Kina dada muwe makini na Foreigners

Pole sana shoga angu weye mm kumhonga mwanaume Nina aleji wallah.
Mshukuru Mungu kama haijakucost bdo
Watu wamebadilika sio wadada sio wakaka.
Jitahid kuwa makini usiamin sana kila kile unachoambiwa

Labda kama huna pesa, wanaume tunajuwana wasanii wanajuwa vizuri lugha wanayoipenda wadada.

wasanii huwa hawapewi tu pesa from no where without a good reason, wao huwa wanaanza kuinvest pesa zao kwanza kwa wadada na muda ukifika ni lazima atakula pesa yako nyingi uku ukitarajia utavuna zaidi akiweka mipango yake sawa.
 

Umenikumbusha mdada fulani ambaye ni mwalimu huku rombo baada ya kuajiliwa alikutana na jamaa ambae kasoma nae UDOM lakn hawakuwa na ukarbu, hvyo baada ya kukuta wakaanzisha uhusiano na bidada akawa anamleta shulen akimtambulisha kuwa ndo husband 2 be, atimae akazama NMB akachukua mil. 6 akamkabidhi msela ili anzishe biashara na ndo ikawa mwisho wa kuonana na bidada akabaki hajielewi mpaka leo
 

Soma hiyo story ya mdada yeye yeye alishindwa kujua utapeli wa jamaa mapema akawa anahonga akitegemea atavuna zaid
Kama ni boy wako na hupend aadhirike ndo ukamkopee hela banki?au Hela yako ambayo ipo kwenye budget ya uzalishaji..au.ukakope kwingine umpe yeye

Kumsaidia kuna mipaka kama lipo ndani ya uwezo wako na haitakuaffect kiuchumi MPE.
Sio umkopee bali msaidie cos ni boy wako don't expect return.hiyo umetoa sadaka kwa umpendae.
Ila suala LA kwenda kutikisa biashara au kuchukua mkopo ndo umpe noo
 


Advertise ya kwanza jamaa alirekebisha gari la huyo dada maana lilikuwa home kwa sababu ya ubovu wa hapa na pale, kilichofuata ilikuwa ni kuchota hela.
ICHANA
 
Last edited by a moderator:

Sikatai hili mna ujanja ila sis ndo tunatengeneza hayo mazingira
tunapokea hela zenu sana , tunapenda kudanganywa na tunaona tunapendwa sana pale kila siku mnavyokuja na new ride to pick us...every day new business plan mnazo
hapo akili zetu xinakuwa dormant kabisaaaaa
Hat ukituambia tukachukue mkopo was 20m nikupe nakimbia kama land rover mpya LA jesh

Kumbe tunajikaanga wenywew na mafuta yet like kambale.
 
mumshauri tu asijewaza kujiua maana hawachelewi
 
hahaha watakoma mwaka huu, pole yake kuna rafiki yangu Alipata mnaigeria yule kaka alijifanya ni mfanya biashara na akawa anatuletea vitenge kutoka kwako tukajua kweli, ila baadae mi nilimstukia kuna sehemu nilimfuma anaongea kiswahili kizuri sana wakati akiwa na rafiki yangu anajifanya kiswahili hakipandi, mambo yakaenda mpaka akazaliwa mtoto akapewa jina la kikwao, mwanamke alikuwa anaamini kama vile anavyowaona wanaigeria kwenye sinema zao akaona na yeye mambo yake yatakuwa safi, ikafikia wakati wa kujitambulisha mwanaume akadai ndugu zake hawawezi kuja watakuja kwenye ndoa, wakwe wakaweka ngumu ikabidi akawatoe huko walipo, kumbe yule bwana alizaliwa Naigeria tu, ila ni mtanzania kakulia huku kasoma huku na kwao ni sinza mapambano na hana kazi wala nini vitenge sijui alikuwa anaiba wapi. wasichana wanabidi wawe makini sana hali ya maisha imekuwa ngumu
 
Mkuu sio Mimi # ichana# I swear never labda unigonge sindano ya usingiz achukue kwenye pochi au niwe unsound mind
Na akili timamu hii hupati mkuu

Hahaaaaaa we ka mie hata jero yangu mwanaume apatii
 
Ha ha ha! Kama urikuwepo (red) mura! Basi na hiri rijamaa unaweza kuwa unarifahamu. Maana rimetuachia majanga.

Ulivyosema alitoka russia nimemhisi mmoja wao alitoka russia akapita hapa kwa lengo la kwenda U.K lakini alishindwa hiyo ilikuwa mwaka jana kama mwezi wa tatu.
Hivyo aliikaa hapa tz almost mwaka mzima...
 

Whether umekopa benki,umechukua uliyohongwa na mwenzie,umechota akiba yako....suala si linabaki palepale UMEMPA?
 

Hahahahah....daaah hii dunia Mungu atunusuru jamani
 
Whether umekopa benki,umechukua uliyohongwa na mwenzie,umechota akiba yako....suala si linabaki palepale UMEMPA?

Omba Mungu yasikukute wewe hujakutana na hawa wacameroon nakwambia..
Anaanza kwa kukupa wewe wanajifanya high class kula hotel kubwa na watu wa international business.
Ata invest muda wake hata miezi mitatu siku atakuja anakwambia kuna container lake limekamatwa anahitaji milion 7 wewe hutahisi kweli na kwa jinsi ulivyoongopewa huwezi hisi kama ni mtu wa kukimbia na milion 7. Ukimpa ndo sahau
 
Basi wameamua hao wacameroon, me nlikutana na mmoja Bank..Wacha aning'ang'anie....na vile mtoto nlikuwa nimetupia ushungi akaja na gia kali sana ya ndoa...
Bahati nzuri sijawahi kuwaza kuolewa na foreigner even mmakonde mwenzangu wa Msumbiji....tutabanana huku huku uzaramoni....

Cha ajabu katika Chating nikamuuliza unaishi wapi? Mara anambie Kinondoni, mara Magomeni, mara Kariakoo...mwishowe akafunguka eti anataka aje aishi kwangu....Mwee hapo me mwenyewe nlikuwa naishi hostel...!

Nikaona hapa ni shida tu, nikampotezea...halafu mtongozo wenyewe ulikuwa kwa kizungu ndo kabisaa nikaona ananichosha kunihangaisha na dictionary...

Wadada tuwe makini sana, jamaa wameamua...!
 
Hahaaaaaa we ka mie hata jero yangu mwanaume apatii

Hongera kwa hili kula maisha
Na tusitoe mianyaa ya kupokea pokea vyao..
Ukimkopea mpenz utakosa Uhuru wa kumdai bhana hat stareh ya kugegedana itapungua kisa hajakulipa hela
 

Aaah.... God forbid....wanatufundisha ukauzu hadi wale wakweli wataonekana ndo walewale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…