Kinachomsumbua Lowassa ni hiki

Kinachomsumbua Lowassa ni hiki

CosaNostra

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
382
Reaction score
139
Wadau, nimejiuliza mara nyingi kuwa kama ni kweli EL ana utoshelevu wa mali kama anavyotajwa na kama alikwisha kuwa PM, Ni nini kinachomfanya afanye yote tunayoshuhudia ili tu kuwa na tiketi ya CCM kuwania urais.

Nimefuatilia mahitaji ya binadamu kimaslahi kama yalivyochambuliwaga na wanataaluma nguli. Mmoja wa watu hao ni Maslow katika Theory ya Hierarchy of human needs. Zipo hatua tano 1. Basic needs 2. Security 3. Love 4. Esteem na mwisho pale ni hitaji lijulikanalo kama Self Actualization " what man can be, he must be"

Hili hitaji la 5 ndilo linalomtesa EL, tayari yote mengine kayamudu. Kitu kigumu kuelewa ni kuwa hitaji hili kamwe hiliwi fulfilled, ukipata mali utahitaji zaidi na zaidi, jina kuuubwa, ukipata vyeo hadi juu utahitaji zaidi na zaidi, ukipata urais wa TZ, utahitaji kupata wa EA, kujulikana Ulaya, kutukuzika zaidi, kuwa na majumba hata mitaa Ulaya, kumiliki vitu vikubwa mf. timu za mpira, vitega uchumi vya majina makubwa, n.k.

Kifupi ni vita isiyo mwisho.

Ushauri: EL amechoka mwili na akili, tumshauri tu apumzike ajilie mali zake kwa raha zake, sivyo amuulize Mobutu hiyo Self Actualization ilipomfikisha.
Naomba kuwasilisha.
 
Mhusika ataupata ujumbe wako halafu atafakari mwenyewe na kujua afanye nini.
 
Ashakwisha kisiasa huyo, hebu akae atulie sasa. hata kama ni tamaa ya urais aisee!!! huyu kazidi
 
CosaNostra

EL ni mtu mzima, anawajibika kwa maamuzi na matendo yake mwenyewe, kama yatamuumiza au kumnufaisha ni yeye mwenyewe wala sio sisi mashabenga wa nje, hiyo self actualisation unayoisema ndio path yake kama mwanasiasa,

hatakiwi kuchoka mpaka aipate the biggest prize in the political game; The Presidency! so it is upon him and him alone to decide what he wants to do with his life and face consequences for his chosen path, NOT we mere bloggers!
 
Last edited by a moderator:
Ashakwisha kisiasa huyo, hebu akae atulie sasa. hata kama ni tamaa ya urais aisee!!! huyu kazidi

Siku moja akihojiwa kwenye TV alikuwa akimshangaa Gadaffi kwa kujilimbikizia mali. Hiyo ulikuwa ni wakati wa vurugu za Libya. Huenda sisi tunamuona vingine tofauti na yeye anavyohifahamu!!
 
CosaNostra

Hivyo vitabu huwa mnavisoma lakini nina mashaka kama hata huwa mnaelewa hasa maudhui yake!
Kwa maana hayo uliyoyataja yako kwa Binadamu wote na kama hivyo ndivyo basi unaweza kusema kwa Msaka yoyote yule wa Uraisi kuanzia Pinda, Kigwangala, Slaa, Zito, mpaka Lipumba hivyo kama ni kweli umekielewa hicho kitabui sielewi ni kwa nini unamwandama Lowasa peke yake!
 
Last edited by a moderator:
EL ni mtu mzima, anawajibika kwa maamuzi na matendo yake mwenyewe, kama yatamuumiza au kumnufaisha ni yeye mwenyewe wala sio sisi mashabenga wa nje, hiyo self actualisation unayoisema ndio path yake kama mwanasiasa, hatakiwi kuchoka mpaka aipate the biggest prize in the political game; The Presidency! so it is upon him and him alone to decide what he wants to do with his life and face consequences for his chosen path, NOT we mere bloggers!

But we are here to be analysts Bro!
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Hivyo vitabu huwa mnavisoma lakini nina mashaka kama hata huwa mnaelewa hasa maudhui yake!
Kwa maana hayo uliyoyataja yako kwa Binadamu wote na kama hivyo ndivyo basi unaweza kusema kwa Msaka yoyote yule wa Uraisi kuanzia Pinda, Kigwangala, Slaa, Zito, mpaka Lipumba hivyo kama ni kweli umekielewa hicho kitabui sielewi ni kwa nini unamwandama Lowasa peke yake!

We are all come from history, Ujasiria mali na uongozi wa walala hoi wapi na wapi?
ukishajijengea himaya pumzika waache walio safi watuongoze
 
Mimi naona ni namba 2, yaani security. Kwa madhambi waliyonayo kwa pamoja na akina Rostam, wanachelea kuandamwa pindi nchi ikitawaliwa na wengine.
 
Back
Top Bottom