Maboso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 5,163
- 5,765
Duniani kuna vituko sana. Ni jana tu,Katibu Mkuu wa CCM Kanali Mstaafu Abdurahman Kinana ameivua nguo Serikali ya chama cha Mapinduzi.
Akiwa ziarani mkoani Njombe,Kinana ameitaka Serikali izungungumze na wananchi wake kabla ya kuanzishwa kwa miradi ya maendeleo.Amedai kuwa Serikali ( tena ya CCM) haina utaratibu wa kuzungumza na wananchi wake na kusababisha kutokea kama yale ya Mtwara.
Waungwana,haya kweli ni maneno ya Kinana kuzungumza mbele ya wananchi? Alilenga kuwalaghai au kuidhalilisha Serikali? Nani atamwamini Kinana,mtu mwenye nafasi mujarabu wa kushauri vikaoni mambo kama haya kwa kuimarisha chama na Serikali ya chama chake?
The next Hollace Kolimba in speech?
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Hajaivua nguo bali kaongea ukweli. Kama serikali na chama chake vinakosea kwa nini asiseme? CCM si kama Chadema ambacho ukikosoa unavuliwa uanachama.