Kilimo cha vitunguu maji

Mnaweka nini kwenye vitunguu maji..... Vitunguu maji tukiwa tunapika jikoni havina harufu, havitoi machozi..... Havina ladha kabisa Au ni GMO pia??
Mmmh ww unanunua wapi hvo vitunguu mkuu...
 
Kitunguu maji ni zao ambalo watu wengi wanalikimbilia ila si zao rahisi kama wanavyofikifikiria...ni zao gumu na linahitaji usimamizi makini kuanzia vitalu mpaka kuvuna.

Kama huna muda wa kukaa shambani nakushauri usililime hiki zao maana litakufelisha vibaya sana.

Changamoto kubwa za shambani ni hali ya hewa na udongo.

Kitunguu ni zao linaloathiriwa sana na mabadiliko ya hali ya hewa, jua likiwa kali sana ni tatizo na baridi likizidi sana pia ni tatizo....kifupi kitahitaji hali ya hewa ya wastani kuweza kustawi na kukuva mavuno.


Kitunguu kinapenda hali ya ukame hivyo mvua nyingi au maji yanayotuama pia ni tatizo.

Kitunguu kinastawi vizuri ktk udongo ambao una mchanganyiko wa tifutifu na kichanga....Udongo mgumu wa mfinyanzi haufai kwa kitunguu kwani unatuamisha maji kwa muda mrefu na kichanga kabisa pia hakifai kwani hakishiki maji na wakati wa jua kali kinachoma vitunguu na pia upotevu wa virutubisho huwa mkubwa.

Changamoto nyingine ni kuwa kitunguu maji kinapenda maji...yaani unyevu wa kutosha katika ukuaji wake wote hivyo hakikisha eneo unalotaka kulima lina maji ya kutosha.

Changamoto nyingine ni ya magonjwa ya fangasi na wadudu waharibifu.
-Kitunguu kinaathiriwa na magonjwa mengi ya fangasi kama Downy mildew, Purple blotch, stemphillium blight, (soft,pink and neck rot), tip burn,botrytis leaf blight,damping off n.k)..hivyo unatakiwa uwe na elimu ya kutosha kuyajua magonjwa na vipi utakabiliana nayo.

Pia wadudu wasumbufu kama vithiripi (thrips) , Red and black spider mites (utitiri mwekundu na mweusi), leaf hoppers (mbilizi) pamoja na leaf miners... unatakiwa ujue unakabiliana nao vp.

Changamoto nyingine ni mtaji...kitunguu kinataka pesa iwe mfuko wa shati ili ulihudumie shamba kwa wakati, dawa upige kwa wakati, mbolea uweke kwa wakati na maji umwagilie kwa wakati.

Mwisho changamoto nyingine ipo kwenye masoko....bei hubadilika badilika kutegemeana na uzalishaji wa mwaka husika na pia kipindi gani umelima...Kiangazi changamoto za magonjwa ya ukungu hupungua, wadudu huwa wengi ila mavuno nayo huwa ni makubwa tofauti na kipindi cha mvua....Bei za chini hushuka mpk sh 70000 kwa gunia ya kilo 100 na huweza kupanda kufika hadi 400,000.
 
Hivi vitunguu soko lake ni uhakika?
 
Hivi vitunguu soko lake ni uhakika?
soko lake linabadilika badilika....hupanda ghafla na kushuka ghafla kutegemeana na wingi wa bidhaa masokoni. Leo inaweza kuwa laki baada ya wiki mbili bei ikalipuka kufika hata laki 2 kwa gunia..na pia unaweza kuona bei ni laki 2 baada ya wiki mbili ukasikia bei ni elfu themanini...
 
Namaanisha kwamba mtu anaweza kuja kuchukua mzigo wote au ndio mambo ya gunia mojamoja?
 
Mkuu kwemaah naomba mrejesho WA hii project yako,

Mafanikio yakikuwa yapi na changamoto zilikuwa zipi.Mrejesho wako ni Somo Zuri kwa wengine
 
kitunguu maji ni zao lenye wivu kama mwanamke kigoli. Linaathirika kwa vitu vingi sana vikiwemo na ardhi, hali ya hewa, uwepo wa wadudu kama thrips na magonjwa ya fangasi. Kwahiyo shamba lake linataka umakini sana ndani ya siku 60 za kwanza toka kupandikiza. Pia ni zao ambalo linaweza kukupa pesa kama bei zipo vizuri na vilevile linaweza kukutia umasikini kama ukikutana na msimu mbovu , bei mbovu sokoni na hali ya hewa mbovu shambani.. Linataka huduma zaidi ya mke au watoto...Mbolea uweke ya kutosha ,madawa na sumu za wadudu upige kwa wakati na maji umwagilie kwa wakati
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…