Nenda Kijiji cha Kongwa, Kata ya Mvuha, Tarafa ya Mvuha, Morogoro Vijijini kuna mbuga nzuri sana ya mpunga. Pia kuna scheme ya umwagiliaji. Mwaka jana serikali imeingiza billion 4 kwaajili ya ukarabati wa scheme wakandarasi wapo site wanaendelea na ukarabati. Kilimo ni cha uhakika na gharama za uendeshaji ni nafuu sana ukilinganisha na maeneo mengine. Ekari moja unatumia mifuko 2 tu ya mbolea (mmoja wa kupandia na mwingine wa kukuzia). Eneo la scheme ya umwagiliaji ekari moja wanakodi kati ya laki moja hadi laki na nusu pia kuna gharama ya maji elfu kumi na gharama ya uendeshaji na matunzo ya miundombinu elfu hamsini. Ekari moja unavuna kati ya gunia 25 hadi 30.
Eneo la mbugani wanakodi kati ya elfu sitini hadi elfu themanini kwa ekari. Huko hutumii mbolea kabisa na wastani wa mavuno kwa ekari ni gunia kumi na tano hadi ishirini.