Kinachowachelewesha UKAWA hiki hapa

Kinachowachelewesha UKAWA hiki hapa

hawawezi huu upepo ni noma ndo maana wanakimbia hovyo hovyo,watakimbia adi mwisho wa uchanguzi mwaka huu,

Wewe unajilisha upepo wenzenu Rais yupo!wanasafisha njia tu nyie hata jina bado mnakalia kuvutana na kusogeza siku!
 
ukawa watapona kama wataibadilisha saccoss kuwa chama cha siasa,
 
Msimamo wa Tingatinga kwenye mkutano wake wa leo na wakazi wa Dar Mbagala Dsm ni nomaaaa, Hapa lazima UKAWA wazime ghafla bila kupigwa!
 
Wanabodi
Nawauliza ukawa kunani mbona vikao vingi ambavyo hatujui hitima yake.mimi binafsi nimechoka kuona ukawa wanakuwa kama wasaka tonge wapiga ramli wa habari wanatunga habari zisizoleweka kuwahusu.Hii inanikumbusha methali msipiganie fito kujenga nyumba moja...kitabu kikubwa kinasema NITAMPIGA MCHUNGAJI NA KONDOO WATATAWANYIKA..

UKAWA FUNGUKA
 
natamani UKAWA KUNITOA UKIWA ikiwa na ishara ya matumaini.,,hivi mkitengana mtawaambia nn wananchi ??mbakie hukohuko
 
Yaani hii nchi cjui nani kailoga na watu wake
Yaani tumesha sahau
ESCROW
EPA
RICHMOND
KAGODA
BUZWAGI
MEREMETA
TEMBO KUUAWA
TWIGA KUPANDA NDEGE
MISAMAHA YA MADINI
MISWADA YA HOVYO YA GESI NA MAFUTA
KUPANDISHWA HOVYO BEI YA MAFUTA
WATOTO KUKAA CHINI
AKINA MAMA KUZALIA CHINI
MATAJIRI KUTHAMINIWA
UBOVU WA BARABARA
UBOVU WA RELLI
UHABA WA MAJI SAFI NA SALAMA
KUUZWA BENKI YA TAIFA
KUUZWA KWA SHIRIKA LA NDEGE
KUUZWA KWA NYUMBA ZA TAIFA
KIWIRA COAL MINE
UKOSEFU WA DAWA HOSPITALI ZA UMMA
KUSHUKA KWA ELIMU
MIGOMO YA WAALIMU NA MADAKTARI
MIGOMO YA WANAFUNZI
MIGOGORO YA ARDHI KUTOKANA NA SERIKALI
KUWATHAMINI WAWEKEZAJI WA KIGENI
KUHODHI VIWANJA VYA MICHEZO
KUHODHI MAJJENGO YA UMMA
KULINDA WEZI, MAFISADI NA WAHUJUMU UCHUMI
KUUA VIWANDA ALIVYO VIJENGA MWALIMU
NYERERE
KUUA MASHIRIKA YA UMMA
KUONGEZA MATABAKA KWA WANANCHI
KUUA WANAHARAKATI NA WAANDISHI WA HABARI
( MWANGOSI)
KUPITISHA RASIMU ISIO YA MUAFAKA
ILIYO
FEKI
HIvyo basi,
nashangazwa na watu waelewa humu wanaosema
magufuli jembe
Wakati yupo serikalini tangu 1995
Ndani ya ccm
Nani ametuloga ??
Hapa magufuli ni pombe ile ile kwenye chupa
mpya.
Maskini Tz
Au elimu ya uraia tatizo ???
haya ndo matunda ya kuwa mtanzania na nchi imetulia shuguli zinaenda kama kawa na mijizi inatembea mtaan ikitamba bila ya kuwa na wasiwasi bt cha kushangaza mbona hatupo kwenye top ten ya nchi zenye amani?
 
Mnapiga dana dana tu! kikao cha uraisi majimbo yanahusika vipi mlisema J4 mnatangaza, hizi ni figisu tu mnasubiria mgombea option A kutoka CCM akubali maombi yenu.
 
Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA vimetangaza rasmi kufikia makubaliano ya kusimamisha mgombea mmoja wa urais katika uchaguzi mkuu ujao.

Akitangaza makubaliano hayo mara baada ya kumalizika kwa kikao kirefu kilichokuwa kikijadili mustakabali wa kumpata mgombea urais pamoja na ugawanaji wa majimbo mapya, mwenyekiti mweza wa UKAWA James Mbatia amesema kuwa umoja huo umemteua mgombea ambaye ni chaguo la watanzania.

“Mgombea tutakayemtaja ndiye chaguo la watanzania” Amesema Mbatia. Mbatia amegoma kutaja jina la mgombea aliyepitishwa na umoja huo na kusema kuwa atatangazwa siku chache zijazo kwa madai kuwa anaandaliwa utambulisho maalum utakaoambatana na shamra shamra.

“Tayari jina tunalo lakini tutaliweka hadharani baada ya siku mbili tatu hivi, na tutamtoa kwa kimasomaso”
Katika kikao hicho kilichomalizika majira ya saa 3:30 usiku kikihusisha wenyeviti wa vyama hivyo pamoja na kamati ya ufundi ya UKAWA, mwenyekiti mwenza wa UKAWA kutoka chama cha wananchi CUF Prof Ibrahim Lipumba hakuweza kuhudhuria.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka CUF, chama hicho kilimuagiza Naibu Katibu Mkuu wa CUF Magdalena Sakaya kuiwakilisha, lakini baadaye Sakaya aliondoka katika kikao hicho bila maelezo yoyote.

Kwa upande wake Magdalena Sakaya alipoulizwa kuhusu kukosekana kwake katika kikao hiho, alisema kuwa ndani vyama bado kuna migogoro kwahiyo ni vema kumaliza kwanza migogoro ya ndani ya vyama na ndipo wajadili hatma ya wagombea wa UKAWA.

Mkurugenzi wa mawasisliano wa chama hicho bwana Abdul Kambaya alipoulizwa kuhusiana na hilo akasema kuwa hakuna mwakilishi yeyote wa CUF aliyekuwepo kikaoni hapo hadi kikao hicho kikimalizika.

Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk Mohammed alipoulizwa kuhusiana na kukosekana kwa Prof Lipumba kikaoni hapo amedai kuwa Prof Lipumba ni mgonjwa, na hali yake ya kiafya haimruhusu kuhudhuria kikao hicho.

“Mwenyekiti wetu ni mgonjwa, alikuwa safarini kutoka Kigoma, amerejea lakini hali yake si nzuri, ameshikwa na Malaria kali sana na miguu pia inamsumbua” Amesema Rajab Mbarouk.

Viongozi waliokuwepo wakati wa mazungumzo na waandishi wa habari ni James Mbatia, Freeman Mbowe, Tundu Lissu, John Mnyika, Emmanuel Makaidi, Dkt Wilbroad Slaa, Mosena Nyambabe, Dkt George Kahangwa (mgombea urais kupitia NCCR) na mtu anayetajwa kuwa mwakilishi kutoka chama cha CUF.

Licha ya kushindwa kutaja jina la mgombea urais kupitia UKAWA, baadhi ya vyanzo vya ndani vinaonesha kuwa mgombea urais aliyepitishwa na UKAWA ni Dkt. Wilbroad Slaa ambaye ni Katibu Mkuu CHADEMA.

Katika hatua nyingine, afisa habari wa CHADEMA Tumaini Makene aliwaambia waandishi wa habari kuwa tayari vyama hivyo vimekamilisha kazi ya kugawana majimbo mapya 26 kazi iliyofanyika leo katika kikao hicho.

Kuhusiana na mgombea wa CCM Dkt John Magufuli, viongozi hao wamesema kuwa hawatishiki naye, na wala hawamfikirii, na kusisitiza kuwa mgombea ambaye ni chaguo la watanzania atatoka UKAWA na atatangazwa siku chache zijazo.

Source: EATV Facebook page
 
nimeipenda sana hii mind game kwenye soka.... naifananisha mbinu hii kama ile ya Jose Mourinho
watanzania mtapata mgombea mnayemtaka si michezo yao ya kubadili HOUSING ilhali simu ni ileile
 
Ukitaka kujua chadema ni chama cha mfano na cha kuigwa suburi uone siku wanamtangaza mgombea wao utajionea mwenyewe,itakuwa ni historia na haijawai kutokea nchini tanzania
 
Ukawa Hawana jipya,huyo padri slaa mwizi wa wake za watu kashazeeka ataweza kupambana na kijana magufuli

Najua miaka mi5 ijayo utakuja upinzani tu. Hata cc wengine tulikuwa kama wewe. Labda kama wewe sio rational man
 
KINACHOWACHELEWESHA Muunganiko wa Vyama vikuu vya Upinzani vinavyounda ukawa, kutaja Mgombea wa Urais imebainika,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo. Akizungumza na Mtandao huu, Afisa Habari wa Chadema Tumain Makene amesema sababu hiyo taarifa Majimbo mapya yaliotangazwa jana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini NEC. “Watanzania wasiwe na wasi kinachowachelesha ni Viongozi wa Ukawa ni mgawanyo wa Majimbo mapya ya uchaguzi yalioatangazwa jana na tume ya uchaguzi ndio hayo yanayojadiliwa na kuchelewesha kumalizika kwa kikao” Makene ameongeza kuwa , "kwa sasa Viongozi wa Ukawa wameingia kwenye mapumziko ikiwemo kupata Futali,ila baada ya Hapo Kikao hicho kitaendelea". Vilelevile Afisa Habari huyo amewataka wana chama wa Vyama vinavyounda Ukawa Ikiwemo Chadema,CUF,Nccr Mgaeuzi pamoja na NLD wazipuuze taarifa zinaonea mitandaooni kwamba umoja huo umemeguka na kusema kwa sasa kikao hicho kinaendlea vizuri. Mwandishi wa Mtandao huu aliokuwepo kwenye Hoteli moja hapa Jijini Dar es Salaam ambapo Vikao hivyo vya Ukawa vinafanyika alishuhudia Viongozi mbali mbali wa vyama vya Vitatu ambavyo ni NLD,Chadema pamoja na Nccr-Mageuzi, CUF wakipata Chai ya jioni huku wakioneka wapo pamoja. ENDELEA KUFUATILIA UTAPATA TAARIFA KAMILI MAANA TIMU NZIMA YA WAANDISHI WAKE WAPO KWENYE MKUTANO HUO UTAPATA TAARIFA KAMILI,WWW.FULLHABARI.BLOG.COM

ImageUploadedByJamiiForums1436908292.845504.jpg

CCM B sijui MALIBERALI sijui MAGASHO au jina jipya Bar yetu ya Vichaa tulilolianzisha la WASALITI yatamuhusu Lipumba na CUF
 
Ukawa Hawana jipya,huyo padri slaa mwizi wa wake za watu kashazeeka ataweza kupambana na kijana magufuli

nimeipenda sana hii mind game watanzania UKAWA wana mgombea mnayemtaka me kwenye soka.... naifananisha mbinu hii kama ile ya Jose Mourinho
watanzania mtapata mtu kutoka umoja safi
 
nimeipenda sana hii mind game,kwenye soka
naifananisha mbinu hii kama ile ya Jose Mourinho
watanzania mtapata mgombea mnayemtaka si
michezo yao ya kubadili HOUSING ilhali simu ni
ileile
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom