Kim Poulsen kocha mpya Simba

Kim Poulsen kocha mpya Simba

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,345
SIMBA imeamua kufanya mabadiliko kwa kumtwaa kocha Kim Polusen raia wa Denmark katika nafasi ya Mzambia, Patrick Phiri.Simba imeingia kwenye harakati za kumng’oa Phiri ambaye ameiongoza Simba katika mechi sita tu za Ligi Kuu Bara na zote ametoka sare. Simba imefunga mabao sita, imefungwa sita na ina pointi sita.


Mdenishi Poulsen ambaye yuko kwao nchini Denmark baada ya kuzinoa timu za taifa za vijana na baadaye Taifa Stars, aliondolewa kwenye kiti chake baada ya kuingia kwa uongozi wa Jamal Malinzi.Habari za uhakika ambazo Championi Jumatano limezipata ni kuwa, Simba wamefanya mazungumzo na Poulsen na kukubaliana kila kitu na yupo tayari kuja nchini wakati wowote.


Lakini kumekuwa na suala la Phiri kidogo limekuwa likiwagawa baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji kutaka apewe mechi ya mwisho ambayo itakuwa ni dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, Jumapili.


“Kweli viongozi wamejadili kila kitu na Poulsen, ni uhakika kama ulivyosema. Wamekubaliana suala la mshahara na kila kitu kipo wazi.“Poulsen amewaeleza mshahara, mwisho wamekubaliana. Halafu likafuatia suala la nyumba, kocha amesema angependa kuishi Masaki, pia wamekubaliana katika hilo.


“Mwisho lilikuwa ni suala la usafiri na tiketi za kwenda na kurudi kwao Denmark, hilo pia wamekubaliana. Hivyo wanachosubiri huenda kikawa ni mechi ya Jumapili na kama si mechi hiyo, basi angekuwa ameishatua,” kilifafanua chanzo.


“Ila hata hivyo inachanganya, kama Simba ikishinda sijajua itakuwaje. Kinachoonekana ni kwamba kocha Phiri si mbaya, ila hana nguvu kwa baadhi ya wachezaji ambao wamepoteza nidhamu.
“Pia amekuwa na tabia ya kutotaka kuwaudhi watu, anataka kila mtu afurahi hata kama anaharibu. Ndiyo maana viongozi wameona vema kumleta Poulsen.”


Iwapo Simba itashikilia msimamo wake wa kumleta Poulsen, basi lazima itaendelea na rekodi yake ya kuwa timu iliyofukuza makocha wengi zaidi kwa misimu mitatu mfululizo.Katika misimu miwili iliyopita, Simba ilifundishwa na makocha wanne tofauti, kila mmoja akifundisha nusu msimu.

GlobalPublishers
 
Dah, hii timu yangu..
Kwahiyo akija Kim, lile tatizo la beki ya kati litaisha? Kim akitua tu, ule usajili bomu wa Kwizera utaonekana ni bora? Kim atakuja na miujiza ya kubadiri tabia za kina Kisiga?
Aveva bhana.. Anyway Kim Poulsen karibu Simba SC "Taifa Kubwa".
 
Dah, hii timu yangu..
Kwahiyo akija Kim, lile tatizo la beki ya kati litaisha? Kim akitua tu, ule usajili bomu wa Kwizera utaonekana ni bora? Kim atakuja na miujiza ya kubadiri tabia za kina Kisiga?
Aveva bhana.. Anyway Kim Poulsen karibu Simba SC "Taifa Kubwa".
Kwa mwenendo huu elfu tano tano zangu uwanja wa Taifa watazisikia tu. Hawa viongozi ni matatizo matupu.
 
Luga alikuwa mkali kwa wachezaji wakamtimua huyu si mkali nae wanamtimua dah wampe Julio Pereira tu.
 
Dah, hii timu yangu..
Kwahiyo akija Kim, lile tatizo la beki ya kati litaisha? Kim akitua tu, ule usajili bomu wa Kwizera utaonekana ni bora? Kim atakuja na miujiza ya kubadiri tabia za kina Kisiga?
Aveva bhana.. Anyway Kim Poulsen karibu Simba SC "Taifa Kubwa".
Hilo ndo soka la bongo ndugu,,,
 
Tanzania yetu ya ajabu sana. Kila kona watu utawasikia wakipiga stori za mpira tuu. Dar ndio kabisaaa mpira mpira mpira toka asubuhi hadi nyingine. Mpira ni poa lakini usidumaishe akili zetu kufikiri mambo mengine ya maana. Fikiria hadi watoto wanajaza wachezaji kwenye mitihani. Tubadilike bana
 
Kim Polsen bonge la kocha. Kumbukeni Stars na alitengeneza viyoso kibao. Lakini Phiri naye namkubali, ni kwamba kuna shoti mahali Simba.
 
Wataletaje kocha aliyevunjiwa mkataba na TFF? Au ndio anakuja kutoa ushahidi dhidi ya TFF kuhusiana na fedha alizodaiwa kulipwa? Hii si mikakati ya Ndumbaru dhidi ya Malinzi? Mungu wangu!
 
Kim Polsen bonge la kocha. Kumbukeni Stars na alitengeneza viyoso kibao. Lakini Phiri naye namkubali, ni kwamba kuna shoti mahali Simba.
Ni wale wale tu! bonge la kocha wapo timu za maana, mbona uwezo wake unafanana tu denis kitambi!!!!! labda angekuwa anakuja mourinho ningesema kweli bonge la kocha lakin kama huyu poulsen ni wa kawaida sana hata pale starz hakuna cha maana alichokifanya zaidi ya kutafuna mamilion yetu..
 
Kama kweli poulsen anakuja simba itashuka daraja bora wamrudishe loga. Phiri ni bonge la kocha hakuna ubishi. Tatizo la simba ni hao viongozi na okwi wao waliyemgeuza mfalme na kuwaacha wachezaji wengine kama yatima. Viongozi watafute suluhu na wachezaji wawafanye wawe na umoja kama zamani. Wakilifanya hili hata leo nina uhakika week end jkt ruvu hatoki hakuna cha ukawa wala nini.
 
Wanajibu mapigo kwa Yanga iliyomleta Maximo. Wakumbuke kuwa siyo kila kitu kinafaa kuigwa. Wahenga walisema: 'Ukiiga kunya kwa tembo utapasuka msamba'.

Simba ng'oeni Aveva na genge lake fasta!
 
Wanajibu mapigo kwa Yanga iliyomleta Maximo. Wakumbuke kuwa siyo kila kitu kinafaa kuigwa. Wahenga walisema: 'Ukiiga kunya kwa tembo utapasuka msamba'.

Simba ng'oeni Aveva na genge lake fasta!
Kuigana ndiko kunaziponza hizi timu mbili, angali wenzao MCC, msimu wa pili Ligi Kuu tayari wana mikataba mitatu ya kibiashara pamoja na mipango mingine.
Yaani timu iko tayari kutumia mamilioni ili kuwaharibia wenzao usajili huku wakiwa na madeni ya wachezaji wao...
 
Kuigana ndiko kunaziponza hizi timu mbili, angali wenzao MCC, msimu wa pili Ligi Kuu tayari wana mikataba mitatu ya kibiashara pamoja na mipango mingine.
Yaani timu iko tayari kutumia mamilioni ili kuwaharibia wenzao usajili huku wakiwa na madeni ya wachezaji wao...
Na mngesemaje kama licha ya mikataba mitatu minono Yanga na Simba zingekuwa mkiani mwa msimamo wa Ligi kama walivyo hao 'wenzao' hivi sasa? Si ndio nyinyi ambao mngezinanga kwa matumizi mabaya kwa kushindwa angalau usajili wa mchezaji mmoja wa maana? Mpeni Kaizari kilicho cha Kaizari, na mpeni Mungu kilicho cha Mungu!
 
Back
Top Bottom