tikatika
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 2,330
- 4,115
Sisi binadamu kwa asili ni waongo!! Na kwa mwenyezi Mungu uongo ni dhambi. Tunapaswa kuishinda hii dhambi ya uongo! Lakini mara nying watu husema uongo kwa mtu mmoja mmoja na sio kwa jamii nzima. Na uongo uliozoeleka kwa sasa ni kudanganya ulipo kwa mtu aliye mbali nawe. Tuombe Mungu kwa hili atuepushie tulishinde.
Lakn katika maisha ya kawaida katika jamii tuna watu ambao husifika kwa uongo! Ina maana hao huongea uongo uliopitiliza. Mfano kuna rafiki yangu mmoja alikua mwongo hadi alikua anaboa. Sasa safari hii alikua anamdanganya mchumba wake wa kike had wakaachana.alikua na mchumba msom aliye amua kuwa hakimu. Sasa jamaa wakati anamdet alijitangaza kwamba naye ni msomi wa kiwango cha juu mpaka amefikia ngazi ya uhandisi. Huku aliishia la saba, (sio dhambi kuishia la saba). Na masomo yake mengine kasomea nchi za ng'ambo ikiwemo china. Huku kusafiri kwame koooooote kaishia kongo huku akiwa kondacta wa roli!!!.
Sasa alikua anamshangaza sana mchumba wake kwa kumkataza pale anaponogesha maongez yao kwa kuchomekea kizungu. Jamaa alikua mkali kweli kwa mchumba wake asitumie kizungu maana kati yao hakuna mzungu kwanini achanganye kizungu wakati hamna mzungu!. Huku akimpiga mkwala mchumba wake kwamba yeye ni bingwa wa kichina, vip na yeye akiamua kunogesha na maneno ya kichina?? Lakn mkwala huo ilikua ni kuogopa kuumbuka pale na yeye atakapotaka kuchanganya na lugha ya malkia atajikuta ni mwendo wa kiswangilishi! Sasa akipiga mkwala anatupia maneno ya uongo na ukweli ya kichina feki . Si unajua kichina ni rais kuongea kwa mtu asiye kijua ili mrad unamalizia na ng. Ching chong pyong yong n.k. Waliishia kuachana maana karibia kila kitu jamaa alikua anamdanganya mwanamke.
Sasa twende kwa viongoz wetu waliopita na waliopo. Wawe wa upinzani au chama tawala. Huwa wanatudanganya sana . Ni wakati mwafaka kuwaweka hapa na kuweka maneno yao ya uongo. Hii itafanya wajue wananchi tunawafatilia kwa karibu sana matamshi yao, hivyo wanapaswa kuwa makini wanapotamka.
Kwangu mimi mtu pekee ambaye hunishangaza sana na aina ya uongoz wake na maneno yake ni rais wangu wa sasa. Aisee naweza kusema ni mwongo sijapata ona kiongoz mwongo kama huyu tangu nipate akili. Tena ni kwa muda mfupi sana: sijui akifikisha miaka mitano nitakua nimesikia kauli ngapi toka kwake zilizo jaa upotoshaji wa makusudi.
Naweka kauli zake chache zilizokua zimejaa uongo mkubwa ila aliongea huku akiwa na amani usoni ila sijui moyoni.
Hakuna serikali duniani iliyowahi kuwajengea waathirika wa maafa yeyote duniani. Na mimi serikali yangu haiwejengei! Huku anamalizia kwa kusema msema kweli mpenz wa Mungu. Je hili lina ukweli??
Ujenzi wa reli ya mwendokasi unajengwa kwa hela ya ndani na hela ipo . Baada ya siku mbili anaomba msaada na mikopo kwa viongoz waliomtembelea kwa ujenzi wa reli hiyo hiyo! Baadaye tena anaongea na wananchi wale wale kwa kulalamika . Wezi hawa wamesababisha tushindwe kujenga reli ya kwenda dodoma hadi tunaenda kukopa wakati tuna mahela mengi kwenye dhahabu.
Na hupenda walio chini yake waseme mambo makubwa makubwa ili kumkweza . Na hii tabia hutumika sana kwa mtu mpenda sifa zisizo na msingi. Yaan angetamani kila mtu amsifie. Kwangu mimi ndiye kiongozi pekee aliye na aina ya uongoz wenye kupenda sifa zisizo stahili ila huzilazimisha kwa kutumia hata lugha za uongo ili aonekane kiongoz bora kuwahi tokea tangu tupate uhuru.
Huyu ndio kiongoz mpotoshaji (mwongo) kupita wote niliowahi kuwasikia. Kwenye hotuba zake nyingi lazma umsikie akijikweza.
Yapo maneno meng sana kayaongea ila sina sababu ya kujifanya peke yangu ndio nimemsikia ni wakati wako na wewe kuweka kauli zake hapa. Au za wengine unaohisi kwako wewe ndio waongo kupitiliza.
Lakn katika maisha ya kawaida katika jamii tuna watu ambao husifika kwa uongo! Ina maana hao huongea uongo uliopitiliza. Mfano kuna rafiki yangu mmoja alikua mwongo hadi alikua anaboa. Sasa safari hii alikua anamdanganya mchumba wake wa kike had wakaachana.alikua na mchumba msom aliye amua kuwa hakimu. Sasa jamaa wakati anamdet alijitangaza kwamba naye ni msomi wa kiwango cha juu mpaka amefikia ngazi ya uhandisi. Huku aliishia la saba, (sio dhambi kuishia la saba). Na masomo yake mengine kasomea nchi za ng'ambo ikiwemo china. Huku kusafiri kwame koooooote kaishia kongo huku akiwa kondacta wa roli!!!.
Sasa alikua anamshangaza sana mchumba wake kwa kumkataza pale anaponogesha maongez yao kwa kuchomekea kizungu. Jamaa alikua mkali kweli kwa mchumba wake asitumie kizungu maana kati yao hakuna mzungu kwanini achanganye kizungu wakati hamna mzungu!. Huku akimpiga mkwala mchumba wake kwamba yeye ni bingwa wa kichina, vip na yeye akiamua kunogesha na maneno ya kichina?? Lakn mkwala huo ilikua ni kuogopa kuumbuka pale na yeye atakapotaka kuchanganya na lugha ya malkia atajikuta ni mwendo wa kiswangilishi! Sasa akipiga mkwala anatupia maneno ya uongo na ukweli ya kichina feki . Si unajua kichina ni rais kuongea kwa mtu asiye kijua ili mrad unamalizia na ng. Ching chong pyong yong n.k. Waliishia kuachana maana karibia kila kitu jamaa alikua anamdanganya mwanamke.
Sasa twende kwa viongoz wetu waliopita na waliopo. Wawe wa upinzani au chama tawala. Huwa wanatudanganya sana . Ni wakati mwafaka kuwaweka hapa na kuweka maneno yao ya uongo. Hii itafanya wajue wananchi tunawafatilia kwa karibu sana matamshi yao, hivyo wanapaswa kuwa makini wanapotamka.
Kwangu mimi mtu pekee ambaye hunishangaza sana na aina ya uongoz wake na maneno yake ni rais wangu wa sasa. Aisee naweza kusema ni mwongo sijapata ona kiongoz mwongo kama huyu tangu nipate akili. Tena ni kwa muda mfupi sana: sijui akifikisha miaka mitano nitakua nimesikia kauli ngapi toka kwake zilizo jaa upotoshaji wa makusudi.
Naweka kauli zake chache zilizokua zimejaa uongo mkubwa ila aliongea huku akiwa na amani usoni ila sijui moyoni.
Hakuna serikali duniani iliyowahi kuwajengea waathirika wa maafa yeyote duniani. Na mimi serikali yangu haiwejengei! Huku anamalizia kwa kusema msema kweli mpenz wa Mungu. Je hili lina ukweli??
Ujenzi wa reli ya mwendokasi unajengwa kwa hela ya ndani na hela ipo . Baada ya siku mbili anaomba msaada na mikopo kwa viongoz waliomtembelea kwa ujenzi wa reli hiyo hiyo! Baadaye tena anaongea na wananchi wale wale kwa kulalamika . Wezi hawa wamesababisha tushindwe kujenga reli ya kwenda dodoma hadi tunaenda kukopa wakati tuna mahela mengi kwenye dhahabu.
Na hupenda walio chini yake waseme mambo makubwa makubwa ili kumkweza . Na hii tabia hutumika sana kwa mtu mpenda sifa zisizo na msingi. Yaan angetamani kila mtu amsifie. Kwangu mimi ndiye kiongozi pekee aliye na aina ya uongoz wenye kupenda sifa zisizo stahili ila huzilazimisha kwa kutumia hata lugha za uongo ili aonekane kiongoz bora kuwahi tokea tangu tupate uhuru.
Huyu ndio kiongoz mpotoshaji (mwongo) kupita wote niliowahi kuwasikia. Kwenye hotuba zake nyingi lazma umsikie akijikweza.
Yapo maneno meng sana kayaongea ila sina sababu ya kujifanya peke yangu ndio nimemsikia ni wakati wako na wewe kuweka kauli zake hapa. Au za wengine unaohisi kwako wewe ndio waongo kupitiliza.