King Mswati na Utamaduni wa Kizulu

King Mswati na Utamaduni wa Kizulu

KWEZISHO

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2016
Posts
7,519
Reaction score
6,524
Utamaduni ni kitu cha ajabu sana. Hivi ushawahi kuangalia jinsi King Mswati anavyotafuta jiko. Ni utamaduni wa aina yake. Utamaduni wao wa kila mwaka umekuwa ukivutia watu kutoka mataifa mbalimbali. Kinachovutia ni dansi na muziki wao. Dah, ni starehe ya aina yake, ila kwa wengine inahitaji roho ngumu kama sio ya paka.
Nimekuwa nikisikiliza na kuangalia muziki ya watu wa mataifa mbalimbali. Ila nastaajabu na hawa ndugu zetu Wazulu (Wangoni hawamo) utamaduni wao unanishangaza sana wanacheza huku matiti yakiwa vululuvululu. Mbele ya Mfalme, hivi hawaoni soni!!?? Hebu nawe waone walivyo, kwa huku kwetu ingekuwa balaa kubwa.


 
Tusibeze hizi ndizo tamaduni zetu.....ila hazina hustarabh kabisa
 
Tusibeze hizi ndizo tamaduni zetu.....ila hazina hustarabh kabisa
Inataka moyo, kwa huku TZ, sipati picha jinsi itakavyokuwa iwapo tungeukuta utamaduni kama huu.
 
Ustaarabu ni nini mkuu? Na kwa kigezo cha nani?
Ustaarabu wa jamii ni mjadala mpana sana. Ustaarabu wa jamii moja unahusisha desturi zenye kuakisi maadili yenye uungwana pasipo kupendelea au kukiuka haki, sheria, kanuni na taratibu za jamii husika.
Kimsingi hakuna kigezo cha kimataifa au kitaifa kinacho shadidisha kwamba jamii moja imestaarabika kuliko nyingine. Jambo kuu linaloshadidisha ustaarabu ni jinsi jamii inavyozingatia maadili yanachukuliwa kama uungwana na ustaarabu wa kufuata mambo mema yaliyokubalika katika jamii na wakati mwingine huchukuliwa kama elimu ya kufahamu mema na mabaya.
Na hapa tuwe waangalifu sana mema ya jamii moja yanaweza kuakisi mabaya ya jamii nyingine. Au mabaya ya jamii moja yaweza kuwa mazuri ya jamii nyingine.
 
Ustaarabu wa jamii ni mjadala mpana sana. Ustaarabu wa jamii moja unahusisha desturi zenye kuakisi maadili yenye uungwana pasipo kupendelea au kukiuka haki, sheria, kanuni na taratibu za jamii husika.
Kimsingi hakuna kigezo cha kimataifa au kitaifa kinacho shadidisha kwamba jamii moja imestaarabika kuliko nyingine. Jambo kuu linaloshadidisha ustaarabu ni jinsi jamii inavyozingatia maadili yanachukuliwa kama uungwana na ustaarabu wa kufuata mambo mema yaliyokubalika katika jamii na wakati mwingine huchukuliwa kama elimu ya kufahamu mema na mabaya.
Na hapa tuwe waangalifu sana mema ya jamii moja yanaweza kuakisi mabaya ya jamii nyingine. Au mabaya ya jamii moja yaweza kuwa mazuri ya jamii nyingine.
Asante mkuu. Maelezo ya ki Great thinker kabisa. Japo ni hivi bado kuna ule ukoloni wa kitamaduni ambapo, kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kihistoria na kiuchumi, utamaduni mmoja huchukuliwa kuwa ni bora kuliko mwingine. Ndiyo maana leo hii karibu kila kitu cha mzungu kinaigwa karibu na kila mtu duniani kwa sababu huchukuliwa eti ndiyo ustaarabu unaokubalika. Ziangalie dhana za urembo wa mwanamke, demokrasia na sasa tunatamadunishwa kukubali ushoga na usagaji kwa sababu ndiyo ustaarabu kisa tu mzungu mwenye ustaarabu wa juu karidhia.

Mabinti hawa kwa Mswati kwa wazungu wanaakisi ustaarabu wa kinyama kwa sababu kwa mzungu matiti ya mwanamke ni matakatifu mno. Wangekuwa wanaachia matako na kuziba matiti bila shaka kungekuwa hakuna makelele ya kulalamika na kuita ustaarabu wa kijinga na udhalilishaji wa mwanamke. Kwa nini mabinti wakondefu waliovalia vibikini na kulazimishwa kupita mbele ya umati wa watu huku wameanika vitako vyao vilivyosinyaa katika mashindano ya urembo wachukuliwe sawa lakini hawa wanaocheza kwa furaha na mimea yao mikononi wakiwa na furaha ya dhati waonekane hawana ustaarabu? Kwa vile wameachia matiti nje?
 
Asante mkuu. Maelezo ya ki Great thinker kabisa. Japo ni hivi bado kuna ule ukoloni wa kitamaduni ambapo, kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kihistoria na kiuchumi, utamaduni mmoja huchukuliwa kuwa ni bora kuliko mwingine. Ndiyo maana leo hii karibu kila kitu cha mzungu kinaigwa karibu na kila mtu duniani kwa sababu huchukuliwa eti ndiyo ustaarabu unaokubalika. Ziangalie dhana za urembo wa mwanamke, demokrasia na sasa tunatamadunishwa kukubali ushoga na usagaji kwa sababu ndiyo ustaarabu kisa tu mzungu mwenye ustaarabu wa juu karidhia.

Mabinti hawa kwa Mswati kwa wazungu wanaakisi ustaarabu wa kinyama kwa sababu kwa mzungu matiti ya mwanamke ni matakatifu mno. Wangekuwa wanaachia matako na kuziba matiti bila shaka kungekuwa hakuna makelele ya kulalamika na kuita ustaarabu wa kijinga na udhalilishaji wa mwanamke. Kwa nini mabinti wakondefu waliovalia vibikini na kulazimishwa kupita mbele ya umati wa watu huku wameanika vitako vyao vilivyosinyaa katika mashindano ya urembo wachukuliwe sawa lakini hawa wanaocheza kwa furaha na mimea yao mikononi wakiwa na furaha ya dhati waonekane hawana ustaarabu? Kwa vile wameachia matiti nje?

Hapo ndipo utaelewa unafiki wa wazungu. Wamekuwa muda mrefu wakihudhuria Samba Festival kule Brazil na wanaisifia mno. Na sisi tumekuwa wepesi wa kudharau ustaarabu wetu. Tumekuwa watu wa kujidhihaki na kusifia kile kinachopendwa na mzungu. Tunashabikia vibikini!

images


images
 
Hao jamaa usije fikiri kuna siku vita itatokea. Wanaishi maisha fulani ya kuenjoy na kuridhika na kidogo ulicho nacho
 
Back
Top Bottom