Kingunge: Wagombea urais CCM hakuna msafi

Kingunge: Wagombea urais CCM hakuna msafi

Comi

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2011
Posts
3,328
Reaction score
958
Kati ya watu wanaoheshimika ndani ya CCM ni Kingunge Ngombare Mwiru. Leo katika mahojiano na mwandishi wa habari ITV amezungumza jambo ambalo wananchi hawana budi kuyazingatia.

Tuchague viongozi bora na si bora kiongozi. Pia kwa kauli ya kwamba hao wanaojitembeza sasa hivi siyo wasafi,Sasa je CCM imejiandaa vipi kupata mtu msafi?

Je, nani aliyemsafi ndani ya CCM?
 
Mwanasiasa mkongwe wa chama cha mapinduzi na kada mshauri wa chama Kigunge Ngombare Mwilu asema wagombea urais CCM hakuna aliye msafi mwenye kumnyoshea kidole mwingine kwamba ni mchafu.

Ameenda mbali zaidi na kusema wagombea wote watatumia fedha na wote wanahitaji fedha hivyo haina haja ya kuonyoshea vidole wengine hivyo wananchi wanachotakiwa ni kupima utandaji wao.

Chanzo: itv
 
wasafi bado wapo wengi tu, hata Mungu (kwa mujibu wa maandiko) alipotaka kuiangamiza Sodoma, Nabii Lutu alikuwapo kama mwaminifu pekee na alibaki na kuendeleza kizazi.
 
huo ndo ukweli wa mambo hakuna wa kimnyoshea kidole mwenzake ndani ya ccm. watangaza nia wote wameandaa milima ya pesa kwaajili ya uchagiuzi na wote wana wapambe na mitandao nchi nzima kuhakikisha wanashinda. kilichopo wanazidiana pesa ndo maana wanaki na Lowasa kila kukicha. nina imani na halmashauri kuu ya ccm kwamba watatenda haki na wtatuletea mtu makini bila kujali majungu ya kimtandao.
 
Ndani ya ccm hao wanaojitangaza kuutaka urais si wasafi kamwe. Ingawa wasafi hawana mtandao ndani ya chama. Pia hawana fedha kamwe.
 
kama wote wachaf bas apewe yeye hyo nafas agombee urais wa JMT.
 
Huyu mzee na mwenzake Kawawa walitubambikiza likwete. Kwa kujidai wanahekima n akutumia uzee wao, kule Dodoma wakazuia report ya maadili ya kikwete isisomwe. Tena kwa maneno haya haya anayoyatumia leo, kwamba 'hakuna sababu ya kusoma report hii,kwani nani kati yetu hapa hana makosa??..".

Kama kuishi kwa mzee huyu ni kwa maangamizi ya taifa,.. asije akashangaa.
 
Ndani ya ccm hao wanaojitangaza kuutaka urais si wasafi kamwe. Ingawa wasafi hawana mtandao ndani ya chama. Pia hawana fedha kamwe.

ni kweli ndugu. ila utashangaa baadhi ya watu watakuja na kumponda kingunge ilhali ni ukweli usio na shaka.


ila kwa mtazamo wangu mimi msafi atakuwa yuko chini sana na siyo rahisi kuteuliwa kutokana na mtandao ndani ya chama
 
Alimaanisha Hakuna aliyekamilika mbele ya Mungu, kila mtu ana mapungufu yake ktk Dunia hii, hata kama sisi binaanadamu hatuujui chafu wako ila mungu anajua zaidi. Malaika pekee ndio hawakosei lkn sio ninaadamu. Kwa hiyo wanao uwania URAISI sio malaika ni binaadamu.
 
Wewe huwaoni?

Kinachoongelewa hapa ni uchafu wa ccm nzima. UKaWA umewaingizaje?

Kwa akili yako unadhani kwa kuwa ccm wote wanatoa funza unadhani na UKAWA pia?

Pole yako, limekukuta!.


Haya tueleze nani msafi kwa upande wa UKAWA???
 
Huyo ndio mtata qlianza hivyo na katiba mpyanikaharibika alisema kuna muungano pasipo washiriki ikqwa nongwa
 
Alimaanisha Hakuna aliyekamilika mbele ya Mungu, kila mtu ana mapungufu yake ktk Dunia hii, hata kama sisi binaanadamu hatuujui chafu wako ila mungu anajua zaidi. Malaika pekee ndio hawakosei lkn sio ninaadamu. Kwa hiyo wanao uwania URAISI sio malaika ni binaadamu.

ni katika maana hii wasaka urais na makundi yao waache kuchafuana. mamlaka za kuteua ndo watakao chambua na kuona nani anafaa na nani hafai
 
Kwa hiyo unamaanisha hata kama mijitu imeonekana bayana ni michafu tena mijizi, mizembe na isiyokuwa na uwezo, ichaguliwe tu?

Nini lengo la kuwa na sifa za viongozi?


Acheni fikra kwamba kukwama kwa ccm ndiyo mwihso wa nchi.

Ni kweli kila mtu anajua ccm inakufa na kuzikwa lakini Tanzania inakwenda kustawi sana chini ya serkali nyingine.

Sikuwazaga kwamba ccm itakuja kufia madarakani.

Alimaanisha Hakuna aliyekamilika mbele ya Mungu, kila mtu ana mapungufu yake ktk Dunia hii, hata kama sisi binaanadamu hatuujui chafu wako ila mungu anajua zaidi. Malaika pekee ndio hawakosei lkn sio ninaadamu. Kwa hiyo wanao uwania URAISI sio malaika ni binaadamu.
 
Mwanasiasa mkongwe wa chama cha mapinduzi na kada mshauri wa chama kigunge ngombare mwilu asema wagombea urais ccm hakuna aliye msafi mwenye kumnyoshea kidole mwingine kwamba ni mchafu.ameenda mbali zaidi na kusema wagombea wote watatumia fedha na wote wanahitaji fedha hivyo haina haja ya kuonyoshea vidole wengine hivyo wananchi wanachotakiwa ni kupima utandaji wao
chanzo itv
Kama hayo maneno yanatoka kwa magamba wenyewe kuwa katika chama chao hakuna msafi basi anguko la CCM liko dhahiri.
 
Back
Top Bottom