Echolima
JF-Expert Member
- Oct 28, 2007
- 3,826
- 2,057
Kwa wiki sasa kumekuwa na Mtafaruku katka migodi mingi kama vile GGM, NORTH-MARA, BULYANHULU, TULAWAKA na BUZWAGI hii inatokana na habari kuwa mifuko ya jamii kama vile NSSF, PPF na mingine itaacha kuwalipa wafanyakazi mafao yao pindi watakapofukuzwa au kuacha kazi wenyewe mpaka watakapo fikisha miaka 60.
Kutokana na hali halisi ya kazi zao inakuwa ngumu sana kuweza kuipata hiyo haki yao wakiwa na zaidi miaka 60 maana Mazingira ya kazi yao mara nyingi ni ya hatari sana na yana madhara ya baadaye.
Mbali na hayo waajiri wao mara nyingi sana huwa wakati mwingine wanafukuza wafanyakazi ovyo-ovyo, kama sheria hii itapita basi itasababisha maafa makubwa sana kwa wafanyakazi wengi.
Kwa sababu sasa hivi bado kuna kikao cha WABUNGE wetu tunaomba waweke nyuma malumbano yao waliangalie upya suala hili walinde maslahi ya wafanyakazi kwa ujumla, kwa sasa sheria iliopo mtu akiacha au kufukuzwa kazi alikuwa analipwa mafao yake yote bila matatizo.
Kutokana na hali halisi ya kazi zao inakuwa ngumu sana kuweza kuipata hiyo haki yao wakiwa na zaidi miaka 60 maana Mazingira ya kazi yao mara nyingi ni ya hatari sana na yana madhara ya baadaye.
Mbali na hayo waajiri wao mara nyingi sana huwa wakati mwingine wanafukuza wafanyakazi ovyo-ovyo, kama sheria hii itapita basi itasababisha maafa makubwa sana kwa wafanyakazi wengi.
Kwa sababu sasa hivi bado kuna kikao cha WABUNGE wetu tunaomba waweke nyuma malumbano yao waliangalie upya suala hili walinde maslahi ya wafanyakazi kwa ujumla, kwa sasa sheria iliopo mtu akiacha au kufukuzwa kazi alikuwa analipwa mafao yake yote bila matatizo.