King'amuzi cha Continental matatizoni

King'amuzi cha Continental matatizoni

mkalimani4

Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
26
Reaction score
29
Nina miaka miwili nimekuwa nikitumia King'amuzi cha Continental ambacho mmiliki wake ni mkazi wa Jiji la Mwanza.

Nilikipenda king'amuzi hicho kwa kipindi hicho kutokana na kuvutiwa na matangazo yao kuwa hakina malipo ya kila mwezi.

Baada ya muda mfupi King'amuzi hicho kikabadilika na kuwa cha kulipia Tshs. 12,000/= kwa mwezi wakati hakina hata channel moja inayoonyesha mpira mubashara.

Niliendelea kufuata matakwa yao ya kulipia kila mwezi na nikishindwa kulipia ghafla wanakata channel zote isipokuwa Star tv tu.

Majuzi nimegundua kuwa ni haki yangu kuangalia channel hata kama nisipolipia kama vile; TBC1, ITV, CHANNEL TEN, CLOUDS TV . Haki hiyo nimeigundua baada ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania "TCRA" kutupasha habari njema.

Mpaka leo hii tarehe 12/12/2017 King'amuzi hicho hakijatii Agizo la TCRA wala kutupasha habari kuwa ni lini watatekeleza Agizo hilo halali.

Kutokana na kunyimwa haki yangu ya Msingi ya kupata Habari, nipo kwenye mchakato wa kutafuta Mwanasheria ili niweze kuwafungulia kesi ya Madai ya Tshs. 50,000,000/= kwa kuninyima haki zangu za Msingi.

Vielelezo nitakavyotumia ili kuthibitisha Madai yangu:-
1. Risiti ya kuuziwa King'amuzi
2. King'amuzi chao cha Continental.
3. Gazeti lililotoa Tangazo la TCRA
4. TCRA ili wathibitishe kuwa walitoa Agizo hilo.
 
Hata star times wako hivo, ila mi nimetuma ujumbe tcra bado hawajanijibu chochote nahisi nao niwahuni tu
 
Utapoteza muda wako bure mkuu, hiki king'amuzi ni cha mwenyekiti wa CCM Mwz hivyo hawezi kufanywa chochote, rejea mkulu aliahikid milioni 50 kila kijiji mpaka leo kimya. Usiwaamini viongozi wa CCM hata siku moja.
 
Hata star times wako hivo, ila mi nimetuma ujumbe tcra bado hawajanijibu chochote nahisi nao niwahuni tu
Watakuwa wamepewa maagizo na wao kwenye satellite wanajua sana kama king'amuzi fulani kina wafanya nini na wakati gani, ni wahuni kama walivyo ccm.
 
Sisi wa digitek tangu ninunue ni mwaka wa tano kama sikosei lakini sijawahi kulipia na hakuna malipo
 
Ukweli ni kuwa channel wanaonyesha bure

Leo asubuhi nilikuwa naangalia lakini kwa Sasa no signal
Wameanza juzi kuobyesha bure star TV itv Eatv TBC channel ten uhai star TV plus morning star hizo zote zinaonekana bure
 
Ukweli ni kuwa channel wanaonyesha bure

Leo asubuhi nilikuwa naangalia lakini kwa Sasa no signal
Wameanza juzi kuobyesha bure star TV itv Eatv TBC channel ten uhai star TV plus morning star hizo zote zinaonekana bure
Ting ndio wametii Agizo la TCRA, hao Continental bado wajuaji na mbaya zaidi kwa sasa channel zao hazina signal.
 
Hatimaye wamesalimu Amri ya TCRA. Nimeahirisha kuwafungulia mashitaka.
 
Back
Top Bottom