Kilimo cha miti ya mbao - Kibondo

CHE GUEVARA-II

JF-Expert Member
Jun 17, 2010
571
156
Mkuu, mambo vipi?
Naomba ushauri wako. Kuna eneo naweza kupata Kibondo (Kigoma), nahitaji nipande miti ya mbao.

Nimeambiwa miti hii inastawi Kibondo.
1)Acrocarpus
(2)Casuarina spp
(3)Cedrela odorata
(4)Pinus
(5)Cypres
(6)Acacia mangium

Naomba kujua kwa ujumla ni miti ya aina gani katika hiyo ina-return kubwa (yaani ina faida kubwa na ndani ya muda mfupi)?

Pia nahitaji kujua mchanganuo wa kila aina ya mti hapo juu katika vitu hivi:
(a)Inachukua miaka mingapi (minimum & maximum) kufikia kuvunwa?

(b)Inapandwaje (umbali kati ya mche na mche na umbali kati ya mstari na mstari?

(c)Mti mmoja ukikomaa baada ya hiyo miaka una uwezo wa kutoa mbao ngapi (minimum & maximum)?

(d)Mti mmoja una uwezo wa kutoa mbao za sh. ngapi kwa bei ya sasa (minimum & maximum)?

(e)Mti mmoja ukishakomaa unauzwa kwa bei gani (minimum & maximum) ili mnunuzi apasue mwenyewe?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom