BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 654
- 1,598
Kijana Mmoja mwenye umri wa miaka 35 ajulikanae kwa jina la Allen Malya anadaiwa kujinyonga hadi kufa kwa kutumia shuka lake, tukio hilo la kusikitisha limetokea katika Kitongoji cha Sereni Kijiji cha Usari, Kata ya Machame Narumu, Kilimanjaro.
Kaka Mkubwa wa marehemu ajulikanae kama Samora amesema alishtushwa na kitendo cha mdogo wake kutokuamka mapema kitu ambacho sio kawaida yake, hadi inafika saa nne asubuhi mlango wake ulikuwa haujafunguliwa ndipo alipoamua kwenda kucheki dirishani na kukuta marehemu akiwa ananing'inia na shuka shingoni, akaita majirani na baadaye polisi walifika na kuchukua miwili wake.
Hata hivyo, mwenyekiti wa kijiji hicho, Wilfred Maiko amesema kuwa hili ni tukio la mtu wa nne kujinyonga ndani ya Kijiji chake ndani ya mwaka mmoja na nusu na katika matukio yote hayo manne waliojinyonga wote ni vijana wa kiume.
Kaka Mkubwa wa marehemu ajulikanae kama Samora amesema alishtushwa na kitendo cha mdogo wake kutokuamka mapema kitu ambacho sio kawaida yake, hadi inafika saa nne asubuhi mlango wake ulikuwa haujafunguliwa ndipo alipoamua kwenda kucheki dirishani na kukuta marehemu akiwa ananing'inia na shuka shingoni, akaita majirani na baadaye polisi walifika na kuchukua miwili wake.
Hata hivyo, mwenyekiti wa kijiji hicho, Wilfred Maiko amesema kuwa hili ni tukio la mtu wa nne kujinyonga ndani ya Kijiji chake ndani ya mwaka mmoja na nusu na katika matukio yote hayo manne waliojinyonga wote ni vijana wa kiume.