Kilimo cha mpunga Morogoro

Kilimo cha mpunga Morogoro

Kwa Morogoro nenda Dutumi kule wanalima sana mpunga
 
Eneo ni laki 4 kwa huku, mpunga unacheza kwa 90,000 huku mawindi kule rujewa naskia ni 105,000 kwa gunia....eneo mimi nipo kata ya mawindi kijiji cha isunura
Na heka moja inatoa wastani wa gunia ngapi?
 
Nenda Kijiji cha Kongwa, Kata ya Mvuha, Tarafa ya Mvuha, Morogoro Vijijini kuna mbuga nzuri sana ya mpunga. Pia kuna scheme ya umwagiliaji. Mwaka jana serikali imeingiza billion 4 kwaajili ya ukarabati wa scheme wakandarasi wapo site wanaendelea na ukarabati. Kilimo ni cha uhakika na gharama za uendeshaji ni nafuu sana ukilinganisha na maeneo mengine. Ekari moja unatumia mifuko 2 tu ya mbolea (mmoja wa kupandia na mwingine wa kukuzia). Eneo la scheme ya umwagiliaji ekari moja wanakodi kati ya laki moja hadi laki na nusu pia kuna gharama ya maji elfu kumi na gharama ya uendeshaji na matunzo ya miundombinu elfu hamsini. Ekari moja unavuna kati ya gunia 25 hadi 30.
Eneo la mbugani wanakodi kati ya elfu sitini hadi elfu themanini kwa ekari. Huko hutumii mbolea kabisa na wastani wa mavuno kwa ekari ni gunia kumi na tano hadi ishirini.
 
Nenda Kijiji cha Kongwa, Kata ya Mvuha, Tarafa ya Mvuha, Morogoro Vijijini kuna mbuga nzuri sana ya mpunga. Pia kuna scheme ya umwagiliaji. Mwaka jana serikali imeingiza billion 4 kwaajili ya ukarabati wa scheme wakandarasi wapo site wanaendelea na ukarabati. Kilimo ni cha uhakika na gharama za uendeshaji ni nafuu sana ukilinganisha na maeneo mengine. Ekari moja unatumia mifuko 2 tu ya mbolea (mmoja wa kupandia na mwingine wa kukuzia). Eneo la scheme ya umwagiliaji ekari moja wanakodi kati ya laki moja hadi laki na nusu pia kuna gharama ya maji elfu kumi na gharama ya uendeshaji na matunzo ya miundombinu elfu hamsini. Ekari moja unavuna kati ya gunia 25 hadi 30.
Eneo la mbugani wanakodi kati ya elfu sitini hadi elfu themanini kwa ekari. Huko hutumii mbolea kabisa na wastani wa mavuno kwa ekari ni gunia kumi na tano hadi ishirini.
Na vipi upatikanaji wa mashamba
 
Na heka moja inatoa wastani wa gunia ngapi?
Kiukweli siwezi kukupa exact figures mana mm nilikua nafanya kilimo cha simu kile....sahivi nmekuja rasmi naingia front mwenyewe ambapo mapato ni wastani wa gunia 30 mbaka 35 kwa hesabu za fasta mkuu...na msimu huu wenyeji wanasema hali ni mbaya mvua haikua ya kutoshaa sana
 
Kama una pesa, nenda kalangue kwa wakulima. Usilime mwenyewe!
Ukilangua, unakuwa na control kubwa! Risks zote hazikuhusu!
Pia kibongobongo kulima hakulipi kibiashara! Daima gharama zitakuwa kubwa kuliko utakachopata!
 
Back
Top Bottom