Kinadada acheni tabia ya kuzalishwa zalishwa Ovyo bila Ndoa mnawanyima haki za msingi watoto wenu

Mango juice

JF-Expert Member
Feb 25, 2019
345
465
Kwa kweli Dada zetu sijui Mnakwama wapi? kwamba hamna elimu ya uzazi, au mnakubali kudanganywa na kubebeshwa mimba ambazo mwisho wa siku mmakuja kutelekezwa na kusabisha watoto kukosa haki zao za msingi.

Sio ajabu leo kumkuta mtaani mdada ana watoto 3 alafu kila mtoto ana baba yake sasa mtu kama huyu kweli alijipanga kubeba mimba zote hizo au kazibeba kwa bahati mbaya? Je kwa Mwanamke kama huyu Kuna haja ya kuwalaumu Wanaume kuwa wanawakimbia na kuwatelekeza watoto wao.

Hapa mtaani Kuna kesi ya Vijana watatu walio zaliwa na Mama mmoja kila mtu ana baba yake sasa Mama yao huyo akaenda kuolewa na mwanaumee mwingine aliyekuwa anaishi nyumbani kwake na watoto zake 2 baada ya mkewe wa kwanza kufariki sasa Mama huyu kwa sababu alizalishwa watoto 3 akaenda kuishi nao kwa Mme wake wa Ndoa.

Kilichotokea sasa huyu Mama alifanikiwa kuzaa watoto 2 na Mme wake huyu watoto wake hao 2 wakajengewa nyumba yao

Kimbembe kimekuja kutokea baada ya huyu mwanamke pamoja na mumewe kufariki hawa watoto 3 wa huyu Mama ambao aliwazaa kabla ya kuolewa na kila mtoto ana baba yake wanadai Urithi wa Nyumba kwa Baba yao wa Kufikia Wakati mzee huyo alijenga nyumba 2 Moja kwa ajili ya watoto wake wa kwanza kwa mkewe wa kwanza aliyefariki na Nyumba ya pili kwa ajili ya watoto zake wawili aliyezaa na mkewe huyu wa pili

Sasa katika mtafaruku huu nani alaumiwe, na Je hao watoto 3 wa huyu Mama aliowapata kabla ya kuolewa wanahaki ya kumrithi Baba yao wa kufikia?
 
Mkuu nimekuelewa vizuri tatizo linakuja mimba hizi ńyingi zinakuwa ni Mimba zisizo tarajiwa sasa inakuwaje bint anabeba mimba bila ya kupanga kwanza na mwanaume?

Mwanaume hajajipanga kimaisha bado kweli atakubali kulea mimba za akina dada zetu wa leo?
Pia Mkuu ungewaambia wakina kaka wanaowapatia mimba hao wakina dada kuchukua majukumu yao na si kuyakimbia

Ukikubali wajibu timiza wajibu, usiwalaumu wao peke yao ikiwa hawapata hizo mimba kwa njia ya roho

Fikiri kabla ya kurusha lawama popote ni hayo tu Mkuu
 
Mkuu ugomvi umetokea kwa jiran mmeitwa kwenye ugomvi kuepusha madhara kweli utajitenga?
Jamii za kiafrika uwezekanaji wa jambo ili ni Mgumu sana labda uwe unaishi ushuani, wabongo wafukunyuku sana

Japo ni vizuri mtu kufuata biashara zake mwenyewe
 
Mkuu nimekuelewa vizuri tatizo linakuja mimba hizi ńyingi zinakuwa ni Mimba zisizo tarajiwa sasa inakuwaje bint anabeba mimba bila ya kupanga kwanza na mwanaume?

Mwanaume hajajipanga kimaisha bado kweli atakubali kulea mimba za akina dada zetu wa leo?

Wakaze wasifanye Mkuu, si kila ambalo akili zetu na mioyo yetu inatamani basi twaweza kulipata

Una jikaza Tu
 
Kwa Tz ya sasa hii inshu ni Unavoidable.

Maana kila siku wanazalishwa kwao na ni bonge la chanzo kikubwa katika migogoro katika mahusiano mengi hasa kwenye mahusiano ya pili baada ya kuzalishwa.

Only Almighty God knows about this problem.
 
Kwaiyo tatizo hili halina Solution au?
Kwa Tz ya sasa hii inshu ni Unavoidable.

Maana kila siku wanazalishwa kwao na ni bonge la chanzo kikubwa katika migogoro katika mahusiano mengi hasa kwenye mahusiano ya pili baada ya kuzalishwa.

Only Almighty God knows about this problem.
 
Back
Top Bottom