Soma "Things Fall Apart" ya marehemu Chinuo Achebe.
Hazikuwa na hazina jambo lolote la maana. Kuna mambo mabaya na ya kipuuzi mengi ambayo yameambatana na hizo "Dini za Kiafrika", ambayo ukiyajua hutataka kuhusishwa nazo. Karibu zote zina misingi ya kishirikina, utoaji kafara (ikiwa ni pamoja na binadamu) na matambiko ya mizimu.
Hizo ndizo ambazo watu wasiozijua ama wapotoshaji wanapenda sana kuzisifu. Soma kitabu nilichokueleza hapo juu uone jinsi moja ya dini za Kiafrika ilivyotumika kumshughulikia "Ikemefuna". Kwenye makabila menig kuna historia za kidini zilizotumika kuwatupa ama kuwaua watoto mapacha (ndio maana makabila mengi hayana majina ya mapacha - ukiacha Wasukuma na Wanyamwezi), waliozaliwa na ulemavu (miaka kadhaa iliyopita usingeona albino - cheki miongoni mwa wamasai), waliozaliwa wakiwa ama wakubwa sana ama wadogo, walioota meno ya juu kabla ya chini, kutelekeza waliozaa kabla ya ndoa na mambo yanayofanana na hayo.
Kwa ujumla, ukilinganisha na dini zenye asili ya mashariki ya kati, "Dini za Kiafrika" zilikuwa na ukatili mkubwa na kuleta mdhara makubwa hasa kwa wanyonge miongoni mwa jamii.