Vyombo vya habari zimeshajipambanua kiasi kwamba watu wenye akili wameshaacha kusoma baadhi ya magazeti, kama vile ya Habari Corporation na yale ya serikali (HabariLeo na Daily News). Haya yamepewa maelekezo ya kuandika kila kitu negative kuhusu Dr SLAA na Chadema, lakini wanapaswa kuipamba CCM na vyama vingine pandikizi vya mafisadi. Ni tofauti kabisa ukisoma magazeti mengine kama Tanzania Daima na Mwananchi ambayo huandika bila bias. Ni wazi kabisa Tanzania Daima linalomilikiwa na mwana-Chadema litazipa zaidi kipaumbele habari za Chadema wakati huu wa kampeni, lakini pia huandika ukweli kuhusu CCM na ahadi za mgombea wake. Lakini hayo magazeti ya Habari Corporation na Daily News/HabariLeo yanatumika kumchafua Dr Slaa na Chadema na kupindisha kila wanachosema kionekane kibaya. This is not professionalism! Siamini kama wahariri wake ni mbumbumbu kiasi cha kutoelewa kwamba wanapotoka. No wonder mauzo ya magazeti haya yamepungua sana kiasi cha kampuni kama Habari Corporation kushindwa hata kulipa mishahara ya wafanyakazi kwa miezi mitatu, huku mhariri wake mkuu akila kuku kama kiongozi wa kampeni za chama cha mafisadi kwa upande wa habari. This is incredible! Ndio maana katika nchi fulani fulani vyombo vya habari vya aina hii vilichangia kwa kiasi kikubwa kuleta machafuko kwenye nchi. Maelekezo ya kuwapotosha watanzania, yametolewa na viongozi wa chama cha mafisadi, yametolewa pia kwa TV stations kama TBC na Channel 10. Wote mnajua kinachoendelea huko, ni KICHEFUCHEFU!