SAKATA la gesi sasa limeingia hatua mpya, baada ya watendaji wakuu wa CCM; Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kuitaka Serikali ikae na wana-Mtwara ili kuona namna ya kumaliza mgogoro huo kwa amani.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Ofisi za CCM Wilaya ya Uvinza, Kigoma, Kinana aliitaka Serikali isikilize hoja za wakazi wa Mtwara na kuzitafutia usumbufu sahihi.
Serikali ikae na wana-Mtwara na kuwasikiliza, wananchi hao wana hoja na Serikali inapaswa kutoa majibu sahihi kwa hoja hizo. Lakini pia iwasake na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha uvunjifu wa amani, alisema Kinana.
Kwa upande wake, Nnauye aliitaka Serikali kuwasikiliza wananchi wa Mtwara kwa kuwa madai yao ni ya msingi... Wakazi wa Mtwara na Lindi wanazo hoja za msingi juu ya suala la gesi, hoja ambazo ni muhimu kusikilizwa na kupatiwa majibu sahihi.
Hivi kwenye vikao vyenu CCM huwa mnazungumza nini?kama siyo umbeya kwaninini viongozi wenu wanalalamika kama wapinzani wakati nyie ndiyo wenye serikali?Pooor CCM
chezea nguvu za umma sasa nape na kinana wanashauri serikali ikaongee na wahuni, wahaini, wasio na akili? au wamesahau matamshi ya wajumbe wa ccm hapo awali kwanza wanamtwara sijui kwanini hawakuchoma nyumba ya rc pumbavu kabisa..kazi nzuri sana wana Mtwara masikio yao yatazibuka tu na macho yao watayatoa tongotongo na vinywa vyao watavisuuza ili wajue nini cha kuongea na wenye mali au wanajua mwenye mali ni Kinana na Majangili wenzake wa ccm..
Kinana na Nape wana ingia baraza la mawaziri? Tumia akili bana
Unafiki unafiki unafiki mtupu. Kuna serikali zaidi ya CCM? Kwanini Kinana asimwambie hayo bosi wake badala ya kuwatapeli wananchi? Mbona wananchi walimtaka aache kuua tembo wetu hakuwasikiliza? Hao anaotaka kuwasikiliza wananchi wana nini cha mno tofauti naye wakati wote ni wezi wanaotumia madaraka kujineemesha? Shame on you Kinana!
Kinana na Nape wana ingia baraza la mawaziri? Tumia akili bana
Hivi kwenye vikao vyenu CCM huwa mnazungumza nini?kama siyo umbeya kwaninini viongozi wenu wanalalamika kama wapinzani wakati nyie ndiyo wenye serikali?Pooor CCM
yani hapo nashindwa kuelewa kazi ya chama tawala... wanalalamika kuliko nccr
Kinana na Nape
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Ofisi za CCM Wilaya ya Uvinza, Kigoma, Kinana aliitaka Serikali isikilize hoja za wakazi wa Mtwara na kuzitafutia usumbufu sahihi.
Serikali ikae na wana-Mtwara na kuwasikiliza, wananchi hao wana hoja na Serikali inapaswa kutoa majibu sahihi kwa hoja hizo.
Alipoingia kwenye uongozi, Kinana na Nape walikuwa wanaenda kwa wananchi na kuwasimamisha viongozi ili wajibu hoja. Nawaomba waende Mtwara, wamsimamishe Muhongo ajibu hoja za wananchi...