Kioja cha mhudumu wa basi la ngorika:

Kioja cha mhudumu wa basi la ngorika:

Tanzania Tunatatizo kubwa kabisa la Customer Care nazani kuliko nchi yoyote ile Duniani, na hili ndo litatumaliza kibiashara, mhudumu unakuta anatkana hadi wateja,

Na hii iko kila mahari, Madukani, Mahotelini, Guest house na kazalika, Mtu anaanzisha project kubwa kabisa ya mamilino ya pesa anamchukua, Mchumba/Mme/mke/Dada/Kaka/shemeji/mjomba/mama/baba/shangazi na kumuweka pale bila elimu yoyote matokeo yake ni wahusika kutoa lugha za ajabu kwa wateja, wanaona mteja kama shidando zimempeleka pale.

Mabinti nao pale wanawaz kutongozwa masaa 24 tu, nakumbuka kuna gest mmoja tulifikia tulikuwa kikazi, kwa sababu tulikuwa na ratiba ya kurudi tena mara nyingine, tuliomba mhudumu namba ya simu ili basi siku tunakuja tumpigie kwa ajili ya booking, Mhudumu alikuwa Mdada, aligoma kabisa kutoa namba yake,

Sehemu zingine/Nchi zingine unaweza fika mhudumu akakuchangamkia hadi busu na hag, na wewe ukazani amekufia kube yeye yuko kibiashara na wala hayupo kwa ajiri ya kustarehesha watu,

Bongo kuna tatizo kubwa sana
 
Leo nimewaambia live sipandi bus lao wapiga debe wa ngorika moshi stand nikapanda buffalo raha mstarehe, tupo foleni kuingia ubungo sasa
 
wameshaanza kuringa sasa maana wanajua december hawatapiga debe tena abiria kibao ndio jeuri yao
 
huyu ni dereva wa NDEJELA jamani hii gari ni nzuri kupanda usipime utafikiri uko sijui kwenye ndege ama kwenye hoteli fulan nzuri kwa huduma zao


Leo NDENJELA (NDEJELA)? kapata promo ya kutosha humu, wasivimbe bichwa tu kama la mgema....
 
Kwa route ya Dar Mbeya natoa ushauri wa bure kabisa, mwanaJf yeyote atakayesafiri njia hiyo ajaribu kupanda basi linaitwa NDENJELA , hakika utashangaa na kujiuliza kwanini wanamjali abiria kiasi kile.
Basi linapoondoka pale Ubungo unaweza kujisahau ukadhani upo kwenye ndege, maana utasikia sauti mororo ya mdada ikiwasalimia, kisha wanatoa briefing ya safari yote na kusisitiza kuwa abiria ukiwa na tatizo lolote usisite kumwita mhudumu akusaidie.
Basi kama hilo likija route ya Arusha hakika akina Ngorika, Saibaba, Dar Xpress wote watatafuta vigagura ili wawawekee ndumba lipinduke.

Mkuu PakaJimmy,

Ile ndege ya watu - FastJet - imeshaanza safari za kwenda Mbeya...!
 
Niliwahi kupanda basi la Kilimanjaro express toka dar kw Moshi. kwenye tiketi hawakuniandikia namba ya gari, na wakati nilipokuwa nakata tiketi ofisini niliwauliza mbona hakuna namba ya gari? nikiingia ndani (UBT) nitalijuaje? wakasema ukiingia wewe nenda kule mabasi yetu yanapopaki kisha uliza basi namba moja.

Nikafanya kama walivyosema nakule ndani nikapokelewa vizuri tukwenye basi.

Tulianza safari tulipofika Kibaha kuna trafic akaingia ndani ya basi na kutuomba baadhi ya abiria, hususan tulokuwa siti za mbele, tumuoneshe tiketi. Alipochukua yangu akaniuliza kwanini haina namba ya gari nikamueleza ukweli wenyewe. matokeo yake jamaa wakapigwa faini palepale tukiwa tunaona na trafic akatueleza abiria kwa ufupi kuhusu tiketi kuwa ni sheria, inatakiwa iandikwe;

Jina la msafiri
Anakotoka
Anakokwenda
Kiasi cha nauli
Muda wa kuondoka gari
Namba ya kiti
Namba ya gari

Kisheria kukosa kumuandikia msafiri tiketi kwa ukamilifu mwenye basi atawajibika.

Lakini hali hiyo ya kufanya ubabaishaji kwenye tiketi pale Ubungo bado inaendelea kwa babasi mbalimbali NIMESHUHUDIA.
 
Watoa huduma vihiyo wako wengi wamezagaa kila mahali. Jibu sahihi ni CHEAP LABOR. Huwezi ukamwajiri msomi ukamlipa mshahara wa kuku. Nenda kwenye mahoteli, bar, na watoa huduma mbali mbali, wengi wao wanalipwa mshahara mdogo mno hivyo vichwa vyao kila siku vimejaa mawenge. Dereva mmoja anatoka na bus mwanza mpaka Dar peke yake, njiani ananuniana na abiria wakitaka kuchimba dawa. Safari bado ndefu.
 
Ukitaka kwenda Moshi/Arusha, maliza mchezo mzima na KILIMANJARO tu!!!!! Hayo ndiyo mabasi ya uhakika kwa sasa kwa njia ya kwenda Moshi.
 
Mkuu kitala naamini kama kweli wewe ni mhusika huyu mdada mliyempatia ajira kimakosa ataondolewa mara moja.Hizi ajira za mtoto wa mjomba,mtoto wa Mama mkubwa na ajira za ngono ndiyo zitaizika hiyo kampuni yenu.

nikuombe samahani san wahusika tupo humu humu jf. Nimelisikia hilo nitalifanyia kazi huwa kuna no zetu kwenye tiketi unaeza kupiga ukaomba kuongea nasi ofisi kuu kabla hujashuka kwenye gari. Nimepeta no ya gari nitafanyia kazi. Ila tusamehe sana ndugu yangu. Ngorika leading other follow. Tupo barabarani kuanzia mwaka 1963 hatutaki tupoteze wateja leo kwa ajili ya mtu mmoja. Usiache kupakia ngoria pakia yeyote.
 
Last edited by a moderator:
RATCO nzuri inajitahidi ila hata nusu hawaifikii Ndenjela wahudumu hawako ki professional kama Ndenjela, alafu ninadhani ata form four sidhani kama wamefika kuwawezesha kujua Kingereza na alafu sia active ladies kama wa Ndenjela. Lakini kwa Tanga RATCO ni mkombozi na ni bora kuliko basi lolote la Tanga ukitilia maanani Tanga kuna mabasi kama Air bus ya hovyo huwezi amini kwanini serikali inayaacha yanaoperate, maana kiukweli ukipanda Air bus na kufika salama kwa wakati basi nenda nyumba ya ibada ukashukuru Mungu
Wiki iliyopita, ilikuwa jumanne, nilipanda gari la RATCO kutoka Dar hadi Muheza. Nilihudumiwa vizuri. Jioni ya siku hiyo hiyo, saa 10:30 jioni nikapanda tena RATCO kurejea Dar. Nikiri kuwa hili gari la jioni nilihudumiwa vizuri zaidi. Kiyoyozi safari nzima. Kilichonivutia zaidi ni moyo wa uungwana aliouonyesha mhudumu (kondakta?) wa basi hilo. Ni mweupe, mwembamba. Nilimuomba tukifika Mkata nipate 'mchuzi' wa mbuzi. Yule dada hakufanya hiana. Akanitaka tukishakaribia, nimkumbushe. Kweli, tulipokaribia nilimkumbusha. Wakati huo nilishamweleza jamaa yangu muuza 'mchuzi' awe tayari. Kilichofanywa ni dereva kushika breki na mimi nikakabidhiwa 'mchuzi' wangu kwa raha mustarehe kabisa. Kwa ukarimu huo, sidhani kama kampuni nyingine zaidi ya RATCO zitakuwa na fursa ya kunitambua kama abiria wao.
 
huyu ni dereva wa NDEJELA jamani hii gari ni nzuri kupanda usipime utafikiri uko sijui kwenye ndege ama kwenye hoteli fulan nzuri kwa huduma zao

Binafsi nasafiri sana lakini sijapata kupanda hilo basi la Ndenjela. Kwa sifa mlizozimwagia Inshallah nikija bara ntalitafuta maana nina safari ya kwenda Mbeya miezi miwili ijayo.
 
Back
Top Bottom