hapa nikapewa BAN, nitaikubali!
jitayarishe na ban.. Ha ha ha.. Lkn umesema ya moyoni..
Sent from my BlackBerry using JamiiForums
mi naona wameamua kufanya tu ili litimie la kwamba tunahesabu watu kila baada ya miaka kumi na kuharibu kodi zetu. Haiwezekani vitambulisho viwe vya kisanii namna ile! Yaani picha mtu akabandikie nyumbani! Hakuna hata muhuri wa mamlaka! Hivi fikra zetu waafrica ndo zinaishia hapa,? Kwamba kwenye jambo lolote we ni kuiba tu hata kama linasaidia kwenye mipango muhimu? Ngoja vijana wawatengenezee data za uongo tuambiwe tuko milioni 27!