Kuna watu hata humu JF na mtaani wanajifanya wajanja sana na waelewa ila Wazazi wao wanasombwa na Malori waende kwenye mikutano ya CCM

Kuna watu hata humu JF na mtaani wanajifanya wajanja sana na waelewa ila Wazazi wao wanasombwa na Malori waende kwenye mikutano ya CCM

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2020
Posts
5,496
Reaction score
14,113
Wale Wazazi wanao sombwa na malori kule bushi wana watoto wao mijini na wengine hata ni members wa JF. Ila sasa ukiwakuta huko mjini au humu utawaona ni watu waliopiga hatua kubwa ya upeo wa fikra kumbe ni full wajinga tu.

Sasa kupiga hatua ya upeo kuna maana gani kama Wazazi wako wanasombwa kwenye malori kama mbuzi wano pelekwa sokoni na wewe uko town unajifanya mjanja kumbe fala tu?

Huwezi ukawa unapinga watu kusombwa kwenye malori kama kuku ilihali miongoni mwa wanao sombwa wamo kabisa wazazi wako na ndugu zako wengine wa karibu. Huu ni ujinga mkubwa sana na ushamba.

Sasa kama kukemea wazazi wetu au ndugu wa karibu waache ujinga na waache kutumika kwa kubebwa kama kuku, tutaweza je tutaweza kukomboa hili taifa?

Kama ndugu zetu tu kuwakomboa kifikra hatuwezi tutawezana kwa wasio ndugu?
 
No reforms no election , wanao kubali umasikini oktoba wanatiki, Ili waendelee kuwa maskini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom