Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Shibuda alitangaza kugombea urais katika kipindi cha kwanza cha miaka mtano ya utawala wa Kikwete. Alipoona hana nafasi ya kutia mguu aliendelea na mipasho pale bungeni kwa chama chake CCM kama anavyofanya sasa kwa Chadema. Katika kikao cha mwisho cha bunge kabla ya uchaguzi mwaka jana Shibuda alipokuwa amegeuza kauli na kuanza kumpongeza Kikwete, Speaker Samweli Sitta na viongozi waandamizi wa serikali kwa ajili ya kujisafisha atakaporudi kugombea ubunge awe amesafishika dhidi ya mabezo yake kwa viongozi na chama chake cha CCM hapo awali, Speaker Samweli Sitta alimwuliza Shibuda kama angali bado na nia ya kugombea urais pale pale ndani ya kikao cha bunge. Shibuda kama kawaida yake alitoa jibu la kishairi kama si kingonjera kwa kusema; "unapoutua mzigo toka kichwani hufikia mabegani kwanza" mwisho wa kumnukuru.
Kwa matarajio yake kujiunga Chadema na kujiona kama msemaji sana na mzoefu bungeni alitazamia angepata wadhifa mkubwa ndani ya Chama na hivyo kujenga ndoto zake za Urais. Kutokana na kutoweka kwa ndoto hizo ndio maana tunachoshuhudia sasa ni kwenda kinyume cha sera za chama chake, kuwabeza na kuwatukana wakubwa wake wa Chadema ngazi ya kitaifa. Kama mtakumbuka katika baadhi ya vikao vya bunge amewahi kuwarudi wabunge wa upinzani kwamba hawana uzoefu na wawaheshimu wazee.