Kila mtu ana malaika wake amlindaye

Kila mtu ana malaika wake amlindaye

Lucky One

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2013
Posts
663
Reaction score
431
Habari zenu wanajamvi wa humu "Kila mtu ana malaika wake amlindaye" ni maneno kauli ambayo nimeisikia katika nyumba za ibada na ndani ya jamii na tangu nimesikia kauli hii mara nyingi nimekuwa nikiwaza kuhusu jambo hili kwamba kama ni kweli kwanini hatuwezi kuongea na hawa walinzi, kuwaona au hata wengine kuhisi uwepo wao.

Nimekuja kutambua kwamba hawa malaika wapo na huenda ndo chanzo cha watu kuwa na bahati za kunusurika katika ajali,bahati za kupendwa na watu ,bahati za mafanikio katika kazi ,biashara na maisha kwa ujumla n.k

Pia katika uzoefu wangu nimegundua kwamba hawa malaika wapo wa aina mbili kuna wale ambao hujidhihirisha kwa watu wanaowalinda na wale ambao huwahawajidhihirishi.

Wale ambao hujidhirisha ni kwamba yule mtu anakuwa anahisi uwepo wao mfano nina rafiki yangu huwa anahisi kitu kibaya kitatokea hata kabla hakijatendeka aliwahikutusihi tusipande basi fulani na kweli lile basi lilipata ajali na kuuwa watu kadhaa tukabaki tukishangaa jinsi gani alivyoweza tabiri.

Wengine wakisema jambo hutokea kama walivyosema na wengine hujua nini kitatokea keshoNa kundi la pili ni wale ambao hawajidhihirishi kwa watu wao hivyo watu huishi bila kuhisi au kufahamu uwepo waoKama kuna mtu ana maarifa zaidi juu ya jambo hili atuarifu na sisi wengine tuelewe zaidi, uwanja ni wenu sasa.
 
Kwa hiyo na wale albino wanaouwawa au kujeruhiwa, watu wanaobakwa, kufa kwa ajali ya gari, kuungua moto, nk, wao hao malaika wao walinzi wanakuwa wameenda wapi, lunch break au malaika wa Ibilisi wamewapa kitu kidogo ili wasilinde watu wao japo kwa muda mfupi? Maana usije ukawapa viongozi wetu kisingizio kwamba hata malaika wanafanya uzembe na kuchukua kitu kidogo katika kutekeleza majukumu yao
 
Unatafuta kesi ya makusudi na Kiranga.

Jamii iliyokosa elimu na hivyo kukosa namna ya kujibu maswali kwa uchunguzi, itajaribu kujibu maswali kwa hekaya, ngano na hadithi zisizo uchunguzi wa kiushahidi wa mantiki.

It is a coping (not to be confused with copying) mechanism universal to human beings.

I suspect we may be able to find alien life with the same traits.

But that also could be coping mechanism for not being able to tell.
 
Last edited by a moderator:
Jamii iliyokosa elimu na hivyo kukosa namna ya kujibu maswali kwa uchunguzi, itajaribu kujibu maswali kwa hekaya, ngano na hadithi zisizo uchunguzi wa kiushahidi wa mantiki.

It is a coping (not to be confused with copying) mechanism universal to human beings.

I suspect we may be able to find alien life with the same traits.

But that also could be coping mechanism for not being able to tell.

Kwa thread hii na maudhui yake, nakubalia na wewe mkuu kwa 100%.
 
Habari zenu wanajamvi wa humu "Kila mtu ana malaika wake amlindaye" ni maneno kauli ambayo nimeisikia katika nyumba za ibada na ndani ya jamii na tangu nimesikia kauli hii mara nyingi nimekuwa nikiwaza kuhusu jambo hili kwamba kama ni kweli kwanini hatuwezi kuongea na hawa walinzi, kuwaona au hata wengine kuhisi uwepo wao.

Nimekuja kutambua kwamba hawa malaika wapo na huenda ndo chanzo cha watu kuwa na bahati za kunusurika katika ajali,bahati za kupendwa na watu ,bahati za mafanikio katika kazi ,biashara na maisha kwa ujumla n.k

Pia katika uzoefu wangu nimegundua kwamba hawa malaika wapo wa aina mbili kuna wale ambao hujidhihirisha kwa watu wanaowalinda na wale ambao huwahawajidhihirishi.

Wale ambao hujidhirisha ni kwamba yule mtu anakuwa anahisi uwepo wao mfano nina rafiki yangu huwa anahisi kitu kibaya kitatokea hata kabla hakijatendeka aliwahikutusihi tusipande basi fulani na kweli lile basi lilipata ajali na kuuwa watu kadhaa tukabaki tukishangaa jinsi gani alivyoweza tabiri.

Wengine wakisema jambo hutokea kama walivyosema na wengine hujua nini kitatokea keshoNa kundi la pili ni wale ambao hawajidhihirishi kwa watu wao hivyo watu huishi bila kuhisi au kufahamu uwepo waoKama kuna mtu ana maarifa zaidi juu ya jambo hili atuarifu na sisi wengine tuelewe zaidi, uwanja ni wenu sasa.

Ni kweli kabisa bwana mkubwa,kila mtu ana malaika wanaomlinda isipokuwa ni kwamba mtu ukiwa wa sala sana ni rahisi sana kuonja hiyo hali uliyoielezea,umeongelea kuwa kwanini hatuwezi kuongea nao,jibu ni kwamba hao ni viumbe waliopo ktk ulimwengu wa Roho,hivyo ili kuongea nao ni kupitia sala,mtu anaye sali sana kwa imani ni rahisi kuomba hitaji fulani na kisha kujibiwa,lakini km siyo mtu wa sala ni vigumu kuonja uwepo wao;Kwa hakika na kweli kabisa hawa malaika walinzi hutuepusha dhidi ya hatari mbalimbali.kwa uelewa zaidi jitahidi kusoma sana BIBLIA ili kujua namna hawa malaika walivyo busy kutulinda sisi wanadamu,kumbuka kuwa hawa ni wajumbe wa MUNGU.
NB:Yapo mambo yanafanya mtu aonje nguvu itokanayo na malaika walinzi,nayo ni;Sala,matendo mema,kujiweka karibu
na MUNGU,n.k.Mambo yanayofanya mtu asionje nguvu hiyo ya malaika walinzi na wakati mwingine kujikuta akiingia ktk
hatari bila ulinzi wowote,ni pamoja na;Kutopenda kusali,kuzama sana ktk malimwengu,kuwa mbali na MUNGU,n.k.Aidha
dhambi za mauti,km vile kuua,ujambazi,utoaji mimba,n.k.huathiri kwa kiwango kikubwa mahusiano yetu ya kiroho na
malaika wetu walinzi hivyo kujiona km hatuna hao malaika.
 
Kwa hiyo na wale albino wanaouwawa au kujeruhiwa, watu wanaobakwa, kufa kwa ajali ya gari, kuungua moto, nk, wao hao malaika wao walinzi wanakuwa wameenda wapi, lunch break au malaika wa Ibilisi wamewapa kitu kidogo ili wasilinde watu wao japo kwa muda mfupi? Maana usije ukawapa viongozi wetu kisingizio kwamba hata malaika wanafanya uzembe na kuchukua kitu kidogo katika kutekeleza majukumu yao
tusubiri tupate majibu kwa wanaojua
 
tusubiri tupate majibu kwa wanaojua
Hayo majibu utasubiri hadi jua litoke kusini kwenda kaskazini sababu hamna aliyemuona malaika, afu hiyo idea sijui umeitoa wapi, hehehe! kama malaika wanatupa kazi bac maskini wacngekuwepo
 
Hayo majibu utasubiri hadi jua litoke kusini kwenda kaskazini sababu hamna aliyemuona malaika, afu hiyo idea sijui umeitoa wapi, hehehe! kama malaika wanatupa kazi bac maskini wacngekuwepo
Huenda ni kweli huwezi kumwona malaika lakini hawa malaika wapo wanatulinda na adha mbalimbali katika maisha na kwa watu wengine malaika hawa huwa ndio sababu za wao kuwa na bahati katika maisha,biashara au kazi
 
Huenda ni kweli huwezi kumwona malaika lakini hawa malaika wapo wanatulinda na adha mbalimbali katika maisha na kwa watu wengine malaika hawa huwa ndio sababu za wao kuwa na bahati katika maisha,biashara au kazi

Mkuu mimi nakubaliana na wewe, Malaika wapo lakini na shetani yupo. Mimi juzi nilipark sehemu gari yangu, sasa nafsi yangu ikawa inaniambia hiyo gari iondoshe iweke sehemu nyengine (nafikiri ndio huyo Malaika). Basi wakati huo huo upande wa pili ukaniambia hauna haja ya kuondosha utajipa tabu bure (nafikiri ni huyo shetani). Mimi nikaona kua haina haja nikaiwacha. Jioni yake bwana ile gari ikaja ikagongwa na mtu wakati iko hapo na jamaa akakimbia. Laiti ningesikiliza ile nafsi ya mwanzo, but its too late.
 
Hayo majibu utasubiri hadi jua litoke kusini kwenda kaskazini sababu hamna aliyemuona malaika, afu hiyo idea sijui umeitoa wapi, hehehe! kama malaika wanatupa kazi bac maskini wacngekuwepo

Malaika walinzi wapo na hali kadhalika malaika wabaya wanazungukazunguka pia. Ukaribu na malaika wako hutegemea maisha yako ya kiimani. Unapaswa kuwa mtu wa sala, imani thabiti na matendo mema.

Kuongea na malaika wako ni shauri lako mwenyewe, kama unataka utaongea naye naye atakujibu kwa namna mbalimbali kupitia ishara na hata kwa sauti inayosikika endapo itabidi. Lakini hapa unahitaji kuwa deep in faith isivyo kawaida, lakini yawezekana.

Malaika wako yupo karibu na wewe kuliko mpenzi wako wa dhati na anajua maisha yako na yale yote yanayokuzunguka kulliko wewe mwenyewe ujuavyo.

Malaika wako atakulinda kulingana na jinsi wewe ulivyokuwa connected na Muumba wako na kuishi kadiri ya njia za Mungu.

Kumbuka kwamba ukijiingiza katika dhambi umejiingiza kwenye ufalme wa shetani na lolote laweza kutokea kwani wewe mwenyewe umejiweka katika himaya ya shetani na unakuwa katika hali ya hatari kudhurika kutokana na majini na maajenti wa shetani ambao ni wanadamu wanaozunguka kiroho wakishirikiana na malaika wabaya kukutafuta ili wakuangamize

Kila wakati sali na ongea na Yesu Kristo naye ataongea na wewe moja kwa moja au hata kupitia malaika wako.

Kumbuka hakuna neno lolote utakaloomba kwa Yesu kwa Jina lake bila Yeye kulisikia na kujibu.

Kupokea ulichoomba inategemea sana hali yako kiimani na ukaribu na Mungu. Unapaswa kukuza imani yako kwa kuanza kuomba mambo madogomadogo na ukishapokea omba makubwa na endelea kuomba makubwa zaidi. Imani inakuwa kama ambavyo ujuzi ukuavyo.
 
Malaika walinzi wapo na hali kadhalika malaika wabaya wanazungukazunguka pia. Ukaribu na malaika wako hutegemea maisha yako ya kiimani. Unapaswa kuwa mtu wa sala, imani thabiti na matendo mema.

Kuongea na malaika wako ni shauri lako mwenyewe, kama unataka utaongea naye naye atakujibu kwa namna mbalimbali kupitia ishara na hata kwa sauti inayosikika endapo itabidi. Lakini hapa unahitaji kuwa deep in faith isivyo kawaida, lakini yawezekana.

Malaika wako yupo karibu na wewe kuliko mpenzi wako wa dhati na anajua maisha yako na yale yote yanayokuzunguka kulliko wewe mwenyewe ujuavyo.

Malaika wako atakulinda kulingana na jinsi wewe ulivyokuwa connected na Muumba wako na kuishi kadiri ya njia za Mungu.

Kumbuka kwamba ukijiingiza katika dhambi umejiingiza kwenye ufalme wa shetani na lolote laweza kutokea kwani wewe mwenyewe umejiweka katika himaya ya shetani na unakuwa katika hali ya hatari kudhurika kutokana na majini na maajenti wa shetani ambao ni wanadamu wanaozunguka kiroho wakishirikiana na malaika wabaya kukutafuta ili wakuangamize

Kila wakati sali na ongea na Yesu Kristo naye ataongea na wewe moja kwa moja au hata kupitia malaika wako.

Kumbuka hakuna neno lolote utakaloomba kwa Yesu kwa Jina lake bila Yeye kulisikia na kujibu.

Kupokea ulichoomba inategemea sana hali yako kiimani na ukaribu na Mungu. Unapaswa kukuza imani yako kwa kuanza kuomba mambo madogomadogo na ukishapokea omba makubwa na endelea kuomba makubwa zaidi. Imani inakuwa kama ambavyo ujuzi ukuavyo.

Amina amina amina
 
Habari zenu wanajamvi wa humu "Kila mtu ana malaika wake amlindaye" ni maneno kauli ambayo nimeisikia katika nyumba za ibada na ndani ya jamii na tangu nimesikia kauli hii mara nyingi nimekuwa nikiwaza kuhusu jambo hili kwamba kama ni kweli kwanini hatuwezi kuongea na hawa walinzi, kuwaona au hata wengine kuhisi uwepo wao.

Nimekuja kutambua kwamba hawa malaika wapo na huenda ndo chanzo cha watu kuwa na bahati za kunusurika katika ajali,bahati za kupendwa na watu ,bahati za mafanikio katika kazi ,biashara na maisha kwa ujumla n.k

Pia katika uzoefu wangu nimegundua kwamba hawa malaika wapo wa aina mbili kuna wale ambao hujidhihirisha kwa watu wanaowalinda na wale ambao huwahawajidhihirishi.

Wale ambao hujidhirisha ni kwamba yule mtu anakuwa anahisi uwepo wao mfano nina rafiki yangu huwa anahisi kitu kibaya kitatokea hata kabla hakijatendeka aliwahikutusihi tusipande basi fulani na kweli lile basi lilipata ajali na kuuwa watu kadhaa tukabaki tukishangaa jinsi gani alivyoweza tabiri.

Wengine wakisema jambo hutokea kama walivyosema na wengine hujua nini kitatokea keshoNa kundi la pili ni wale ambao hawajidhihirishi kwa watu wao hivyo watu huishi bila kuhisi au kufahamu uwepo waoKama kuna mtu ana maarifa zaidi juu ya jambo hili atuarifu na sisi wengine tuelewe zaidi, uwanja ni wenu sasa.
Vitu kama hivi kuamini vinataka some experience personal I believe in this 100% based on experience na naamini wazazi sanasana mama ni guardian angel akiwa mzima au marehemu.

Yaani uwa navyotokaga katika mdomo wa mamba anajua mungu tu saa zingine, mtu mmbaya akiwa karibu na maisha yangu nitaonyeshwa tu sababu kwa njia moja ama nyingine ni mimi kuamua how i deal with him na kama mtu ana nia ya kunidhuru immediately itatokea tu situation au mtu atakae vuruga aisee kuna nguvu zaidi yetu inataka experience.

Love you mum wherever you are kwa sasa.
 
Usiumizwe Kichwa Na Mpumbavu Asiyemjua Mungu.

heshimu imani ya mwenzio usilazimishe unachoamini wewe ndo kila mtu aamini hivyo.

Kama hafanyi matendo maovu na haamini uwepo wa mungu yupo sahihi.

na wewe unayeamini uwepo wa mungu upo sahihi pia!
 
Hayo majibu utasubiri hadi jua litoke kusini kwenda kaskazini sababu hamna aliyemuona malaika, afu hiyo idea sijui umeitoa wapi, hehehe! kama malaika wanatupa kazi bac maskini wacngekuwepo

uwepo wa maskini ni kutokana na uwezo wao finyu wa kufikiri vinginevyo maskini hawatakiwi kuwepo!
 
Back
Top Bottom