Kila mwanamke ninayemfuata

Kila mwanamke ninayemfuata

pombe kali

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2014
Posts
312
Reaction score
614
Heri ya Mwaka mpya wana Jamvi wote.

Mimi ni kaka ninaye anza kutimiza miaka thelathini tangu kuzaliwa kwangu.Sasa kiukweli nimebahatika kupata kakibarua sehemu fulani huku Mjini.sasa naamini ni wakati muafaka wa mimi kutafuta mwenza wa Maisha.

Nimechelewa kidogo, tatizo linakuja pale ambapo najaribu kuwafuata wasichana kila ninaye mueleza azma yangu ananiambia pole kaka nishawahiwa na wengine wanadiriki kunitukana matusi . Ni idadi kubwa sana ya wasichana nimewafuata bila mafanikio sura yangu ni ya kawaida tu haitishi ingawa nina kovu kidogo kwenye paji la uso.

Nimekuwa mpweke sana na hii imepelekea niwe mwanachama mzuri wa kimboka kona bar na sehemu zingine kama hizo, naona ndoa kwenye vyombo vya habari wanandoa wana pendeza kweli kweli nimekija humu kuombaushauri wenu ninakosea wapi.
 
Labda unawatongoza kwa kuonesha uharaka wa kutaka kila jambo lifanyike ndani ya muda mfupi. Usiwe mkweli sana hutoaminika weka na uwongo kwenye tongoza zako utawanasa. Ukweli ukizidi sana unakuwa hauna hamasa.
 
mkuu hili swala la sie boys kukosa wadada ndio kwanza nalisikia kwako mie nimewapanga kama watano wote kila mmoja anajihisi ntamuoa hao five ni wale uhakika bado wale chapa ilale kwa kweli wadada ni wengi usipende kuwa mkweli sana utongozapo na pia wakati unafukuzia fata kama hutaki vile yani asijue uko deep that means usi care sana then being smart all in all mwanaume sio sura height na confidence ladies ndo wanaangalia sana na mpunga haswa kwa hapa town dar
 
kheri ya mwaka mpya wana jamvi woote...mimi ni kaka ninaye anza kutimiza miaka thelathini tangu kuzaliwa kwangu ....sasa kiukweli nimebahatika kupata kakibarua sehemu fulani huku mjini....sasa naamini ni wakati muafaka wa mimi kutafuta mwenza wa maisha tho nimechelewa kidogo, tatizo linakuja pale ambapo najaribu kuwa fuata wasichana kila ninaye mueleza azma yangu ananiambia pole kaka nishawahiwa na wengine wanadiriki hata kunitolea matusi kiukweli ni idadi kubwa sana ya wasichana nimewafuata bila mafanikio sura yangu ni ya kawaida tu haitishi ingawa nina kovu kidogo kwenye paji la uso ....nimekuwa mpweke sana na hii imepelekea niwe mwanachama mzuri wa kimboka kona bar na sehemu zingine kama hizo....huwa naona ndoa kwenye vyombo vya habari wanandoa wana pendeza kweli kweli nimekija humu kuombaushauri wenu ninakosea wapi?

Kwani hata huko Kimboka hujapata Wa kuoa? Mkuu kama huku mtaani umekosa chukua huko huko ulikozoea!
 
Hata mimi nashangaa, wengine tunafuatwa na wanawake kama nyuki mpaka napata tabu kuchagua... wengine hawapati. Makubwaaaaa!!!
 
mkuu hili swala la sie boys kukosa wadada ndio kwanza nalisikia kwako mie nimewapanga kama watano wote kila mmoja anajihisi ntamuoa hao five ni wale uhakika bado wale chapa ilale kwa kweli wadada ni wengi usipende kuwa mkweli sana utongozapo na pia wakati unafukuzia fata kama hutaki vile yani asijue uko deep that means usi care sana then being smart all in all mwanaume sio sura height na confidence ladies ndo wanaangalia sana na mpunga haswa kwa hapa town dar

mmmmmh!
 
nensa kwenye kanisa lolote la kilokole utawaona wanavyolia na kusaga kuomba kuolewa.
 
mbona mademu wapo wengi sana dar! usipende kuwa mkweli unapo kuwa unawatongoza! tatizo hujiamini mbona kitaani tunawaona wenye sura ngumu zilizo jaa mikovu lakin wanaopoa mademu wakali! au hujawahi kuona wake za vigogo wakitembea na waokota makopo au watch man
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom