Kimara, Dar: Polisi wawakamata kwa uzururaji Daktari chriscyrilo na Daktari Shindo Kilawa

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Watu waliojitambulisha kuwa ni Askari polisi (bila kuonesha vitambulisho) wakiwa na silaha za moto wamewakamata madaktari wawili, Dr. Chriss Cyrilo (kushoto) na Dr. Shindo Kilawa (kulia) wakiwa maeneo ya Mbezi jijini Dar usiku huu.

Watu hao hawakutaja sababu za kuwakamata, zaidi ya kutumia nguvu kuondoka nao kwa gari aina ya Defender. Nimewasiliana na Polisi kituo cha Mbezi lakini wamekanusha kuwashikilia madaktari hao.

Tafadhali sambaza taarifa hii kwa ajili ya usalama wao, na tushirikiane kupaza sauti ili ijulikane walikopelekwa na sababu za kukamatwa kwao. #Justice4CyriloAndKilawa

FB_IMG_1585021556900.jpg

Updates FROM YERRICKO NYERERE

Kelele zetu zimesaidia Makamanda wetu @dr_chriscyrilo na Dr. Shindo Kilawa wameachiwa na polisi Kimara Temboni, ajabu kesi yao wameambiwa ni uzurulaji.

Hawa ni Madaktari Professional walichelewa kurudi kwao wakiwa Muhimbili ambako kamanda mwenzetu Brock Karume amelazwa kwa ajali, walipofika Mbezi wakakamatwa kwamba ni wazurulaji hadi kufikishwa Kimara Temboni, sauti zetu zikafanya waachiwe!
 
Taarifa iliyotia taharuki mapema leo ktk mitandao ya kijamii ambapo kada wa Chadema Godlisten Malisa ametoa taarifa hiyo kwenye mtandao wa Instagram akidai Madakatari wawili waliokamatwa na Watu wanaodaiwa kuwa ni maafisa wa polisi

Haikufahamika haraka watu hao wana nia gani na ukamataji huo.
Screenshot_20200324-064506_Chrome.jpg
 
Hivi huu utaratibu wa kukamatana bila kuambiwa kosa, kupitia serikali ya mtaa, bila ya taarifa ya kuitwa polisi au mahakamani ni utaratibu wa askari wa Tanzania pekee? Sheria inasemaje kwani wakikuhitaji kwenda polisi either kwa mahojiano au vyovyote vile?
 
Wanamakosa gani

Sent using Jamii Forums mobile app
Usiwe mgeni na mambo ya nchi yetu,Siku hizi unatekwa kwanza ndipo makosa yako unayakuta huko huko kusikojulikana.Utaratibu wa kisheria na uchunguzi hauzingatiwi na hakuna ruhusa kuuliza wala kuhoji uhalali wa lolote.

Hali ni tete na hofu imetamalaki,huku COVID 19,wasiojulukana nao wapo kazini na nchi bado inaitwa ya Amani.
 
Back
Top Bottom