Sikukaririshi, najaribu kukufanya uelewe. Kurudia tafsiri yangu ya awali kutafanya kazi yangu iwe ni kukukaririsha fasili. Uchawi ni uwezo wa kutenda yasiyo ya kawaida, ambayo nasikia hata Yesu alitenda. 'Uchawi' wa uchawi unaamuliwa na malengo yake, maana hapa ni kuwa, mwenye uwezo huo akiutumia kudhuru, ndio mchawi.
Ibada ni mawasiliano kati ya binadamu na Miungu, katika sherehe za Kiafrika huwa kuna sala/maombi. Mathalani sherehe ya kumsimika kijana huwa inaambatana na maombi kwa mizimu, ya kuwa imlinde huyo kijana kama ambavyo imekuwa ikimlinda siku zote za maisha yake. Tayari tuna mawasiliano ya kimungu na roho za Miungu na watangulizi wetu, yatosha kuitwa ibada hiyo, sio?
Utamaduni ni namna ya kuishi ya watu, dini ni kipengele kilicho ndani ya utamaduni. Vingine vikiwa ni desturi (kawaida za kila siku, mavazi, chakula), mila (mambo yasobadilika kama taratibu za ndoa, tunu za jamii) , lugha na teknolojia.